KITABU kinachozungumzia kashfa ya kihistoria ya ununuzi wa rada, uliowahusisha aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Andrew Chenge na aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT) Dk. Idriss Rashidi, tayari kimeingia nchini.

Ndani ya kitabu hicho, kilichokuwa kikusubiriwa na wengi kiingie nchini, kinachoitwa The Shadow World Inside The Global Armrs Trade, Mtunzi Andrew Feinstein ameeleza kwa kina mchakato ulivyoendeshwa, ukiwahusisha watu wa madaraka na kada mbalimbali ambao ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair.


Kitabu cha kashfa ya Rada na mtunzi wake

Andrew Feinstein

Tony Blair anatajwa katika kitabu hicho kuwa ndiye aliyemshawishi aliyekuwa Rais wa Tanzania wakati huo, Benjamin Mkapa, kununua rada hiyo kutoka kampuni ya kutengeneza silaha ya Uingereza BAE-Systems.

Tanil Somaiya

Sailesh (Shailesh) Vithlani

Pamoja na hao, wanatajwa wafanyabiashara wenye asili ya India, lakini ambao wanaishi/walipata kuishi Tanzania, Tanil Somaiya ambaye alikuwa akimiliki kampuni ya uwakala wa simu ya Shivacom na Sailesh (Shailesh) Vithlani, kuwa watu wa kati wa biashara hiyo.Kuibuka kwa kitabu hicho kunaongezea tu katika taarifa za awali zilizopata kuchapishwa na kutangazwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini kuhusu ununuzi wa rada hiyo ambao ulipingwa sana si tu ndani ya Tanzania, bali hata Benki ya Dunia na Uingereza kwenyewe.

Wakati huo aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa, Clare Short, alikataa katakata Tanzania, moja kati ya nchi masikini kabisa duniani, kutumia mabilioni ya fedha kununua rada katikati ya umasikini unaonuka.

Anasema mwandishi wa kitabu hicho katika sehemu moja ya maandishi yake: “Wakati akipigia chapuo, Tume yake ya Afrika (Commission for Africa) juu malengo ya kuwa na utawala bora katika Afrika, Tony Blair alimshawishi Rais wa Tanzania, moja ya nchi masikini kabisa duniani kununua rada ya kijeshi kwa bei ya zaidi ya dola za Marekani milioni 40.

Wakati huo Tanzania ilikuwa na ndege nane tu za kivita, nyingi zikiwa katika hali mbovu kiasi cha kuzifanya zisitengenezeke. Rushwa ya karibu dola za Marekani milioni 10 inadaiwa ililipwa kwenye mpango huo.”

Kwa mujibu Andrew Feinstein, akiba ya dhahabu iliyohifadhiwa katika BoT ambayo, hata hivyo, thamani yake halisi haijafahamika, ndiyo iliyotumika kufadhili upatikanaji wa mabilioni ya fedha kwa njia ya mkopo kutoka Benki ya Barclays, ili kufanikisha ununuzi wenye utata wa rada ya kijeshi.

Katika taratibu za benki kuu mbalimbali duniani, dhahabu imekuwa ikihifadhiwa kama moja ya njia za nchi husika kujimudu dhidi ya mitikisiko ya kiuchumi. Tanzania ni kati ya nchi inayotumia mfumo huo wa kuhifadhi dhahabu.

Mwandishi huyo anasema katika kitabu hicho kwamba Dk. Idriss ndiye aliyekuwa kiungo muhimu katika kufanikisha mkopo kutoka Benki ya Barclays kwa masharti kuwa dhamana iwe akiba ya dhahabu iliyoko katika Benki Kuu ya Tanzania.

Bila kutaja thamani halisi ya akiba hiyo lakini akitaja kiwango cha mkopo husika, Andrew Feinstein anasema: “Katika mchakato huo, Dk. Idriss ndiye aliyekuwa na jukumu la kuidhinisha malipo hayo ya ununuzi wa rada (akiwa Gavana wa Benki Kuu), kwa masharti kwamba Benki ya Tanzania iweke dhamana akiba yake ya dhahabu ili mkopo (wa ununuzi rada) upatikane.

Feinstein anaeleza pia kwamba bosi huyo wa BoT ndiye aliyehakikisha michakato yote ya kifedha (malipo) inafanyika kwa mujibu wa sheria za Uingereza (zenye kinga katika michezo ya utoaji ‘chochote’ katika masuala ya ununuzi) na si sheria za Tanzania.

Mwandishi anasema Chenge, ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Fedha na Uchumi, anatajwa kuhusika kutoa ushauri wa kisheria (kwa wakati huo akiwa Mwanasheria Mkuu), ushauri ambao unatajwa kuzingatiwa katika hatua nyingine za uamuzi, ukiwamo uamuzi wa Benki ya Barclays kutoa mkopo wa ununuzi wa rada.

Inadaiwa kuwa ili kuhakikisha mkopo kwa ajili ya ununuzi wa rada unapatikana kutoka Benki ya Barclays, wakala wa ununuzi huo Sailesh Vithlani, aliwasilisha nakala ya maoni ya Mwanasheria Mkuu wa Tanzania (Chenge) katika Benki hiyo.


Andrew Chenge

Andrew Chenge

“Malipo yaliyofanywa kwenye akaunti ya Chenge yanalingana kikamilifu na uwasilishaji wa maoni yake (ya kisheria) kwa ajili ya kufanikisha upatikanaji wa mkopo na ununuzi wa rada.”

Kwa mujibu wa kitabu hicho, mazingira hayo ya ushiriki wa Chenge kwa njia ya kutoa ushauri wa kisheria yanathibitishwa na mawakili wake wa kimataifa, walioko Marekani pamoja na Uingereza ambao baada ya kuhojiwa walikiri ushiriki huo wa Chenge.

Namna walivyochota mamilioni

Inaelezwa kuwa kwa mujibu wa rasimu ya ripoti ya SFO (Taasisi ya Uchunguzi Makosa ya Jinai ya Uingereza), Chenge alipokea malipo ya jumla ya dola za Marekani milioni 1.5 (zaidi ya bilioni 1.5) kati ya Juni 1997 na Aprili 1998 kutoka Benki ya Barclays, tawi la Frankfurt.

Fedha hizo zililipwa katika benki ya Barclays huko Jersey - Uingereza, katika akaunti inayomilikiwa na kampuni iliyotajwa kwa jina la Franton Investment Limited. Kampuni hiyo imetajwa kumilikiwa na Chenge, ikiwa ni maalumu kwa ajili ya uhamishaji fedha kiasi cha dola za Marekani 600,000 (zaidi ya Sh milioni 600).

Maelezo zaidi katika kitabu hicho yanabainisha kuwa, dola hizo 600,000 za Marekani zilihamishwa kutoka kwenye akaunti ya kampuni ya Chenge kwenda kwenye akaunti nyingine, inayomilikiwa na Kampuni ya Langley Investments Ltd, iliyokuwa ikiendeshwa na Dk. Idrissa Rashidi (aliyewahi pia kuwa Mkurugenzi wa TANESCO).

Katika kitabu hicho, Feinstein ambaye aliwahoji washiriki mbalimbali wa sakata hilo, wakiwamo baadhi ya maofisa wa upelelezi nchini anasema: “Septemba 20, mwaka 1999, Chenge binafsi aliidhinisha uhamishaji wa dola za Marekani milioni 1.2 (zaidi ya Sh bilioni 1.2) kutoka akaunti ya kampuni (yake) ya Franton kwenda Royal Bank of Scotland International, huko Jersey.

Namna BAE ilivyojipenyeza

Mwaka 1997, kampuni ya BAE ilinunua kampuni iliyojulikana kama Siemens Plessey Systems (SPS) ambayo ilikuwa katika mchakato wa mapatano ya kibiashara na Serikali ya Tanzania tangu mwaka 1992 kwa ajili ya mauzo ya rada.

Kama sehemu ya makubaliano katika kuinunua kampuni ya Siemens Plessey Systems (SPS), BAE ilikubali kuendelea kumtumia wakala wa SPS, Sailesh (au Shailesh) Vithlani. Katika mazingira hayo, Sailesh aliomba kufanyike marekebisho kuhusu ahadi zake kwa maofisa wa Serikali ya Tanzania.

Hali hiyo inatokana na ukweli kwamba, ‘dili’ la mwanzo ambalo lingefanikisha biashara ya pauni za Uingereza milioni 110 lilizuiwa na Benki ya Dunia pamoja na Chombo mahsusi cha Uingereza cha kusimamia masuala ya maendeleo (Uk’s overseas Development Administration).

Uingiliaji wa Waziri Clare Short

Mwaka 2000, dili ikaibuka upya na safari hii kampuni ya BAE ikiligawa mradi (dili) huo katika awamu mbili ili kuunfanya uonekane ni mradi nafuu, lakini Clare Short, aliyepata kuwa Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa alipinga mpango huo.

Upinzani huo ulihusisha hoja mbalimbali ambazo ni pamoja na mchakato mzima wa ununuzi umegubikwa na utata na kubwa zaidi, teknolojia ya rada hiyo imekwishapitwa na wakati. Hoja nyingine ni kwamba, Tanzania haina na shida na rada hiyo na badala yake, kilichokuwa kikihitajika ni rada ya ‘kiraia’ kwa ajili ya kuboresha huduma za anga na hasa kwa kuitazama sekta ya utalii.

Hata hivyo, licha ya upinzani wote huo kutoka kwa Waziri Clare Short na Waziri mwenzake wa Mambo ya Nje wa Uingereza kwa wakati huo, Robin Cook, mpango wa ununuzi wa rada uliendelea mwaka 2001 kwa BAE System kuiuzia Tanzania rada kwa thamani ya pauni za Uingereza milioni 28.

Katika hali ya kupinga mchakato wa ununuzi wa rada hiyo, Oktoba, mwaka 2001 ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya Usalama wa Anga (ICAO), ilieleza kasoro katika ununuzi wa rada hiyo ya kijeshi.

Ripoti hiyo inanukuliwa ikisema; “Rada inayonunuliwa ni kwa ajili ya shughuli za kijeshi na kwa hiyo, haitakuwa na msaada mkubwa kwa shughuli za anga kwa ajili ya ndege za kiraia. Mpango wa ununuzi wa rada hiyo si sahihi na ni wa gharama mno.”

Kutokana na ripoti hiyo, Kampuni ya BAE iliishushia lawama ICAO kwamba imetoa taarifa za uongo na hasa kwa upande wa gharama za uuzaji.

Lakini wakati BAE na ICAO wakiingia katika malumbano, Msemaji wa Benki ya Dunia alitoa tamko akisema; “Matumizi hayo ya fedha (ununuzi) hayako wazi, yana utata mkubwa.”

Tafsiri iliyotolewa ni kwamba, bajeti ya dola za Marekani milioni 40 kwa ajili ya ununuzi wa rada hiyo ni sawa na theluthi moja ya bajeti ya elimu nchini Tanzania na kwa hiyo, ni kiwango kikubwa cha fedha ambacho kinakinzana na vipaumbele vya kibajeti vya Tanzania, kama elimu na afya.

Wengi walipata kuzungumzia sakata hilo la ununuzi wa rada wa karibuni kabisa akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambaye alisema katika mkutano na waandishi wa habari kwamba angezungmzia suala hilo kwa kutaja wahusika wakati wa kuwasilisha bajeti ya wizara yake akijibu hoja za wabunge waliokuwa wanataka wahusika watajwe hadharani na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Huko nyuma Chenge mwenyewe alipata kuzungumzia suala hilo, na hasa, kumiliki kwake kwa akaunti za fedha nyingi nje ya nchi yeye akiwa kama mtumishi wa umma.

Akiwajibu waandishi wa habari wakati wa safari yake moja ya kurejea nchini, Chenge alisema fedha hizo zilikuwa ni vijisenti tu, kauli ambayo iliwatibua wengi wa Watanzania ambao shilingi kwao ilikuwa imeota matairi.

Na katika hatua nyingine wakati huo, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Edward Hosea alipata, mara mbili, kunukuliwa akisema Chenge hakuwa na kesi ya kujibu katika kashfa hiyo ya rada.

Kitabu hiki kimetua nchini katikati ya taarifa za ufisadi mwingine uliofanywa na Watanzania, wakiwamo wastaafu wa vyeo vya juu wanaotajwa kuwa wamefutika fedha zinazokadiriwa kuwa mabilioni ya shilingi katika akaunti za nchini Uswisi zinazotokana na migao ya rushwa.

Thanks to Gazeti la Raia Mwema na Uchambuzi makini

Pori la Akiba la hifadhi ya Taifa lililogeuzwa msitu mateso, mauaji Joseph Zablon


WENGI wamezoea kuuita Msitu wa Pande, lakini eneo hilo ni Pori la Akiba, lililopo kilometa 25 kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam katika Barabara Kuu kuelekea mji wa Bagamoyo.

Pori hilo la Akiba linamilikiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, lilitangazwa kuwa la akiba mwaka 1952.
Ili kufika Msitu wa Pande kutokea katikati ya mji, utalazimika kuteremkia kituo cha daladala cha Bunju ‘B’.

Kutoka hapo kuna daladala zisizo rasmi na pikipiki (bodaboda), ambazo zinasafirisha abiria kwa kutumia barabara inayoanzia eneo hilo kupitia katikati ya msitu huo hadi eneo la Mbezi, Barabara Kuu ya Morogoro.

Pori hilo lina ukubwa wa ekari 1,226 na kilometa za mraba 15.
Lilipewa hadhi ya kuwa Pori la Akiba baada ya kuzingatia vigezo mbalimbali na tafiti tofauti kubaini kuwepo kwa viumbe hai na aina za mimea adimu, zisizopatikana maeneo mengine.

Msitu wa Pande unazungukwa na vitongoji vya Mpiji Magohe, Kibesa, Msakuzi na Mbopo.
Hata hivyo, katika miaka ya karibuni pori hilo limejipatia sifa mbaya ya kutumika kama kichaka cha kutesea watu, mauaji na vituko mbalimbali.

Sifa hiyo mbaya ya pori hilo ilianza kuvuma mwaka 2006 baada ya wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge, mkoani Morogoro kuuawa na polisi katika eneo hilo kwa kilichoelezwa kuwa walidhaniwa kuwa ni majambazi.

Baada ya hapo Tume iliundwa kuchunguza tukio hilo, ikabainika kuwa waliouawa hawakuwa majambazi.
Askari waliohusika na maujai hayo walifunguliwa kesi, ambayo ilivuta hisia za wengi kutokana na unyeti wake na mazingira ya tukio lenyewe.

Mbali ya vituko vya hapa na pale vinavyoshuhudiwa na kusimuliwa na majirani wa msitu huo, mwaka huu ikiwa miaka sita tangu kuuawa wafanyabiashara wa Mahenge, pori hilo limezizima tena, baada ya kiongozi wa madaktari, Dk Steven Ulimboka kutekwa, kuteswa na kisha kutelekezwa katika msitu huo.

Ama kweli damu ya mtu haiendi Bure .Baada ya Jana kuendelea kuangalia vyombo mbali mbali juu ya sakata la utesaji wa Daktari Ulimboka ,Joshua Mulindi(Mtesaji),Mchungaji Gwajima na Jeshi la Polisi kuna baadhi ya mambo ambayo kama watanzania tumeendelea kujiuliza maswali mengi sana.Je kuna usiri gani juu ya hili sakata na je ni yupi muhusika mkuu wa hii kitu (Master Mind) na Je hao watesaj wengine 14 ambao walikuwa na Joshua Mulindi(Mtesaji) mbona hawajatajwa mpaka leo au ndio hadithi zile zile za siku zote.

Jeshi la Polisi liliibuka kupitia Kamanda Kova kwa mara nyingine kuhusu swala hili likikemea kuhusu malumbano mbali mbali juu ya mjadala huu kati ya Taasisi za Dini za Kikristo na Jeshi la Polisi baada ya swala hili Kufikishwa katika Mahakama …Na haya ndio maswali ambayo tumekuwa tukijiuliza …


Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu Dar es Salaam,Suleiman Kova


  1. Je Katiba Katiba inasemaje Juu ya Kujadili swala ambalo limefikishwa mahakamani ,Je linaruhusu upande mmoja kutoa taarifa na kuuzuia mwingine kujibu ?
  2. Je katiba inasemaje kuhusu mtu unaporipoti kituo cha Polisi juu ya mtu ambaye analeta fujo kwenye eneo lako?Je anapokamatwa wewe uliyepeleka taarifa unakuwa mtuhumiwa au mshutumiwa bila kuulizwa au kupewa taarifa?
  3. Je kama kuna uthibitisho juu ya kile kinachodaiwa kuhusu mtuhumiwa(Kanisa la Ufufuo na Uzima) kwanini hakisemwi mpaka mtuhumiwa anapolalamika ndipo wewe ujibu tena kupitia vyombo vya habari ?
  4. Je ni upi uwezo wa intelijesia yetu juu ya mambo kama haya …..haswa hizi issue za kupika?...Wako wapi waliorudisha fedha za EPA?Au ndio funika kombe mwanaharamu apite?Hapa ndipo unapokuja usemi kwanini walioko jela wengi ni maskini?

….Kumbuka kuwa hata mara zote mtu mkimiya anaponyamaza sio kuwa hana cha kusema bali hutumia busara na uvumilivu…Muda unapofika uvumilivu ukafikamwisho ndio haya sasa tunayoyaona….

















Pastor Gwajima

Sintofahamu katika Sakata ya issue ya Dr. Ulimboka imechukua sura mpya Baada ya Siku ya Ijumaa Jeshi la Polisi kujitokeza kwenye vyombo vya habari na kueleza Kuwa Mtuhumiwa wa Sekeseke la kumkamata na Kumtesa Dr. Ulimboka amekamatwa baada ya kwenda katika kanisa la Ufufuo na Uzima lililo chini ya Mch. Gwajima, Mchungaji huyo wa Kanisa hilo amefunguka siku ya jana na kueleza kuwa “Joshua The Kenyan” hakuwahi kwenda kwenye Kanisa hilo na wala Kanisa halina Utaratibu wa Kuungama kwa kusema dhambi.

Taarifa zilizotolewa juzi na kuibua maswali katikati ya Jamii ya Watanzania hususan Wakristo waliozipokea taarifa hizo kuwa Mtuhumiwa huyo aliyefikishwa kizimbani siku ya Ijumaa Asubuhi Mr. Joshua Mulindi Kwa maelezo ya Kova anafanya kazi chini ya kundi la Gun Star lililo chini ya Mkuu wa Kundi hilo Bw. Silence kutoka Nchini Kenya Walikuwa Wamekodiwa kuja Tanzania na Kigogo Mmoja kuja nchini kwa kazi moja ya Kutoa uhai wa Dr. Ulimboka na zoezi hilo kushindikana, ndipo kijana huyo wa Kikenya alikwenda kunako kanisa la Pastor Gwajima na Kukiri kuhusika na sakata zima la Dr. Ulimboka.












Kamanda Sulemani Kova akitoa maelezo ya Kukamatwa Joshua Mulindi

Siku Ya Jana Mch. Gwajima amefunguka na kuruka Kimanga kuhusu sakata hilo na kutaka Kanisa hilo lisihusishwe na Sakata la Dr. Ulimboka sababu huyo mtu mwenye jina la Joshua kutoka nchini Kenya hajawahi kutubu kwenye Kanisa hilo na kueleza kuwa Kanisa lake halina utaratibu wa Kuungama kwa Kusema dhambi za waumini kama ilivyo katika Makanisa mengine hususan RC (Kuungama).

Mch. Huyo ambaye anaamini ana mahasimu wengi katika Gospel ameenda mbali zaidi na kusema kama Mkenya huyo ameeleza hayo basi atakuwa ametumwa na baadhi ya Watu wasioitakia mema huduma hiyo maarufu kwa kurejesha Misukule hapa Tanzania.











Dr. Ulimboka baada ya Kutoka kuteswa na Joshua the Kenyan

Pamoja na taarifa hizi muhimu Blog inakamilisha taarifa muhimu ya kulitazama sakata hili kwa jicho la tofauti kwa kutafuta utata wa maeneo yafuatayo.
  1. Je ni kweli Kabisa kwa Intelligencia ya jeshi la Polisi, baada ya kupokea tu taarifa kwa mtuhumiwa walikwenda kwenye vyombo bila ku cross check ukweli na Kanisa la Mch. Gwajima??
  2. Ni kweli Jeshi la Polisi halikujua kuwa Mch. Gwajima atakataa au waliamini Mch. Gwajima atafunika Kombe Mwanaharamu apite??Kwanini Walifikiri kuna njiab ya Uchochoro kupitia Kanisa hilo.
  3. Ni kweli Kanisa hilo kuanzia sasa wataendelea kusali kwa Amani katika viwanja vya Kawe bila kuanza kusikika tuhuma mbalimbali dhidi ya Kanisa hilo baada ya Mch. Kutia mchanga Kitumbua Cha Dola ya Serikali??
  4. Baada ya Kujisafisha Kwa Mch. Gwajima katika Sakata hilo, Je huyu Joshua kutoka Kenya ni nani hasa???
  5. Baada ya Sakata la Jerry Muro na Mengine yanayofanana na hayo ni Kweli Jeshi la Inteligensia ya Polisi imefikia hapo ilipo???

Kuna mambo mengi ambayo kwa jicho la tatu yataanza kuonekana baada ya Sakata hili linaloendelea la Dr. Ulimboka, Mgomo wa Madaktari, Joshua ze Kenyan, Kanisa la Gwajima na Kuhusika kwa Serikali katika Sakata zima.

Kanisa kwa namna moja limeamua kuangalia pia kweli inasemaje na kujiweka sawa, kama Serikali ilivyoamua kuwa LIWALO na LIWE, basi Pastor Gwajima nae ameamua kuwa LIWALO na LIWE katika Sakata la Kukamatwa Joshua Mulindi. Lazima Jeshi la Serikali nayo ijifunze kusoma Alama Za Nyakati lakini pia kama kuna issue za ku-cook (kupika) basi inatakiwa Intelligencia ya hali ya juu hasa kama issue itahusu mambo ya Imani Za Watu.

Efathaaaa, maaana yake "Funguka". Blog inakamilisha Makala Muhimu iliyoahidi mwishoni mwa wiki jana ili iweze fanya "EFATHA" ya Ukweli.

Thanks to my Brother Papaa The Blogger

1. The ultimate measure of a person is not where they stand in moments of comfort and convenience, but where the stand in times of challenge and controversy

2. The world has the habit of making room for the man whose words and actions show that he knows where he is going.

3. If you don't like something change it; if you can't change it — change the way you think about it

4. Live as if you were to die tomorrow. Learn as if you were to live forever

5. Change and growth take place when a person has risked himself and dares to become involved with experimenting with his own life.


ANDREW PALAU

International evangelist Andrew Palau is passionate about the life-changing power of Jesus Christ and is determined to share the Good News wherever God may call him. But it hasn’t always been this way.

Andrew grew up in a strong Christian home, one of four sons of world evangelist and author Luis Palau. Andrew, however, would choose his own way and did not make an early commitment to Jesus Christ. He attended the University of Oregon where the party life was a large part of his studies. After graduating with a degree in English literature, Andrew moved to Boston where he worked in retail for five years at the May Company.

In 1993, Andrew took vacation time to join his parents for Luis’ evangelistic outreach in Kingston, Jamaica. His father preached the same Gospel message he had heard him share hundreds of times, but this time it was different. Having witnessed God’s presence in the lives of some Jamaicans he met, including Wendy Levy whom he later married, Andrew gave his heart to the Lord after 27 years living apart from Him.

Not long after the Jamaica trip, Andrew returned to Portland, Oregon, to serve as Luis’ personal assistant while he determined which direction to take his career. He found he didn’t have far to go — he thrived when involved with his father’s outreach events.

Andrew was instrumental in crafting the content of the first Palau festivals that marked a key shift away from the crusade model for evangelism. The first two festivals were staged in the Palaus’ home base of Portland, Oregon, in 1999 and 2000. Before moving across the country to direct Washington DC’s event on the National Mall in 2005, Andrew directed festivals in Boise, Idaho, and South Florida.

Now Andrew preaches at his own festivals around the world from the United States to Rwanda, Romania, Egypt, Mexico, India, Poland, and Jamaica. He has shared the Gospel with millions of people, and at every opportunity he demonstrates his father’s same passion and love for Christ and for evangelism. In 2009, he joined Luis on his radio feature, Reaching Your World with Luis Palau. Andrew’s two-minute messages are broadcast on 855 radio outlets every Friday.

“There is power for change in Jesus Christ, the cross, His blood, His burial, and His resurrection,” says Andrew. “I long to see all people embracing His gifts of forgiveness of sins, the Holy Spirit to empower life, and the assurance of heaven for eternity.”

He and Wendy have three children, Christopher, Jonathan, and Sadie Anne. They live in Portland, Oregon, close to the world headquarters of the Palau ministry.

NAMNA YA KUFANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MAISHA

1.Kila siku tunafanya maamuzi mbali mbali juu ya maisha yetu.Maamuzi mengine ni rahisi sana na sa nyingine haya maswali sana.Mfano….Je umeshafanya homework au Umeshapika ?Lakini kuna mengine ni magumu mfano je nahitaji kuajiri watu wangapi na kwa nini ,Je nataka wawe na ujuzi kiasi gani n.k…Maamuzi rahisi marazote huwa na hatua rahisi za kuchukua kuliko maamuzi magumu kwenye maisha .

Ili kujua haya ni maamuzi magumu kwenye maisha ni vigezo gani vinaangaliwa ?

1.Kufokufahamu au kuto kujua vitu vingi kuhusu maamuzi unayotaka kuyachukua(Uncertainty)

2.Ugumu wa mamamuzi yenyewe unaoletwa na miingiliano ya vitu vingi(Complexity)

3.Athari unazoweza kupata baada ya kufanya maamuzi(High-Risk Consequences)

4.Njia mbadala ya kufanya maamuzi (Alternatives)

5.Je wengine watakuchukuliaje baada ya maamuzi (Interpersonal Issues)

….Pamoja na maswali yote magumu ambayo unaweza kujiuliza ili kukusaidia kufanya maamuzi magumu kwenye maisha ni kuchagua njia ambayo ni sahahi ya kufanya maamuzi .Njia sahihi ya kufanya maamuzi mara zote huleta matokeo bora na sahihi kwenye maisha .

Part 1.

1.There are two only countries in the entire world that do not Sell Coca-Cola ,North Korea and Cuba

2. Not getting enough sleep and being hungry are the 2 biggest reasons for being angry
3.Tobacco is the leading cause of death in America, much more than any other drug or alcohol. Yet, it's legal.
4.Before the 1930’s,Pink was for boys and blue a girls color




5.Listening to music can repair and make your immune system stronger