Maisha yetu ya kila siku ni mithili ya mapambano kuelekea jambo fulani kwenye kufikia hatma za maisha yetu.Kila siku tunafanya vitu mbali mbali kuweza kufikia hatma iliyo bora ya maisha yetu.Hakuna mtu anayependa kuwa na hatma mbaya kwenye maisha.Iwapo utafanikiwa hata kukaa na mlevi wa matapu tapu karibu akiwa amelewa chakari ukimuuuliza unataka kwenda jehanamu atakwambia hapana nataka kwenda mbinguni pamoja na ulevi alio nao.Wazuoni wachache siku za nyuma walisema Maisha ni Mapambano,Sehemu yeyote inayokuwa na mapambano maana yake ni vita baani ya pande mbili zinazotofautiana kimaslahi.Mmoja anaona anaonewa na mwingine anaona yuko sawa.

Ni hatari kuingia kwenye mapambano fulani bila kujua adui yako yukoje kwenye uwanja wa vita na pia ni hatari kutokulijua eneo la kupigani vita lakini pia silaha za kupigania vita na jeshi la aina gani linaweza kupigana vita.Unapokosa kujua vyote hivi ni rahisi kupoteza aina yeyote ya vita kwenye maisha yako.


Mara nyingi tumeingia kwenye mapambano bila kujua adui tunayepambana nao kwa wakati huo kwenye maisha yetu na kutupelekea sisi wenyewe kupapasa pasa kwenye kila jambo ambalo tunalifanya.Ni rahisi kwa mlokole kukemea pepo la umaskini na kuendelea kuomba bila kuchukua hatua fulani kwenye maisha.

Umaskini hautoki kwa maombi bali kwa kufanya kazi kwa bidii na bila kukataa tamaa na kufwata kanuni halali za kiutendaji.Ujinga ni tatizo kubwa kwenye jamii yetu juu ya adui ambaye tunafikiri tunapambana naye.Ni rahisi kupambana na CCM tukiwaona kama ni shida kumbe tatizo sio wao ni msingi mibovu ilojengwa tangu mwanzo wa uongozi na fikra zao.


Tunaweza kujua adui ambaye tunapambana naye kwenye maisha yetu ya kila siku ili kuweza kufikia hatma bora ya maisha ya kila siku lakini tatizo linakuja namna ya kujua eneo la mapambano,je ni jangwani au msituni au kwenye maji..??je kama ni jangwani je ramani ya jangwa hilo ikoje na kama ni msitu je msitu huo ukoje??

Ni muhimu kujua eneo ambalo utalitumia kama eneo la mapambano  ya vita vyako vya kila siku.Ni rahisi kwa mwanafunzi mpya wa chuo kujua course anayoifikiria kuisoma chuo lakini kipi ni chuo bora na chenye walimu bora juu ya course anayotaka kusoma.Unapokosa kujua battle ground yako ni bora usianzishe vita maana kuna uwezekano wa adui yako kukushinda maana eneo na uwanja wa vita ana ufahamu wa kutosha.


Silaha za kupia vita vyovyote inategemea na adui unayepigana naye na eneo ambalo mnalotumia kupigana vita.Ni ngumu kurusha makombora ya masafaa marefu zaidi ya kilomita 1500 kwa saa na huku ukiwa unapigana vita na Kisiwa cha Mafia.

Adui yako ndio anayekupa lead ya kwamba ni aina gani ya silaha utumie kupigana naye.Miaka ya mwanzo mwa 1990 tuliambiwa mtu akienda chuoni anapewa pesa lakini kutokana na wrong info basi tulijua mtu anapofika chuoni ni maisha ya burudani na raha lakini kumbe ni kinyume chale unapaswa kuweka jitihada zaidi.Kama ulikuwa ukikesha kusoma mara mbili kwa mwaka ulipokuwa Sekondari unapofika chuo kulala usiku wa manane ni jambo la kawaida tu lisilo na mjadala.Mara ya kwanza watu wengi hupata shida sababu hawakuelewa adai aliyeko mbele yao.


Kuna aina tofauti tofauti za department za jeshi linapofika swala la mapambano kwenye vita haiwezekani vita ikawa inapiganwa kwenye Eneo la Bahari wewe ukapeleka jeshi za miguu au vita ikapigana kwenye msitu wewe ukapelekea jeshi la maji.Kila sehemu inachagua aina gani ya jeshi unaloweza kulitumia kwenye mapambano ya vita vyako as long as umeshajua adui,eneo,silaha na pia unaweza kujua aina ya jeshi unaloweza kutumia kwenye uwanja wa mapambano.

Kwenye Jeshi kuna aina mbali mbali za wataalamu ni lazima ujue kama unaweza kutumia expert wachache tu na ukamaliza vita kwa upesi au unaweza ukatumia aina gani ya wataalamu kufikia hatma yako kwenye maisha.Maisha ni mapambano hakuna anayefikiri kushindwa lakini tangu mwanzo wa vita yeyote ni rahisi kujua yupi ni mshindi na yupi ni mshindwa.


.....Kupigana Vita usiyoijua nia Kucheza Kamali Karibu na Kituo cha Polisi.......
Hakuna kitu kilicho kirahisi kwenye maisha ya mwanadamu,Vyote vinahitaji nguvu ya ziada kuweza kufika malengo na kilele cha mafanikio binafsi.Unaweza kuona kitu kwa mtu kinaenda tu kwa njia nyepesi lakini hauwezi jua ameanzi wapi.Ukionacho leo ni Rahisi Kuna siku Kilishawahi kuwa Kigumu.

Kufikia malengo ya kimafanikio kwenye maisha kunahitaji nguvu,uwezo kujitoa na hata kuachana na vitu vingine ili kuweza kufikia maisha ya kimafanikio.
Wakati tunaanza darasa la Kwanza miaka ya nyuma tuliingia tukiwa hatujui kusoma wala kuandika kabisa lakini baada ya kujitoa na kufanya kwa bidii leo hii ukishika kitabu tuu unajua namna ya kusoma na kuandika.


1.Ni Rahisi Kuona Mafanikio Ya Mwingine na Ukayafurahia.

Hakuna jambo lilorahisi kufurahi kama kufurahia mafanikio ya mwingine bila kuja wapi alianzia na maamuzi gani alioyachukua.Sisi tunapoona matokeo ni rahisi kufurahia matokeo bila kutaka kujua mwanzo wa jambo ulikuwaje.
Miaka Michache iliyopita watu tulikuwa hatujui Precision Air lakini wanaojua historia ya Mzee Michael Shirima(Mwenyekiti wa Precision Air) wanaweza kuelewa nini Maana ya Kufilisika na Kurudi Kijijini na Kulima Kahawa na Ndipo Mtu anapata mwanga mpya wa kuanza kujaribu tena kuanza na wazo la kuwa mmiliki wa Kampuni ya Precision Air.
Leo hii sisi tunafurahia matokeo yake kwa kupanda ndege lakini kumbe kuna mtu alifilisika na akarudi kijijini na kuanza tena.Kufikia mafanikio inabidi uyashinde mazoea binafsi maishani mwako

2.Ni Rahisi Kukosoa Mafikio ya Mtu kuliko Kuanza ya Kwako.

Moja ya kipaji ambacho tunacho watu tulio wengi ni cha Kukosoa,Mtu anapoona mwenzake anapiga hatua baada ya kumsaidia kuboresha hatua zake kuweza kufikia mafanikio yake tunaanza kukisoa angefanya hiki au kile alafu unakaa pembeni ukisubiri aanguke uanze kusema nilitabiri mithili ya Nabii fulani.

Hakuna kitu kiachoaanza kikiwa chepesi.Kila ukionacho leo ni Rahisi  Kuna Siku Kilishawahi Kuwa Kigumu .
Hakuna urahisi kwenye jambo lolote wahenga walisema Siku zote Mwanzo ni Mgumu na Njia iendayo uzimani ni Nyembamba na Imesonga.
Ni rahisi sana kuanza kusema vibaya mafanikio ya mwingine kuliko kuweza kuanza ya kwako na ikafikia kipindi ukajivunia.
Mtu shujaa na mwenye mafanikio ya kweli ni yule anayechukua changamoto anazokutana nazo na kuweza kuzitumia kujijenga na kusonga mbele.Kama haukuwahi kukosea juu jambo lolote base tambua haukuwahi kujaribu kufanya kitu siku zote maishani mwako.

 Hakuna Mwanzo ulikokuwa rahisi kwenye kila jambo unapotaka kulianzisha ndio maana ukitaka kufikia mafaniko yako binafsi haupaswi kuishi na makosa ya jana leo na haupaswi kuishi na matarajio ya kesho leo bali unapaswa kuitumia vizuri kila dakika na sekunde unayoweza kuipata leo.
Kumbuka jana ni historia lakini Kesho ni Muujiza.Fanya jambo ambalo litakuwezasha kufikia malengo fulani ukitegemea urahisi wa jambo tambua upotevu uko karibu kuliko unavyodhani.
Laini Laini Maana yake si rahisi.Mwanzo ni Mgumu.Mwanzo wa Neno ni Mgumu kuliko Mwisho wake.

"Kila ukionacho leo ni Rahisi  Kuna Siku Kilishawahi Kuwa Kigumu"