Nikiwa nimeamka Siku ya Tarehe 1/1/1994,Mama aliniambia Hata sisi tuliwahi kuwa kama wewe ulivyo.Wakati maneno hayo yanasemwa sikuelewa yana maana gani,Maana sikuwahi kufafanuliwa ila niliona siku zikienda na zikisogea mbele,Mara nikajikuta namaliza Level Moja Ya Elimu huku nikienda Nyingine na Mara Elimu Ya Juu.Naam Muda unaenda na Muda haurudi.Kufanya malengo yoyote bila kuwa na mipaka ya muda bado hauwezi kufikia lengo.Hakuna Lengo Lisilokwenda na Muda.

Jamii yetu ya Kitanzania imelelewa kuishi kwamba kesho ipo tu,Lakini cha kushangaza hatufikirii kama hiyo kesho sio yetu maana hakuna kilicho na uhakika wa kuiona Kesho hiyo.

Baada ya Kusoma Kidogo..Zamani tukiwa tunakuwa Shule za Msingi Tulikuwa tunafundishwa kumeza Nyakati Mbali Mbali za Sentensi kwa Kingereza Yaani Tenses,Kwa Mara ya Kwanza Nilisikia Kitu Kinaitwa Future Tense Mwaka 1996,Niliimeza Baada Ya Miaka Michache Kupita Kuna Siku Nikajiuliza Ivi Kuna Future Tense au ni Future Time na Hiyo Future Time or Future Tense Zinatoka wapi....Ingawa sikuwa na Uelewa Mpana,Baada ya kufwatilia nilikuja kupata Ufumbuzi kwamba Hakuna Future Tme wala Future Tense...Wewe Binafsi Ndio Future Tense na Future Tense....Fikiria kama wewe ukiwa Haupo Je kuna kuwa na future Tense au Future Time??

Dunia ya Kwanza yaani Naamanisha Nchi zilizoendelea Muda kwao ni Muhimu wanafanya Kila liwezekanalo kuweza kuokoa Muda ili kuweza kufikia malengo wanayojiwekea,Kuanzia kwenye usafiri na Utendaji wao wa shughuli za kila siku.Kuna wakati unajiuliza Kama unakaa kwenye Foleni ya Gari Masaa Matatu na Unapokwenda Ukitumia Mguu hayazidi hata Masaa Mawili kwanini usichague kutembea???Kizazi chetu kina Excuse nyingi....Utasikia Jua kali,Je wazazi wetu hawakuliona Jua?Au Sisi Ndio Ngozi Zetu zina ukakasi kuliko wao?Swali la kujiuliza??Maisha yetu hapa duniani yamefungwa kwenye Muda,yaani Unapochezea Muda ndio Unachezea maisha yako Pia.


Unapochezea Muda Unachezea Maisha yako pia,Ni ngumu kumshauri mtu aliyezoea kuishi kwenye maisha yasiyozingatia Muda,Ukimwambia Utasikia "No Hurry In Africa".Mtu huyu akikwama juu ya jambo fulani ukimwambia jambo hili ulipaswa ufanye miaka mitano iliyopita ananza kutoa macho,Sasa unabaki unajiuliza huyu vipi,Tangu tunakuwa kuna watu hawaendi mbele wala hawarudi Nyuma yaani wapo wapo,Ukimwambia na Ukimshauri Utasikia Sisi Tumeliona Jua Kabla yako.Kumbuka Kila unachofanya Hapa duniani kina mwisho wake kama kilikuwa kina mwanzo basi mwisho Upo.

Unapochezea Muda Pia na Hata Resources nazo Zinapotea.Fikiria Mfano wewe ndio Mchezaji Mpira,Mwili wako ndio Resources moja wapo ya kutumia ili kukuwezesha kufikia malengo fulani kwenye maisha yako.Kumbuka kadri unavyokuwa mtu mzima Resources hiyo inazeeka na mwishowe kuchakaa na kutokuweza kutumika tena na kama itatumika sio katika kiwango husika kwenye maisha yako.Fikiria wewe ni mwimbaji Sauti yako ndio resources yako ,Je unafikiri Unavyoweza kuimba leo na Ndani ya Miaka 30 ijayo utaweza kuimba hivyo hivyooo???Anayekupotezea Muda,Anakipotezea Malengo.

Mwisho wa Siku Nashaangaa yaani mtu kazunguka huko katafuta cha kufanya kakosa anakuja kwako anakuambia twende mahali fulani,Ukifika Kule mahali utasikia twende mahali kwingine,Mwisho siku unamaliza siku nzima umechoka una umetumia muda wako kuzurura barabarani bila kufanya kitu cha maana unapoona kuna vitu vunaweza poteza muda wako kataa kuvilea,Badilisha mfumo wa maisha.Kumbuka hakuna wakati ujao,Wakati Ujao ni sasa na Wakati Ujao ni Wewe.Usifikirie ya Kesho wakati ya Leo Haujayamaliza.

Maisha Yetu Yamefungwa katika Muda,Baada ya Muda fulani unapaswa uwe umefanya jambo fulani,Ndio maana kwa sisi mabachela mtu akifika hadi Miaka 40 hajaoa watu wanajiuliza kwanini hajaoa,Tatizo sio Kuoa tatizo ni muda wa kuoa.Zingatia Muda wako kwenye Kila jambo Maana Muda ni Wewe na Wewe ni Muda.

...Punch Of The Week..............Anayepoteza Muda,Anapoteza Malengo