Mwanamuziki wa Injili anayeishi nchini Sweden Katika Mji wa Malmo anayejilikana Kwa Jina Rachel Sharp katika siku ya Jumamosi 26/1/2013 alizundua Albamu yake ya Pili hapa nchini Tanzani ijulikanayo kwa jina "NI MUNGU WA AJABU" yenye jumla ya nyimbo 10 zilizo katika mfumo wa CD na nyimbo 8 zilizo katika DVD.
Rachel Sharp alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari katika Eneo ya Nyumba yake katika Eneo La Tegeta Ambapo ndipo uzinduzi ulipofanyika alitoa Rai kwa Wanamuziki wa Tanzania Kuendelea Kuenzi Muziki wetu wa Asili kama Ilivyo Mdumange na Mdundiko pia aliongezea kwa kusema Lugha ya Kiswahili kwenye Muziki inalipa zaidi kuliko ilivyo Lugha za Kigeni tunazojaribu kutumia.Akitoa mkazo zaidi aliendelea kusema tuache kuiga miziki ya watu na sisi tukae chini tubuni aina yetu ya muziki ambayo inaweza kutumika kama utambulisho wetu kwenye soko la kimataifa la Muziki.


Mc wa Event Ritha Chuwalo akimtambulisha Rachel Sharp

Rachel Sharp akiwatambulisha Wazazi wake Kwa Waandishi
Rachel Sharp Akitoa Wito kwa Waandishi kufikisha Ujumbe alioukusudia

Mume wa Mtangazaji Maarufu Zawadi Machibya akiweka wakfu Albamu ya Rachel Sharp.

Hadi Kieleweke.....Mwanamuzi wa Injili Rachel Sharp akiwa kwenye Stage 

Mwanamuziki wa  Injili Rachel Sharp akienda sawa kwenye 

Nguli wa Muziki Nchini Tanzania Upendo Kilahiro akifanya kazi kwenye Stage
Rachel Sharp na Upendo Kilahiro wakiwa kwenye Jukwaa Moja
                                           
Mwisho wa yote Rachel Sharp alisisitiza Kuwa Mafanikio Yetu hayaji kirahisi kwenye Kila Kitu imetupasa kujituma katika kila jambo bila kujali wengine wanatonaje,akimaliza alisema Upendo na Umoja Miongoni mwa wanamuziki wa Injili kukaa chini na kuja na ubunifu mpya kutawaongezea mafanikio katika tasnia ya Muziki wa Injili ndani na Nje ya Mipaka ya Tanzania.