The Meaning of Marriage: Facing the Complexities of Commitment with the Wisdom of God.

Kitabu cha The Meaning of Marriage kimeandikwa na  Mchungaji Timothy J. Keller ambaye  alizaliwa mwaka 1950.
Timothy J.Keller ni Mchungaji wa Kanisa lijulikanalo  Redeemer Presbyterian Church kwenye Mji wa New York nchini Marekani.
Mwaka 1989 alipewa kanisa hili likiwa na Watu 50 tu lakini kwa Sasa lina washirika zaidi ya 5000 ambao wamejisalijili kwenye kanisa hilo la Mchungaji Timothy J.Keller.

Mchungaji Timothy J.Keller anaamini kwamba mafundisho mengi ya ndoa yanayofundishwa siku hizi yamepotosha maana halisi ya ndoa.
Mchungaji Timothy J.Keller ni mpinzani wa ndoa za jinsi moja pia ni mpinzani wa swala la kutoa mimba.Lakini anaamini Ndoa ni sehemu ya kumfanya mtu akue kiroho kufikia kiwango cha juu zaidi cha Maisha yake.

Mchungaji Timothy J.Keller anaamini Biblia ndio Muongozo sahihi kwenye swala linalohusu ndoa.

Kanisa la Mchungaji Timothy J.Keller linahesabika kuwa kanisa la 16 nchini Marekani lenye ushawishi mkubwa zaidi kwenye jamii.

Hiki ni Moja ya Kitabu cha Kikristo kilichofanya Vizuri kwenye gazeti Maarufu ya Nchini Marekani lijulikanalo Kama New York Times.
Mchungaji Tim J. Keller ameoa mke anaitwa Kathy na Sasa wana jumla ya Watoto watatu(David, Michael and Jonathan).

Kionjo Kutoka kwenye Kitabu hiki cha Mchungaji  Timothy J.Keller.

Marriage has the power to set the course of your life as a whole. If your marriage is strong, even if all the circumstances in your life around you are filled with trouble and weakness, it won't matter. You will be able to move out into the world in strength.”
Siku ya Jamamosi tarehe 23/03/2013,Huduma ya Soul Breakfast Chini ya kitengo cha Campus Ministry cha Kanisa la Victory Christian Center Tabernacle  a.k.a VCCT kutakuwa na sherehe ya Kutimiza miaka miwili toka huduma hii ya wanafunzi ianzishwe.Napenda kuchukua nafasi hii kama mmoja ya Wadau wa Huduma hii ya Wanafunzi kwenye mji wa Dar es Salaam kukukaribisha.
Inter-Collage Praise Worship Team ndio itaongoza Kusifu na Kuabudu.
Comedy itaongozwa na Mc Pilipili na King Chavala.
Msemaji Mkuu atakuwa Pastor Dr Huruma Nkone.
Vyeti Vitatolewa Siku Hiyo ...n.k

Usafiri wa Kwenda na Kurudi Utukuwepo bure kuanzia Saa Mbili na Nusu Asubuhi kwenye Kituo Cha Mwenge kama Uneelekea Maeneo ya Kiwanda Cha Coca Cola. 
Chai ya Nguvu itatolewa Bure.

Karibuni wote