Mwanamuziki wa Injili anayeishi nchini Sweden Katika Mji wa Malmo anayejilikana Kwa Jina Rachel Sharp katika siku ya Jumamosi 26/1/2013 alizundua Albamu yake ya Pili hapa nchini Tanzani ijulikanayo kwa jina "NI MUNGU WA AJABU" yenye jumla ya nyimbo 10 zilizo katika mfumo wa CD na nyimbo 8 zilizo katika DVD.
Rachel Sharp alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari katika Eneo ya Nyumba yake katika Eneo La Tegeta Ambapo ndipo uzinduzi ulipofanyika alitoa Rai kwa Wanamuziki wa Tanzania Kuendelea Kuenzi Muziki wetu wa Asili kama Ilivyo Mdumange na Mdundiko pia aliongezea kwa kusema Lugha ya Kiswahili kwenye Muziki inalipa zaidi kuliko ilivyo Lugha za Kigeni tunazojaribu kutumia.Akitoa mkazo zaidi aliendelea kusema tuache kuiga miziki ya watu na sisi tukae chini tubuni aina yetu ya muziki ambayo inaweza kutumika kama utambulisho wetu kwenye soko la kimataifa la Muziki.


Mc wa Event Ritha Chuwalo akimtambulisha Rachel Sharp

Rachel Sharp akiwatambulisha Wazazi wake Kwa Waandishi
Rachel Sharp Akitoa Wito kwa Waandishi kufikisha Ujumbe alioukusudia

Mume wa Mtangazaji Maarufu Zawadi Machibya akiweka wakfu Albamu ya Rachel Sharp.

Hadi Kieleweke.....Mwanamuzi wa Injili Rachel Sharp akiwa kwenye Stage 

Mwanamuziki wa  Injili Rachel Sharp akienda sawa kwenye 

Nguli wa Muziki Nchini Tanzania Upendo Kilahiro akifanya kazi kwenye Stage
Rachel Sharp na Upendo Kilahiro wakiwa kwenye Jukwaa Moja
                                           
Mwisho wa yote Rachel Sharp alisisitiza Kuwa Mafanikio Yetu hayaji kirahisi kwenye Kila Kitu imetupasa kujituma katika kila jambo bila kujali wengine wanatonaje,akimaliza alisema Upendo na Umoja Miongoni mwa wanamuziki wa Injili kukaa chini na kuja na ubunifu mpya kutawaongezea mafanikio katika tasnia ya Muziki wa Injili ndani na Nje ya Mipaka ya Tanzania.
Miaka Michache iliyopita Tanzania kulikuwa na Blogs Chache sana na tulikuwa tunajiuliza ivi mtu anawezaje kumiliki blog,Lakini baada ya muda fulani kupita watu wengi tulijifunza angalau namna ya kuanzisha na kuendesha blog.Miaka ya 2005 teknolojia ya blog Tanzania ilikuwa ngeni kidogo lakini nashukuru kwamba kadri siku zinavyozidi kwenda blogs zinaongezeka na zimekuwa nyingi zaidi lakini pamoja na haya yote kutokana na ukuaji wa teknolojia hii nchi yetu imekuwa taratibu sana kutunga sheria au kufanya mabadiliko ya sheria mbali mbali yatakayoendana na ukuaji wa teknoloji mbali mbali.Sina mengi ya kujadili kwa upande huo.

Baada ya kufanikiwa kupitia blogs nyingi hapa Tanzania hata mwanzo naanzisha blog hii nilijua copying and Paste ndio namna ya uendeshaji wa blog lakini baadae baada ya kufwatilia kiundani kidogo nikajiuliza je mtu alianzisha teknolojia ya blog alikuwa na maana hii ya copy and paste au kulikuwa na maana nyingine zaidi?

Blog sio copying and Paste blog ni sehemu ya kuonyesha kile ulichonacho kwenye ubongo wako,Baada ya kufwatilia sana nimekuja kugundua tasnia ya uandishi hapa Tanzania ina Critical Thinker wachache na hata waliopo hawaandiki maswala yanayohusu jamii na maisha yetu ya kila siku katika kuikwamua jamii yetu.

Blog sio sehemu ya matangazo baada ya kufwatilia tena nimekuja kugundua yaani sisi huwa vitu vingi tunafanya kinyume nyume yaana baada ya kwenda mbele sisi tunarudi nyuma.Yaani siku hiz utakuta blog ina matangazo mpaka unaboreka,hata hamu ya kuendelea kuangalia blog hauna hamu.Na tatizo kwa walio wengi sio vibaya kuwa na matangazo lakini sababu na maana ya msingi ya kuwepo blog isifutwe au kupotezwa kwa tamaa ya fedha.

Blog ni kama diary ambayo unaweka kumbukumbu zako muhimu za maisha ambazo zinaweza kuwasaidia wengine na kuweza kutoa majibu ya maswali amabayo wengine wanayo juu ya maisha na maswala mbali mbali ya kijamii katika kila nyanja yaani kiuchumi , kijamii na hata kisiasa ili kuweza kuleta hamasa kwenye jamii yetu katika maisha yetu ya kila siku.

Je Blogger ni Mwandishi wa Habari ?Kuna tofauti gani kati ya Blogger na Mwandishi wa Habari?
Mwisho jifikirie kuna tofauti gani kati ya website na blog...Na kama blog ni website ndogo kwani kuna website kubwa....Nini maana ya neno www.ww.com na nini maana ya www.fm.blogspot.com
Then come up with answers,tuifanye tasnia ya blog kuwa kivutio na sio kero kwa watu.Fikiria na ufanye mabadiliko.Hivi ndivyo Niwazavyo Mimi

Heri ya Mwaka  Mpya kwa Bloggers Wote Wa Tanzania 2013