Katika namna ambavyo mfumo wa kuishi umewekwa na uhalisia wa mambo ulivyo katika sayari yetu iitwayo Dunia Kukua ni mchakato na sio Muujiza.Kitu chochote ili kikue kufikia utimilifu lazima kinapitia mchakato fulani kabla ya kufikia ukamilifu wowote.Hakuna kitu ambacho kinaweza kukua ghafla bila kupitia mchako wa aina Yoyote iwe ni Kiroho au Kimwili.Binadamu ili kufikia hatua ya kukua na kufikia na ukamilifu wake lazima kuna hatua na mchakato fulani amepitia.lazima Mtoto azaliwe,Akue afikie Ujana ,Uzee ndio Unakuwa tamati na kifo huchukua mkondo wake.
Katika maisha yetu ya kila siku tumekuwa tukikumbana na changamoto na vitu mbali mbali ambavyo tunashindwa kuelewa kanuni za msingi za kuendesha vitu.Katika kila unachofanya lazima kwanza kinaanza na kuzaliwa,Hatua ya Katikati ndipo utimilifu wa juu wa kitu hufikia.Unapomuona mtu mzima leo(Mzee) lazima alipitia hatua zote tatu Muhimu.


1.Kuzaliwa(Formation)
Kuzaliwa ni moja ya hatua muhimu ya maisha na uhai wa kitu chochote,katika hatua hii unaweza ukawa umependa kitu kizaliwe au kisizaliwe lakini mwisho wa siku wote tunajikuta kwenye uwanja wa Mapambano.Je unaendelea kulaumu kwa nini kitu fulani kilizaliwa?Hapana,yaani hata kama ukilauma ndio tayari kimeshaonekana kwenye Ulimwengu wako.
Mfano Kuna watoto walizaliwa kwa Uzazi wa Mpango na Wengine Ghafla Bini Vuu wakajitokeza kwenye Hii sayari,Aliyezaliwa kwa uzazi wa mpango na wa Ghafla Bini Vuu Mwisho wa siku wote wako kwenye Sayari hii itwayo Dunia.Kulaumu kwako hakukufanyi urudi tumboni kwa Mama bali ndio Umeshafika sasa.
Yaani Samaki aliyevuliwa kwa Baruti na Wengine kwa Njia Sahihi lakini mwisho wa Yote wamevuliwa na wameshatolewa baharini.

Hapa ndivyo ilivyo kwenye maisha yetu ya kawaida unaweza ukapanga kufanya kitu fulani kwenye maisha au Usipange lakini mwisho wa siku ndio umeshajikuta humo.Je Unafanyaje?Kulaumu hakutasaidia kutatua hilo tatizo au hicho kitu ambacho umekutana nacho.

Kitu kinapozaliwa kinaweza kisiwe na mwelekeo sahihi lakini wewe mlezi wa kitu ndio una uwezo wa kufanya kitu kiwe sahihi,ndio Maana Wahenga husema Mtoto uleavyo Ndivyo akuavyo.usitegemee Utamlea mtoto katika hali ya uvivu na Uzembe alafu akikua awe Mchapa Kazi...
Unapotaka kuanza Biashara lazima Izaliwe kwanza,Unapotaka Kuanza kazi lazima iwe na mwanzo wake...Hakuna kitu kina kua tu...Kumbuka Hata Mbuyu ulianza kama Mchicha Ila Sijui...Kiroboto alianza kama nini....mwisho wa Siku Kukua ni Mchakato na Sio Muujiza........


2.Kukua(Growth)
Siku hizi kwenye jamii kumekuwana matatizo mengi sana ambayo watu wengi tumeshindwa kupata majibu kwa sababu hatujui mchakato wa vitu hivyo vimeaanzi wapi,Mfano Wakati unakuwa nyumbani kwenu unakuta Style ya Maisha ni Matusi na Ngumi kuanzia kwa Baba na Mama Mpaka Kaka/Dada zako.Je Unahisi hapa itakuwaje?Je unapomwona Mtu ni Mlevi unahisi alinza ghafla tu..Hapana Kukua kwenye jambo lolote ni Mchakato na sio Muujiza hata Ukisoma kwenye Vitabu vya Dini Dhambi ili iwe dhambi Kuna mchakato imepitia mpaka kufikia Tamati
Kufikia hatua ya kukua kwenye kila jambo inategemea msingi uliojengwa tangu mwanzo wakati jambo linaanza..Unaapomwona mfanyabiashara mkubwa leo amefanikiwa hakuanza kama uyoga bali kuna mchakato alioupiti kugia Hapo.Mara nyingi tunasahau kwamba hakuna kitu ambacho kinaibuka tu kwenye maisha Yetu ya kila Siku..tangu Mwanzo ukijenga tabia ya kusoma vitabu na kutafuta maarifa na kubuni vitu na ukaendelezwa ndivyo utakavyokua.
Usimshangae mtu alivyo Leo Maana Hukuona Jana Yake,Tabia na Maisha ya Mtu ilivyo leo Inatagemea kwenye hatua za mwanzo alianzaje?
Mara nyingi nimekuwa nikipishana na watu sana kwenye kuwahukumu watu kwenye maisha yao kwa sababu sisi tunaona matokeo lakini hatujui huyu mtu alianzaje...Imekupasa kulaaumu msingi wake ulivyojengwa na sio hii hatua ya Katikati ya Kukua.


3.Maturity(Ukomavu)
Hatua iliyopita ni moja kati ya hatua muhimu ambazo zinaweza zikatoa Majibu ya maswali mengi kufikia kuelekea hatua hii ya Ukomavu(Maturity).
Kutokana na mfumo wa Malezi yetu Watanzani kama si waafrika tulio wengi tunakuja kugundua vitu vingi si sahihi kwenye hatua ya Kukua wakati msingi ulishajengwa vibaya.Mfano wa Ghorofa Ikishajengwa vibaya toka chini kwenye Msingi ndivyo itakavyoendelea Mbele kwenye Ujenzi.Iwapo Fundi hakushtuka basi ujenzi huo utaendelea mpaka mwisho wa safari na Mwisho wa Siku tunashuhudia Ghorofa zinaanguka na kuua watu.
Pamoja na maisha yetu ya kila siku kujengwa Hivyo mpaka tikufikia ujana ndio tunagundua kwamba hiki hakikuwa sahihi Je unafanyaje?Je unaendele kuishi kwenye Ubaya?Je Unavunja Msingi huo Uanze tena?
Kuna maswali mengi ya kujiuliza sasa.
Unapokua kipindi cha Ujana unaweza kufanya Mabadiliko Mengi sana ambayo yanaweza kuleta matoke chanya kwenye kipindi cha Ukomavu wa Jambo lolote.Hakikisha unafanya maamuzi yalio Sahihi kwenye Jambo lolote..hakuna Muujiza...hapa...Hata Uwapo unataka kukuza kiwango chako cha Kufikiria vitu anza mwanzo na utsonga mbele taratibu hakuna Muujiza hapa ....
Jambo Lolote linapofikia mwisho ndipo tunaona Matokea kutokana na hatu mbili zilizopita na Hapa ndio watu wengi tunatoaga hukumu ya Maswali Mengi sana na vitu vingi sana maishani mwetu....Katika yote ukumbuke hili....Growing is a Process Not A Miracle..................

                      
             ...................Kukua Ni Mchakato   Na .............Sio ...............Muujiza..........................
Baada ya wiki Moja iliyopita kwenye Miji ya Dodoma Na Mbeya kutikiswa na tukio la Campus Night,Jana usiku(23/11/2012) ilikuwa ni zamu ya mji wa Singida kutikiswa na tukio hili Adhimu nchini Tanzania,Rise and Shine ndio ilikuwa theme mjini Singida,Baada ya blog hii kupata habari kutoka kwenye chombo cha kuaminika kwamba zaidi ya watu 700 waliamua kumpa Yesu maisha yao huku takribani watu yapata zaidi ya 5000 wakihudhuria kwenye tukio hili ambalo linatokea mara moja tu kwa mwaka

Pata Matukio katika Picha 



Hapa tupo Katika ya Safari kuelekea  Singida 
Victor & Chavala

Ndani Ya Singida

Costa Mbili Watu Full...

Watu Wakifanya Furaha za Shangwe kwa Bwana


Samuel Yonah... the best guitarist, composer, arranger of all times


Watu pipoz...


The audience Praising and dancing


Prosper ,Steve Wambura,and Chavala


Mungu wa Mapendo...


Students Joint Mass Choir


Papaa Ze Blogger(T-shirt Nyeupe) Mc wa Shughuli akienda sawa


Pastor Dr Huruma Nkone na Daniel a.k.a Kenge wakimsifu Mungu


The Mass Choir perfoming


Hata Baada ya Kumaliza Honey Moon siku chache zilizopita lakini  Steve Wambura hakuacha kumsifu Bwan


The Empire wakifanya Vitu vyao


700 peoples received Jesus


Steven Wambura a.k.a Le grand Mopao akiendesha jahazi
Kama kawa Swahiba Mc Pilipili Hakubaki Nyuma..Pasua Mbavu Singida


Rivers of Joy International wakienda Sawa kwenye Praise and Worship


Katika Yote Ujumbe Mkuu ulikuwa Hauwezi songa Mbele Bila Yesu...Yesu Ni Jibu La Mambo yote
Mara zote tumekuwa tukifanya vitu tukijua kwamba tupo sahahi lakini mara nyingi tumekuwa hatupo sahaihi kutokana na upeo wetu mdogo wa kufikiri vitu kwenye nyanja mbalimbali na athari mbali mbali zokanazo na vitu mbali mbali.Unapofanya kitu kwa fikra halisi na utimilifu wa mambo ndipo unaweza kugundua kwamba uko sahihi hapana mara nyingi matokeo mazuri ya kile ulichofanya ndio hutupa jibu kwamba input ambayo umeiweka/umeitumia ilikuwa sahihi au hapana.Maamuzi yetu  huadhiriwa na vitu mbali mbali na hutufanya tuwe sahihi au hapana kutokana na vitu hivyo.Kwenda Kanisani Hakukufanyi kuwa Mkristo na Wala Kusimama Karibu na Karakana ya Magari hakukufanyi kuwa Gari.

1.Mazingira

Mazingira tuliyokulia yanamchango mkubwa sana kwenye maisha yetu na huwa na athari kubwa juu ya vile vitu ambavyo tunaishi na na namna tunavyofanya maamuzi yetu.Mfano Siku Moja tulipokuwa Kanisa fulani...Mzungu alisimama akitoa ushuhuda kwamba Yaani Maisha Mabaya sana kwake na Amechoka Kula Kuku kila siku,Wakati aliposimama Mama mmoja akaeeleza namna ambavyo hawana chakula kabisa.Ukifwatilia kinachowatofautisha hawa watu ni mazingira waliyo kulia.Lakini pamoja na yote Mazingira yanaweza kukufanya uwe sahihi au hapana kutokana pia na mtazamo wako binafsi.....Kwenda Kanisani hakukufanyi kuwa Mkristo wala Kusimama karibu na Karakana ya Magari hakukufanyi kuwa Gari

2.Information 

Habari za kila siku ambazo tunazipata zinaathiri sana maisha yetu tunatoishi kila siku na katika nyanja tofauti tofauti embu fikiria kama tungekekuwa toka tumezaliwa kwenda shule isingekuwa ni lazima/kungekuwa na mfumo mwingine wa kusoma,Habari hizo ndizo zingekuwa chanzo cha namna tunavyofanya vitu vyetu na namna tunavyoralate na wengine na namna tunavyofanya maamuzi ya maisha yeyote kwenye maisha yetu.Fikiri kama tungeambiwa kula makande ni sumu toka tunazaliwa mpaka tulipo maamuzi yetu yangejengeka kwa namna hiyo bila kuzingatia maswala Mengine.Hembu fikiria kwamba tungekuwa tunambiwa Ukimwi hausababishi kifo na hauna madhara kwenye maisha yetu ya kila siku je ingekuwaje?

3.Watu

Marafiki,Ndugu na jamaa wanamchango mkubwa na maisha yetu katika kila tunachokifanya,Ndio maana wahenga walisema ukitembea na mwizi na wewe utakuwa mwizi basi si kama mwizi kwa asilimia zote bali lazima hata uamulie kuwa kibaka,Chuma hunoa chuma siku zote.Marafiki wanaokuzunguka wanamchango mkubwa sana kwenye maisha yako,Wataalamu wanasema ukitaka kujua pato la la mwezi kwene ajira yakeChukua marafiki wake watano wanaomzunguka kwa ukaribu sana,Tafuta wastani wao unaweza kujua pato lake la mwezi.Lakin pamoja na hayo yote ni vizuri kuaangalia marafiki ,ndugu na jamaa wanaotuzungumza wanamchango gani kwenye fikra zet na namna tunavyoishi kila siku.Haiwezekani ukatembea na Chizi wewe ukaonekana mwenye akili.

Pamoja na mambo yote unaweza ukawa umeathiriwa kwa namna mbaya kutokana na sababu hizo tatu za ambazo ndizo zimekuwa sehemu kubwa ya maisha yetu lakini kumbuka bado unaweza kufanya vizuri zaidi
Hata kama umefanya vibaya sana bado unaweza ukabadilika na kufanya vizuri zaidi...Kumbuka ...Kwenda Kanisani Hakukufanyi kuwa Mkristo wala Kusimama Karakana ya Magari Hakukufanyi Kuwa Gari..

...Kwenda Kanisani Hakukufanyi kuwa Mkristo wala Kusimama Karakana ya Magari Hakukufanyi Kuwa Gari..
Rising The Standard ndio ilikuwa kauli mbiu katika Campus Night iliyofanyika katika Mji wa Mbeya siku ya Ijumaa ya tarehe 16/11/2012 bila kusahau mji wa Dodoma nao uliendelea kutikiswa na Event hii ya Campus  Night yenye kauli mbiu My Life,My Love , My All.Naam matukio haya pacha yaliwakutanisha wanafunzi wa elimu ya vyuo mbalimbali katika maeneo husika

Kama ilivyo ada Mc maarufu wa Mji Papaa Sebene ndio alikuwa mshereheshaji wa Event iliyofanyika Mbeya naam...


Katika Segment ya Comedy Mc Pilipili alitikisa mji wa Mbeya,Kama ilivyo ada ya King Chavalla hakukosekana akiwaacha wanafunzi hoi kwa comedy

Wasemaji wa Siku hiyo katika Mji wa Mbeya walikuwa ni Pastor Dr Huruma Nkone,Rose Mushi,Dr Kimambo,Mr Msigwa na Dr Maboko,Wote hawa walizungumzia namna ya ku-rise Spiritual Standard pia na maisha ya kawaida tu ya mwamini katika eneo la uanafunzi



Pastor Dr Huruma Nkone alisema ushalobaro wala utoz toz na u-sista du haumsaidia mtu kuwa na clear future only Jesus can Transform your life na ata-rise standard zako..Kwa mara nyingine tulishudia Radical Gospel ya Dr Huruma Nkone isiyokuwa na kificho.

Nabii Mke a.k.a Rose Mushi alishusha sindano za kurise starndard zako kwenye swala la mahusiano.Alisisitiza kuwa bila Yesu mahusiano yako ni bureee...Alikazia akasema ni Bora uachuke kwa kumtii Mungu kuliko kuumtii mwanadamu.Kama ilivyo ada akiwa hana mic unaweza kumwangalia na kumfikiria unavyopenda..Kosa linafanyika tu pale akiwa na Mic....Ukumbi mzima ulikuwa moved na Nguvu ya Mungu through Rose Mushi.

Dr Kimambo aliongelea swala la Academic and Execellence pindi uwapo shule pia..Akatoa kanuni na mfumo wa namnq ya kurise standard zako na namna ya ku-execel academically..It was more than Powerfully...Kama ulimisi hii na wewe ni mwanafunzi wa mji wa Mbeya pole.Katika yote aliyoongea alisema huwezi fanya chochote bila Yesu.

Dr Maboko aliendelea kuongelea swala Ujasiriamali kwa wanafunzi,alijaribu kushare expirience yake katika swala zima la ujasiriamali bila kusitasita alieleza namna ya kurise standard zako katika swala zima la fedha huku ukiwa bado ni mwanafunzi.Lakini mwisho wa Yote alisema ukitaka kurise standard zako ,Yesu ni jibu la lako.

Mr Msigwa .a.k.a Branch Manager wa CRDB Mbozi mjini,aliendele kusema zaidi kuhusu Mahusiano na Changamoto ambazo kama vijana tunazipitia alieeza namna bora ya kupata mke au mume ambaye anaweza akakufaa na ukaendela kuonekana kuwa bado wewe ni bora na unafanya vizuri kati maswala mengine ya maisha pia
Rose Mushi a.k.a Nabii Mke akiendelea kufwatilia nini kinachoendelea kwenye Campus Night

Pastor Dr Huruma Nkone akeendela kukata Gospel ya ulweli

Music Director Pastor Mathew Sasali pamoja na Mama Pastor Rebecca Sasali wakiongoza jukwaa la Praise and Worship 

Sauti ya Dubu ukipenda Mr Dr Nyanda akiwa kazini kama Mc wa siku hiyo

Praise and Worship chini ya Mama Pastor ikifanya kaziii.....

Watu Pipoz

Sebene ya Yesu ikiwafanya watu wadance

Twende Sawa

Watu Pipoz

Moja ya Matunda ya Campus Night zilizopita akitoa ushuhuda

Mc Shupavu a.k.a Papaa Ze Blogger akiendelea na Kaziii

Twende Sawaaa

Makofi kwa ajili ya Yesuu!!!

Twende Sawa

Pastor  Dr Huruma Nkone akiendelea kukata Gospel kama Katapila

Wanafunzi wakimpa Yesu Maisha yao

Wanafunzi wakimpa Yesu Maisha yao

Dr Kimambo akikata shule 

Watu Pipoz

Nabii Mkee akitabiria Watu

Haikuwa Ya kitoto hata Vice President wa Mzumbe Campus ya Mbeya alikuwepo(Mwenye Top ya Kijani)

Mc Pilipili akiwa Kazini

Dr Maboko akiendelea kuongelea Ujasiriamali

Mr Msigwa akiendela kukata shule ya Mahusiano

King Chavalla akipasu mbavu za watu
Hembu angalia huu umati hapa karibia na Saa kumi na moja asubuhi..lakini watu wapo tuu

Hitimisho katika Jumbe zote zilizoongelewa katika Campus Night hizi ni kwanmba Yesu ndio jibu la kila kitu kwenye kila idara ya maisha na kila kona .Yeye ndio mwanzo tena ni mwisho wa kila jambo.