Huyu ndiye DNG

Baada ya Siku Chache zilizopita Kusadikika kwamba Mwanamuziki wa Secular Music Jaguar kutoka nchini Kenya ndiye aliyelipwa fedha nyingi zaidi na Kupitia chama Cha Mgombe U-Raisi Raila Odinga Katika Kipindi cha Kampeni lakini  Siku Ya Chache zilizopita Imekuja kugundulika kwamba Mwanamuziki wa Injili nchini Kenya DNG ndiye aliyelipwa fedha nyingi zaidi kwenye  Kipindi cha Kampeni na Mgombea wa kiti cha U-Raisi nchini Kenya Uhuru Kenyatta.
Inasadikika Mwanamuziki huyu amelipwa Mara 8 zaidi ya Mwanamuziki Jaguar kuendesha Burudani kwenye Kampeni Nchini Kenya kupitia Chama Cha Uhuru Kenyatta.
Wahenga walisema Tabia ya Mtu ni Mtu Mwenyewe.Hakuna mtu anayeweza kuishi nje ya tabia yake ambayo imo ndani mwake.Jinsi unavyomwona mtu mara zote na vitu anavyovifanya ndivyo alivyo.Tabia ya mtu ni udhihirisho wa vitu vingi sana vilivyo ndani mwake.Unapoona mtu anafanya kitu fulani si kitu ambacho kinaibuka mara moja na kutokeza tu bali ni hali ya ndani iliyojengwa muda mrefu kutokana na mambo kadha wa kadha anayokutana nayo kwenye maisha.

Mwanazuoni Mmoja alisema kwa asili Binadamu ni Wabaya lakini wanajaribu kujibadilisha kutoka kwenye ubaya kuelekea kwenye Uzuri wao.Akaendelea kusema kubadilisha tabia si kazi rahisi kama ilivyo kubadilisha nguo ya mwili.Inakuchukua muda mrefu na kufanya vitu mbali mbali kutoka kwenye ubaya wa tabia kwenda kwenye tabia nzuri.


Mwanazuoni mwingine aliibuka na kusema mtu hawezi kuishi nje ya tabia yake ya asili aliyoijenga maishani mwake na akaendelea kusema zaidi kwenye maisha ya binadamu hakuna siri.Tabia za mtu unazoziona kwenye maisha yake ni udhihirisho wa siri nyingi zilizo ndani mwake,Ingawa kwa sisi binadamu hatupendagi kufwatilia tabia ya mtu hatua moja kwenda nyingine.Lakini Unapofanikiwa kufwatilia tabia na namna wanavyoishi ndipo kuna uwezekano wa kugundu mambo kadha wa kadha ndani ya mtu huyo.

Kujenga tabia mpya na njema kwenye maisha ya mtu ni maamuzi na sio aina fulani ya nguvu ambayo inahitajika kutoka nje.Mungu alipomuumba mwanadamu alimuumba kwa ukamilifu wote ikiwa na uwezo wa kukibadilisha kila anachokutana nacho kwenye maisha.Mfano Dunia iliiumbwa katika Utupu bali kulikuwa na Malighafi tu ambazo zilikuwa hazitumiwa kwa namna yeyote.Baada ya Binadamu Kuumbwa ndipo mabadiliko yalipoanza kutokea kutokana na utumizi wa rasilimali hizo.Kila badiliko unalolitaka kwenye maisha yako lipo ndani yako.Hakuna mtu mzee zaidi ambaye ataamua kubadilisha tabia yake akashindwa.


Maisha ya Binadamu ni mfano wa Chupa ya Maji iliyojaa maji machafu Lakini Chupa hii inapokwenda kuikingwa maji kwenye Bomba la Maji ndipo Maji safi yapozidi kuingia na Maji machafu yanapozidi kutoka,Unapofanya kitu hiki kwa muda mrefu utakuja jua maji machafu yameshatoka na masafi ndiyo yaliobakia.Unapotaka kubadilisha tabia mbaya kwenda nje jaribu kutafuta tabia mpya nzuri ianze kuishi bila kuangalia tabia mbaya ulio nayo,Unapoendelea kuishi inafika siku unakuta una tabia mpya ambayo ni njema lakini mbaya imeshaondoka.

Information mbali mbali tunazoingiza kwenye maisha yetu kwa njia ya kusoma,mazingira,watu zinaathari kubwa kwenye maisha yetu na tabia kwa ujumla.Mfano mtu anapokuwa muagaliaji wa picha za Ngono kwenye Luninga,Je unafikiri anajenga tabia ya namna gani?Tabia haiingi mara moja tu kwenye maisha ya mtu bali ni mchakato wa muda mrefu ambao unajuisha mambo kadha wa kadha.Hakikisha inaformation unazoingiza kichwani mwako na maishani mwako moja kwa moja zina reflect kuelekea kwenye aina ya tabia ambayo unaipenda.No Body can Act against Information alizonazo kichwani iwe ni nzuri au mbaya.Hakikisha unafanya mabadiliko kuleta tabia mpya na njema kwenye maisha yako ya kila siku.Hakuna fisadi ambaye alianza kuwa fisadi bali alianza kidogo kidogo toka akiwa mtoto na alianza kwa udokozi wa vitu vidogo vidogo.

Mwisho wa Safari yetu siku ya leo kwenye Punch Of The Week Naendea kusema Impossible is The Word Found In Fools Dictionary. Anza hapo ulipo na kitu ulicho nacho kuelekea kwenye tabia njema.Wataalamu wanasema tabia njema si kwa ajili tu ya kukufanya kuishi kwenye jamii kwa amani na furaha bali tabia nje husaidia hata kujenga maisha yako ya kiafya na kiakili,Kuna uwezekano wa tabia zako mbaya zinapeleka kukuharibu kiakili na Kiafya pia.Hakuna mtu aliyezaliwa akiwa anajua kila kitu na kuwa na tabia njema katika kila Idara lakini wote tumezaliwa tukiwa na lengo la kujifunza.Tabia yako kwenye maisha ya kila Siku ni Zaidi ya Upepo wa Kisuli Suli ,Uangamivu wa Maisha yako Inategemea kiasi gani umejenga tabia mbaya.Na kufanikiwa zaidi kwenye maisha inategemea kiasi gani umejenga tabia njema