Nikiwa nimeamka Siku ya Tarehe 1/1/1994,Mama aliniambia Hata sisi tuliwahi kuwa kama wewe ulivyo.Wakati maneno hayo yanasemwa sikuelewa yana maana gani,Maana sikuwahi kufafanuliwa ila niliona siku zikienda na zikisogea mbele,Mara nikajikuta namaliza Level Moja Ya Elimu huku nikienda Nyingine na Mara Elimu Ya Juu.Naam Muda unaenda na Muda haurudi.Kufanya malengo yoyote bila kuwa na mipaka ya muda bado hauwezi kufikia lengo.Hakuna Lengo Lisilokwenda na Muda.

Jamii yetu ya Kitanzania imelelewa kuishi kwamba kesho ipo tu,Lakini cha kushangaza hatufikirii kama hiyo kesho sio yetu maana hakuna kilicho na uhakika wa kuiona Kesho hiyo.

Baada ya Kusoma Kidogo..Zamani tukiwa tunakuwa Shule za Msingi Tulikuwa tunafundishwa kumeza Nyakati Mbali Mbali za Sentensi kwa Kingereza Yaani Tenses,Kwa Mara ya Kwanza Nilisikia Kitu Kinaitwa Future Tense Mwaka 1996,Niliimeza Baada Ya Miaka Michache Kupita Kuna Siku Nikajiuliza Ivi Kuna Future Tense au ni Future Time na Hiyo Future Time or Future Tense Zinatoka wapi....Ingawa sikuwa na Uelewa Mpana,Baada ya kufwatilia nilikuja kupata Ufumbuzi kwamba Hakuna Future Tme wala Future Tense...Wewe Binafsi Ndio Future Tense na Future Tense....Fikiria kama wewe ukiwa Haupo Je kuna kuwa na future Tense au Future Time??

Dunia ya Kwanza yaani Naamanisha Nchi zilizoendelea Muda kwao ni Muhimu wanafanya Kila liwezekanalo kuweza kuokoa Muda ili kuweza kufikia malengo wanayojiwekea,Kuanzia kwenye usafiri na Utendaji wao wa shughuli za kila siku.Kuna wakati unajiuliza Kama unakaa kwenye Foleni ya Gari Masaa Matatu na Unapokwenda Ukitumia Mguu hayazidi hata Masaa Mawili kwanini usichague kutembea???Kizazi chetu kina Excuse nyingi....Utasikia Jua kali,Je wazazi wetu hawakuliona Jua?Au Sisi Ndio Ngozi Zetu zina ukakasi kuliko wao?Swali la kujiuliza??Maisha yetu hapa duniani yamefungwa kwenye Muda,yaani Unapochezea Muda ndio Unachezea maisha yako Pia.


Unapochezea Muda Unachezea Maisha yako pia,Ni ngumu kumshauri mtu aliyezoea kuishi kwenye maisha yasiyozingatia Muda,Ukimwambia Utasikia "No Hurry In Africa".Mtu huyu akikwama juu ya jambo fulani ukimwambia jambo hili ulipaswa ufanye miaka mitano iliyopita ananza kutoa macho,Sasa unabaki unajiuliza huyu vipi,Tangu tunakuwa kuna watu hawaendi mbele wala hawarudi Nyuma yaani wapo wapo,Ukimwambia na Ukimshauri Utasikia Sisi Tumeliona Jua Kabla yako.Kumbuka Kila unachofanya Hapa duniani kina mwisho wake kama kilikuwa kina mwanzo basi mwisho Upo.

Unapochezea Muda Pia na Hata Resources nazo Zinapotea.Fikiria Mfano wewe ndio Mchezaji Mpira,Mwili wako ndio Resources moja wapo ya kutumia ili kukuwezesha kufikia malengo fulani kwenye maisha yako.Kumbuka kadri unavyokuwa mtu mzima Resources hiyo inazeeka na mwishowe kuchakaa na kutokuweza kutumika tena na kama itatumika sio katika kiwango husika kwenye maisha yako.Fikiria wewe ni mwimbaji Sauti yako ndio resources yako ,Je unafikiri Unavyoweza kuimba leo na Ndani ya Miaka 30 ijayo utaweza kuimba hivyo hivyooo???Anayekupotezea Muda,Anakipotezea Malengo.

Mwisho wa Siku Nashaangaa yaani mtu kazunguka huko katafuta cha kufanya kakosa anakuja kwako anakuambia twende mahali fulani,Ukifika Kule mahali utasikia twende mahali kwingine,Mwisho siku unamaliza siku nzima umechoka una umetumia muda wako kuzurura barabarani bila kufanya kitu cha maana unapoona kuna vitu vunaweza poteza muda wako kataa kuvilea,Badilisha mfumo wa maisha.Kumbuka hakuna wakati ujao,Wakati Ujao ni sasa na Wakati Ujao ni Wewe.Usifikirie ya Kesho wakati ya Leo Haujayamaliza.

Maisha Yetu Yamefungwa katika Muda,Baada ya Muda fulani unapaswa uwe umefanya jambo fulani,Ndio maana kwa sisi mabachela mtu akifika hadi Miaka 40 hajaoa watu wanajiuliza kwanini hajaoa,Tatizo sio Kuoa tatizo ni muda wa kuoa.Zingatia Muda wako kwenye Kila jambo Maana Muda ni Wewe na Wewe ni Muda.

...Punch Of The Week..............Anayepoteza Muda,Anapoteza Malengo

Mara nyingine katika Punch Of The Week Tunaendelea kuangalia Mada Mtambuko na Zinazotuzunguka kwenye maisha yetu ya Kila Siku....Naam...Leo Tunaangalia Mada inayosema Watu Hawasemi Lakini Wanaambiana.

Mara Nyingi kwenye maisha yetu ya kila siku tumeona watu wanakuwa wanatunyamazia kwa nama moja au nyingine kuhusu swala/jambo fulani linalokuhusu wewe binafsi ili hali wewe ukifikiri wako kimiya,ukweli ni kwamba watu hawasemi tu lakini wanaambiana kuhusu wewe na kila jambo unalolifanya kwenye maisha yako ya kila siku.Mara nyingi kuna mambo mengi yanaweza kuwa yanajadiliwa kuhusu wewe lakini hauwezi jua maana hakuna anayekumbia.Tambua kila unachofanya kwenye maisha yako ya kila siku watu wanaambiana hata kama kiwe kizuri au kibaya unachofanya,kiwe cha kupendeza au cha kuchukiza lakini wataambiana tu.

Mara chache sana watu wanakaa kuzungumza habari za mafanikio ya mtu namna mtu anavyopiga hatua kwenye maisha yake kwenye nyanja mbali mbali na kuweza kufanikiwa kuanzia kwenye Imani,Kiuchumi,Kisiasa na hata kijamii pia.Watu wengi wanapokaa pamoja mara nyingi huongea mambo ambayo sa nyingine yanaweza yasikufurahishe ukiyasikia lakini ndivyo watu walivyo.Ni ngumu kuyasikia maana hawakwambia.Tambua kila jambo unalolifanya kwenye maisha yako ya kila siku unaweza ona watu wamekufungia mdomo na kama hawako na wewe lakini jua ni moto wa kuotea mbali.Hakikisha kila hatua na jambo unalolifanya hakikisha unalifanya kwa usahihi na umakini mkubwa hata iwapo watu hawakuoni.Wanaweza kujifanya hawakoni lakini kiukweli wanakutazama tu wanagojea wakutane na watu wengine ambao wako kama wao na waanze kuzungumza bila ya wewe kujua.

Mara nyingi Habari Mbaya za Mtu husambaa mapema zaidi kuliko nzuri.Mwana saikolojia mmoja alisema Binadamu kwa Asili ni Wachoyo na Walafi yaani hawapendi kuona mwingine anafanikiwa kwenye jambo fulani kwenye maisha yake.Yuko tayari kuharibu kwa kusema mabaya yako hata kama hayana ukweli ili mradi akuharibie maisha yako.Ki-Ukweli wewe unawez ukawa unatembea njia na kuona hamna shida na unacheka na wengine lakini Watu hawasemi Tu ila wanazungumza kwa muda wao wanaoujua zaidi.Je umeshawahi kujiuliza,je kama ungepewa nafasi ya kusikiza maongeze ya watu kwenye simu pale TCRA ya 
kil siku unahisi ukijisikiaje??Watu hawasemi Lakini Wanaambiana.Makosa ya mtu huonekana zaidi kuliko uzuri wa mtu,Waswahili wanasema Baya moja Hufuta Wema 1000 ulioutenda.Ni rahisi kusemwa ubaya wako kuliko uzuri wako Maana kwa asili binadamu ni Wabaya kama Alivyosema mwanasaikolojia.

Mwisho Napenda Kusema imekupasa kuwa makini namna unavyojiwakilisha mbele ya watu,awe mtu wako wakaribu unayemwamini au usiyemwamini ni muhimu kuchukua tahadhari mapema.Fanya maswala yako kwa uminifu ili hali kama ungetamani wengine wakufanyie hata iwapo watu hawakuoni.Make Sure haufanyi vitu kwa ujinga,fanya kwa umakini huenda wanajifanya hawakuoni lakini wanakuona.Fanya kwa kiwango cha Juu lakini pale ambapo unaona umefika mwisho acha,Jitahidi kuweka juhudi kwenye kila jambo unalolifanya na kwa umakini mkubwa sana.Watu hawasemi lakini Wanaambiaana...


..................Watu Hawasemi Lakini Wanaambiana.............................
Miaka michache iliyopita nilikutana na msemo huu( "If you want to hide something from a Black Man Put it in a Book"). ambao ulinitia hasira kidogo na kunifanya nijiulize mara mbili mbili kwanini.Msemo huu miaka ya nyuma ulitumika nchi Marekani ambao ulikuwa una lengo la kuwabagua watu weusi kupata haki ya msingi ya kujifunza maana walikatazwa kusoma na kujifunza vitu kadha wa kadha.Lakini Baadaye baada ya kufwatilia kidogo nilikuja kugundua tatizo lilikuwa halipo kwa waliotunga aina hii ya taratibu bali lilikuwa kwa waliowekewa utaratibu huu.Watu weusi walikuwa ni watu wasiopenda kujifunza na kusoma baada yake waliamua kutumia muda mwingi kufanya vitu visivyo na tija kwa muda mrefu ambavyo vilitumia nguvu zaidi kuliko akili zaidi.

Mfano Michezo kama Basket na Rugby na michezo kadha wa kadha.Waafrika hawa walibuni michezo mingi kadha wakadha ili kujiletea burudani na maisha yao kuendelea lakini walishindwa kushika nyazifa muhimu na kupata maendeleo yaliyobora.Watu weusi wachache waliopata kupenda kusoma walipewa nafasi kubwa na hata uwezo wao wa kusoma na kuendesha vitu ulikuwa tofauti na wengine.

Tukirejea hapa Afrika kwetu na Haswa Nchi yetu ya Tanzania kwa miaka mingi Kutafuta maarifa na elimu ambayo yatakufanya uendelea kudumu zaidi kwenye changamoto za maisha imekuwa ngumu.Tumekuwa tukilalamika kuhusu swala la maendeleo lakini Upande wa pili je tuna uwezo wa ziada ambao unaweza kutufanya tuendelee kwa haraka.Baada ya kufwatilia kwa kiasi kikubwa nimekuja kugundua wasomaji wa vitu ni wachache na wafwatiliaji wa vitu niwachache.Ukitaka kujua uwezo wa mtu na anavyojua vitu angalia hata namna ambavyoa anaendesha maisha yake na anavyofikiria na kuchambua vitu.Katika pita pita zangu za kusoma vitu nilikuna na huu msemo usemaao.."
“Insanity is doing the same thing, over and over again, but expecting different results" by Albert Einstein.


1.Maarifa ni jambo linalodumu ndani ya Mtu Binafsi.

Unapoweza kujiongezea maarifa kwa kusoma na kujiendeleza katika aina tofauti tofauti ya ujuzi kichwani mwako wewe ndio utafaidika kwa sehemu kubwa kwa maisha yako daima.Mtu anaweza akakupokonya cheti au kikapotea lakini Maarifa ya mtu hayawezi kupokonywa wala kupotea maana ni jambo lililoko ndani ya mtu daima na swala ambalo linadumu mpaka siku za mwisho za uhai wake hapa ulimwenguni.Ubongo wa Binadamu ni mithili ya Viungo vingine tu vya mwili kadri vinavylozidi kutumimiwa ndivyo vinavyozidi kudumu daima na kuwa imara.Ubongo ni mfano wa Mguu wa Mcheza Mpira,Maana Mcheza Mpira asipofanya mazoezi kwa muda mrefu au kucheza uwanjani kipaji huanza kupotea taratibu na mwishowe hufa kadhalika ubongo wa mwanadamu ndivyo ulivyo unavyotumika zaidi ndivyo unavyofanya kazi katika hali ya ubora na utadumu kwa muda mrefu zaidi.

2.Kila maarifa yaliyopo kichwani yanathamani yake.

Kila siku tumekuwa tukienda kuomba kazi na kufanya usahili kwenye maofisi ya watu mbali mbali ili mradi tupate ajira.Unapokweenda kwenye usahili mara nyingi hauingi na hata karatasi lengo kubwa linakuwa ni kujua una uwezo na una maarifa kiasi gani kuhusu ulichokisoma na unaweza kuleta tija kwenye kampuni husika?Baada ya kufanya usahili wanaweza kukuajiri na kukupangia kiasi fulani cha malipo ambacho ndicho kinakuwa sawasawa na thamani ya Maarifa yako.Ndio maana kuna viwango vya Mishahara kazini.Ofisi Nyingi mtu anapoenda kusoma akirudi Mshahara huongezeka,Ni kwa sababu ameongez kiwango cha maarifa kichwani mwake.Unapongeza Maarifa mbali mbali kichwani mwako ne ya maisha ya kawaida ya watu wengine ndivyo Thamani yako Hupanda kwa maana nyingine...Mshahara unaolipwa na Maarifa yako vinatosha na vinaenda Kabisa.


3.Maarifa ni Jambo linalorithishwa kutoka kizazi hadi Kizazi kama ulivyo Ujinga.

Familia nyingi zilizo bora kwenye maisha yetu ya kila siku ni familia ambazo ziliwekeza kwenye maarifa siku za nyuma kwenye maisha yao ya kila siku.Mara nyingi tumepika kelele kuhusu swala ma maendeleo na vitu mbali mbali lakini tunashindwa kujiuliza je watu walitumia muda gani kuwekeza katika maarifa.Kun msemo wa wahenga wansema alivyo Baba na Mama ndivyo Watoto walivyo.Tumendelea kupiga kelele kwamba Tanzania kuna anguko la Elimu(Maarifa) maana yake tumejua kuna athari zake katika vizazi vijavyo.Unapokuwa na maarifa zaidi ni rahisi kuwasaidia hata watoto wako kwenye njia iliyobora.Usiwalaumu watoto wa kizazi hiki Bila kujua uwezo wa wazazi wao katika kuwekeza katika swala zima la maarifa.Je wanatumia muda gani na wanawekeza kiasi gani.Na rudi pale pale .Maarifa ni jambo la Urithi kwa Watoto kama ulivyo Ujinga.Kama hautaki watoto wako wawe wajinga siku zote wekeza kwenye maarifa nao watafaidi katika maisha yao yajayo hata usipokuwepo.



.....Maarifa Huuwisha Nafsi Daima Bali Ujinga Hushakaza Mwili......Unapokuwa na maarifa zaidi ndivyo unavyostawi zaidi kuanzia kwenye nafsi na daima lakini Unapokosa maarifa unakuwa Mtumwa wa wengine ambao wanakuwa na maarifa ziadi yako.