Jengo la Ghorofa 15 katikati ya jiji la Dar es Salaam mtaa wa Indra Gadhi limeanguka leo asubuhi  pamoja na Watu wapatao 60 ndani yake mkiwemo watoto wa Madrassa katika jengo hilo. 
Mpaka sasa maiti zilizoopolewa ni 14 na majeruhi zaidi ya 30 wamekimbizwa hospitali.

Pata Habari kwa Picha

Wakati Jengo linaanguka

Muonekano wake Baada ya Jengo Kuanguka

Hili Ndilo Eneo la Tukio

Kazi Uokozi Ikieendelea kwenye Eneo la Tukio
Siku ya Tarehe 23/2/2013 kwenye Ukumbi wa Kanisa la Victory Christian Center Tabernacle (VCCT) kulikuwa na sherehe ya Huduma ya Soul Breakfast Kutimiza Miaka Miwili Tangu ilipoanzishwa Machi,2011.
Huduma Hii ni Maalumu kwa Wanafunzi wa Viwango tofauti tofauti vya Elimu Kuanzia Sekondari Mpaka Elimu za juu hapa nchini Kwetu Tanzania.
Huduma Hii ilianza na wanafunzi wachache sanaa mwaka 2011 lakini mpaka sasa kuna takribani wanafunzi 200 ambao wana hudhuria kwenye huduma hii.Lengo La Huduma Hii ni Kuwawezesha Wanafunzi kupata ujuzi wa kawaida wa maisha ya mtaani baada ya kutoka shule lakini pia na namna ya kutumia fursa zote zinazopatikana wakati wakiwa kwenye maeneo yao ya Elimu wanaposomea.


Ibada ya Sherehe ikianza

Inter -  Collage  Praise and Worship Team ikiwa Jukwaani

Soul Breakfast Team Maurice Okao(Mwenyekiti wa Soul Breakfast) na Director wa Campus Ministry  Samuel Sasali

Praise and Worship Team ikienda Sawa

Pastor Dr Huruma Nkone alikuwepo siku hiyo

Write The Word Coconut kwa Kutumia Mwili Wako

Director wa Campus Ministry Samuel Sasali Akielezea Maana ya Soul Breakfast  

Rivers of Joy International(Junior) Wakienda Sawa

Praise and Worship Imenoga

Cheza muziki wa Yesu

Twende Sawa

Wadau wakienda Sawa na Muziki wa Yesu
Prezzor Chavala akifanya Vitu vyake kwenye Jukwaa

Pastor Dr Huruma Nkone akinena na Watu waliofika Siku Hiyo

Paul Clement kutoka Glorious Team akifanya vitu vyake kwenye Jukwaa

Hawa ndio Presenters na Watu walifanya kazi na Soul Breakfast mwaka 2012-2013 wakiwa wameshika Vyeti Vyao baada ya Kutunukiwa kwa Utayari wao 
Soul BreakFast Committee  wakiwa na Presenter na Wadau Wengine wakipata pich a ya Pamoja na Pastor Dr Huruma Nkone

Maurice Okao Mwenyekiti wa Soul Breakfast Committee akieleza jambo

Mc wa Soul Breakfast Siku hiyo akienda Sawa

Wadau wakisikiliza jambo kwa Umakini Mkubwa Sana

Mwendo wa Celebration tu hapa

MC akienda Sawa

Vuvuzela Zilikuwa Sehemu ya Sherehe ya Soul Breakfast



Huyu ndie Mc Pilipili Mtoto wa Mama Roda

Kikazi Zaidi Mc Pilipili ya Shughuli


Mwendo wa Kazi tu Hapa

Enzi za Primary hizo 

Paul Clement pamoja na Team yake Wakimaliza Shughuli

Siku zote Rasilimali hazitoshi kwenye maisha lakini hatuachi kuzitumia kutokana na uchache wa rasilimali hizo.Kuweza kufikia kiwango cha juu cha mafanikio ni lazima utumie kwa uangalifu kiasi hiko kidogo cha rasilimali ambazo unazo kwa wakati huo.Hakuna mtu ambaye amefanikiwa kwenye jambo lolote alikuwa na Rasilimali zote  alizozihitaji.Anza Hapo Ulipo,Anza na Hicho ulicho nacho na Utaweza kufikia Kiwango cha juu cha Mafanikio kwenye maisha yako na Ndoto zako kutakuwa ni dhahiri.


Kila kukicha ni ukurasa mpya wa maisha ya mwanadamu lililokuwepo jana silo litakalokuwepo leo,Hakuna mjuzi wa safari hii bali wote tu wanafunzi.Dunia ina kanuni na mfumo wake wa kujiendesha ingawa sisi si wakazi wa muda tu wa ulimwengu huu.Watu wapya huja na wengine huondoka kwa namna mfumo wa dunia ulivyo.Kila kukicha kila mtu anakuwa na mishughuliko ya namna yake.

Mara nyingi tumefikiri kwamba tunapopata ujuzi wa namna fulani kwenye maisha yetu ndio mwisho wa aina fulani ya changamoto lakini unakuja kukuta unapopata ujuzi huo tu unakuta changamoto kama hazikuoni na ujuzi uliokuwa nao na ambao umeupata katika taaluma husika.Ujuzi mpya uliopata hauwezi kuzuia changamoto nyingine zisije bali ndio mwanzo wa aina mpya ya changamoto.Mwamvuli unaweza kuzuia Usilowe lakini Hauwezi kuzuia Mvua isinyeshe.

Baada ya Kupata Ujuzi wa Aina fulani tunahisi ndipo mwanzo wa pumziko wa yale tuliokuwa tunayahitaji kwa muda mrefu.Kumbe tunasahau kwamba ujuzi tulio nao ni  Zana ya  kukusaidia na hauwezi kukusaidia bila kuwa mtendaji wa kazi katika taalamu na uhitaji ulio nao.Taaluma ulio nayo haifanyi matatizo/changamoto zikukimbie bali ndio mwanzo wa mapambano wa changamoto mpya.Ki-ukweli hakuna changamoto zinazobadilika bali sisi mitazamo yetu kuelekea changamoto hizo ndio hubadilika baada ya kupata aina fulani ya ujuzi.

Matatizo na Changamoto nyingi za misongo ya mawazo tilio nayo leo ni kwa sababu tulikuwa tunafikiri kwamba ukiwa na ujuzi wa aina fulani tatizo fulani latakuwa limefika mwisho.Wakati tukiwa wadogo tulikuwa tunaambiwa taaluma fulani ukisoma utakuwa na fedha nyingi sana lakini matokeo yake kuna watu hawakuwahi hata kufikia theluthi ya ujuzi tulio nao na wanafedha kuliko wenye hizi taaluma.Kutokujua uhalisia wa vitu kwenye maisha umetufanya tuwa na mitazamo ya picha tu isiyokuwa halisi kulingana na kanuni za utendaji wa sayari hii.

Misongo Mingi ya mawazo kwenye kizazi chetu inatokana na vitu mbali mbali haswaa kutokujua uhalisia wa vitu.Miaka ya Nyuma tulifikiria kwamba Ukiwa Daktari basi Ugonjwa kwako binafsi ni maarufuku lakini ki-ukweli hata madaktari wenyewe wanaumwa pia na wanatafuta wengine wawape tiba.Miaka ya Nyuma tuliambiwa Ukiwa Mwanasheria basi Utakuwa na Uwezo wa Kukonewa na Vyombo vya Dola.Matokeo yake kumbe Taaluma hizi ni Zana za Kazi kuelekea mapambano ya changamoto zilizopo Mbele yetu.Haijalishi una ujuzi wa namna gani na taaluma kubwa kiasi gani kila mtu anachangamoto zake.Hata kama Ungekuwa na Fedha Nyingi na Kila kitu unachofikiri changamoto hazikimbii bali ni mwanzo mpya wa changamoto fulani.

Mwamvuli unaweza kuzuia Usilowe lakini Hauwezi kuzui Mvua Isinyeshe.Kila Safari Moja huanzisha nyingine.Kila siku kuna changamoto mpya lakini hakuna kitu kipya kwenye sayari hii.Kila unachokiona leo kilashakuwepo zamani.Mara zote napendaga kusema hakuna dhambi Mpya zote za kale.Taaluma ulio nayo ni sehemu ya utatuzi wa Changamoto kuelekea mafanikio yako na sio suluhisho la kila kitu kwenye maisha.Hauwezi kuzia changamoto/matatizo yasije lakini unaweza kuzitatua kwa kutumia taaluma ulio nayo.Changamoto hazikimbiwi bali Hutatuliwa.

Wahenga Walisema "Unapofikiri Kuna Amani Tele Kumbe Ndio Mwanzo wa Vita"

The Meaning of Marriage: Facing the Complexities of Commitment with the Wisdom of God.

Kitabu cha The Meaning of Marriage kimeandikwa na  Mchungaji Timothy J. Keller ambaye  alizaliwa mwaka 1950.
Timothy J.Keller ni Mchungaji wa Kanisa lijulikanalo  Redeemer Presbyterian Church kwenye Mji wa New York nchini Marekani.
Mwaka 1989 alipewa kanisa hili likiwa na Watu 50 tu lakini kwa Sasa lina washirika zaidi ya 5000 ambao wamejisalijili kwenye kanisa hilo la Mchungaji Timothy J.Keller.

Mchungaji Timothy J.Keller anaamini kwamba mafundisho mengi ya ndoa yanayofundishwa siku hizi yamepotosha maana halisi ya ndoa.
Mchungaji Timothy J.Keller ni mpinzani wa ndoa za jinsi moja pia ni mpinzani wa swala la kutoa mimba.Lakini anaamini Ndoa ni sehemu ya kumfanya mtu akue kiroho kufikia kiwango cha juu zaidi cha Maisha yake.

Mchungaji Timothy J.Keller anaamini Biblia ndio Muongozo sahihi kwenye swala linalohusu ndoa.

Kanisa la Mchungaji Timothy J.Keller linahesabika kuwa kanisa la 16 nchini Marekani lenye ushawishi mkubwa zaidi kwenye jamii.

Hiki ni Moja ya Kitabu cha Kikristo kilichofanya Vizuri kwenye gazeti Maarufu ya Nchini Marekani lijulikanalo Kama New York Times.
Mchungaji Tim J. Keller ameoa mke anaitwa Kathy na Sasa wana jumla ya Watoto watatu(David, Michael and Jonathan).

Kionjo Kutoka kwenye Kitabu hiki cha Mchungaji  Timothy J.Keller.

Marriage has the power to set the course of your life as a whole. If your marriage is strong, even if all the circumstances in your life around you are filled with trouble and weakness, it won't matter. You will be able to move out into the world in strength.”
Siku ya Jamamosi tarehe 23/03/2013,Huduma ya Soul Breakfast Chini ya kitengo cha Campus Ministry cha Kanisa la Victory Christian Center Tabernacle  a.k.a VCCT kutakuwa na sherehe ya Kutimiza miaka miwili toka huduma hii ya wanafunzi ianzishwe.Napenda kuchukua nafasi hii kama mmoja ya Wadau wa Huduma hii ya Wanafunzi kwenye mji wa Dar es Salaam kukukaribisha.
Inter-Collage Praise Worship Team ndio itaongoza Kusifu na Kuabudu.
Comedy itaongozwa na Mc Pilipili na King Chavala.
Msemaji Mkuu atakuwa Pastor Dr Huruma Nkone.
Vyeti Vitatolewa Siku Hiyo ...n.k

Usafiri wa Kwenda na Kurudi Utukuwepo bure kuanzia Saa Mbili na Nusu Asubuhi kwenye Kituo Cha Mwenge kama Uneelekea Maeneo ya Kiwanda Cha Coca Cola. 
Chai ya Nguvu itatolewa Bure.

Karibuni wote

Kirk Franklin

Kwa sasa unapoongelea mwanamuziki mwenye fedha za kutisha ulimwenguni kwenye Upande wa Muziki wa Injili huwezi kutaja jina Lingine zaidi ya Kirk Franklin.

Utajiri wa Kirk Franklin kwa sasa una thamani ya  Dola Milioni  $ 8.5.
Mwanamuziki huyu alizaliwa  Julai 26,1970 katika jimbo la Texas.


Baada ya Kuzaliwa Mama yake mzazi alimtelekeza na kulelewa na Shangazi yake aitwaye Gertrude .
Aliaanza kujifunza kupiga piano na miaka 4 na akiwa na Miaka 7 alianza kupata mkataba wake wa kwanza wa Kurekodi Albamu yake ya Kwanza Lakini Shangazi yake alikataa.


Mwaka 1996 ndipo alipomuaoa rafiki yake wa Karibu Tammy Collins.Wakati wanaoana watu hawa wawili kila mmoja alikuwa na mtoto mmoja mmoja kutoka kwenye mahusiano yake yaliyopita.Baada ya Kuoana Kirk Franklin pamoja na mkewe wamefanikiwa kupata  Watoto wa Wawili na  kwa jumla wana familia ya watoto wanne.


Wakati tukiwa tunafikiri maajabu yameisha kumbe ndio kwanza yaanaanza siku za karibuni Kitabu(Guinness World Records)  cha maajabu Duniani Kimefanikiwa Kuingiza katika Rekodi yake Balbu ambayo Haijawahi kuzima kwa muda mrefu wala Kuungua kwa takribani Zaidi ya Miaka 110 kwenye Kituo cha Zimamoto  namba 6 nchini Marekani katika Jimbo la California Eneo linaloitwa Livermore.

Balbu hii ambayo iliwekwa mwaka 1901 na kwanza kufanya rasmi kazi mwaka huo huo siku ya Tarehe 18 mwezi wa Saba.Balbu hiyo ambayo inafanya kazi Masaa 24 bila kuzimwa kwenye eneo la Injini.

Mwaka 1976 Balbu hiyo ilihamishwa kutoka kwenye eneo moja kwenda lingine huku kumbukumbu zake za uhamishwaji zikiwa zimetunzwa kwa ustadi mkubwa.Balbu hiyo ilipumzishwa kwa saa 22 tu mfululizo na ndipo ilowekwa tena na kuendelea kufanya kazi mpaka leo.


Adolphe A. Chaillet 
Mbunifu wa Balbu hiyo alijulikana kwa jina la Adolphe A. Chaillet na kisha kutengenezwa na kampuni ya Balbu ijulikanayo kwa jina la Shelby Electric Co. nchini Marekani.

Mpaka sasa wataalamu wengine wameshindwa kutoa sababu kwanini Balbu hiyo haijaungua kwa Muda mrefu lakini pia wameshindwa kutengeneza Balbu Nyingine kama hiyo ambayo yenyewe uwezo wa kuhimili muda mrefu bila Kuungua.

Kwa sasa Balbu hii imefungiwa Kamera Maalumu zakuipoza na Kuingalia muda wote kuendelea kupata kumbu kumbu na utendaji mzima wa Balbu hii yenye Maajabu ya aina yake.

Hii ndio Mistari 10 ya Biblia ambayo Imesomwa mara nyingi zaidi kwenye Mtandao wa Biblia ya Toleo la King James

Psalms 23:4  

Yea, though I walk through the valley of the shadow of death, I will fear no evil: for thou art with me; thy rod and thy staff they comfort me.

Philippians 4:13  

I can do all things through Christ which strengtheneth me.

John 3:16 

For God so loved the world, that he gave his only begotten Son, that whosoever believeth in him should not perish, but have everlasting life.

Genesis 1:1 

In the beginning God created the heaven and the earth.


1 Corinthians 13:11

When I was a child, I spake as a child, I understood as a child, I thought as a child: but when I became a man, I put away childish things.

2 Chronicles 7:14

If my people, which are called by my name, shall humble themselves, and pray, and seek my face, and turn from their wicked ways; then will I hear from heaven, and will forgive their sin, and will heal their land.”

Jeremiah 29:11

For I know the thoughts that I think toward you, saith the LORD, thoughts of peace, and not of evil, to give you an expected end.

Ephesians 6:12


For we wrestle not against flesh and blood, but against principalities, against powers, against the rulers of the darkness of this world, against spiritual wickedness in high places.

2 Timothy 1:7 

For God hath not given us the spirit of fear; but of power, and of love, and of a sound mind.

Genesis 1:2 

 And the earth was without form, and void; and darkness was upon the face of the deep. And the Spirit of God moved upon the face of the waters.”
What the Petitioner (PM RailaOdinga) is asking the court to do:
1. Set aside the results of the Presidential election as announced by IEBC on 9March 2013, and the declaration of Uhuru Kenyatta as President-elect and William Ruto as Deputy President-elect respectively, and declare asnull and void the whole electoral process leading to that declaration.
What the petition says:
· There was no free or fair presidential elections. Consequently no government could lawfully be formed by or from the purported declaration on 9th March 2013, of Uhuru Kenyatta and William Ruto as President-elect and Deputy President-elect respectively, by the IEBC and its chairman to the dishonor of the Kenyan people.
· The voter register was severally altered as to make it difficult to tell which one was used finally. For the purposes of the 4th March elections the registration of voters was carried out between 19November 2012 to 18th December, 2012, at the end of which the IEBC announced that 14,337,399 persons had registered as voters.
· In breach of the mandatory legal requirement, the IEBC has falsely, unlawfully and illegally in flagrant disregard of the law and its declaration of the result of the presidential election held on the 4th March, 2013 reflected the total number of registered voters as 14,352,533 well above the total number of registered voters as the date of closing of registration on 18th December, 2013. Indeed, during February 2013, the IEBC announced that they had discovered approximately 20,000 persons who had double registered in the December registration, and accordingly reduced the register tally to 14,267,572 voters as displayed on its website. The illegally inflated March 2013 register exceeded this corrected figure by some 85,000 voters
· The Petitioner avers that increasing the number of registered voters was intended to permit the IEBC to manipulate the presidential election held on 4th March, 2013 and their purported results and declaration, on 9th March, 2013 was null and void. That by abandoning the process of electronic identification at the polling stations and releasing results based not on the safeguarded, agreed, determined and credible electoral process it had promised and committed to, and by which legitimate expectations accrued, but a process that failed so significantly, substantially and endemically, IEBC effectively failed to reflect the will of the Kenyan people at the election.
· Arising from the acts and omissions of the IEBC, Hon. RailaOdinga and indeed the people of Kenya, were deprived of a free and fair election devoid of manipulation, an expectation which was denied, thereby irreparably undermining the entire process and result as declared on 9th March, 2013.
· Because of the IEBC and its chairman’s acts and omissions, the electoral process and the outcome thereof is so flawed in so fundamental and grave a sense, taken together or viewed separately, that it is difficult to tell whether the results were the true, lawful and proper expression of the Kenyan people's will.
· The EVID and BVR system and the electronic results transmission systems adopted by the First Respondent were so poorly selected, designed and implemented that they were destined to fail from inception, to the knowledge of the IEBC; the failure and collapse, on a catastrophic scale on the polling day, so fundamentally changed the system of polling and the number of votes cast, owing to inordinate and inexplicable delays at the polling stations thereby reverting Kenya to the discredited manual system, with all the attendant risks and opportunities for abuse and manipulation which in fact took place.
· The IEBC and its chairman’s purported official tally of registered voters inexplicably and mysteriously grew overnight by a large proportion on the eve of the election, notwithstanding that registration had closed some thirty days and was by law not permitted to be opened or changed.
· The results as declared and recorded by IEBC contained wide spread instances of manipulation of the returns through manipulation of Form 36 and in some instances the votes cast exceeding the numbers of registered voters, in flagrant breach of the fundamental Constitutional principles (see examples below).
· Although a common register was to be - and indeed was - compiled for all the six levels of elections in the general elections of 4th March, 2013, it turned out from the results declared by IEBC that the total number of registered voters and votes cast in respect of the presidential elections in some instances exceeded that of the registered voters and those cast for Parliamentary elections after taking due account of any spoilt or rejected or disputed votes to the detriment of RailaOdinga. The numerous instances of huge discrepancies in the total numbers of votes declared by the First and Second Respondent in the presidential election held on 4th March, 2013 is inexplicable upon any reasonable hypothesis other than the existence of actual ballot stuffing, multiple voting or gerrymandering or inflating of the numbers of votes in the tallying thereof by the IEBC or their officers or their condoning of or connivance in the same to the advantage of Uhuru and Ruto thereby rendering their alleged win invalid, illegal, null and void.
Anecdotal examples of widespread anomalies:
Glaring anomalies were observed in the process from voter registration, to transmission of results, to tallying.
(a) the result were declared on the basis of unsigned Form 36
b) multiplicity of Form 36, and variants of entries in some constituencies
(c) alterations on files and
(d) brazen disregard by the IEBC of the entries on the files of constituencies which were eventually reflected in the final tally of Presidential election results and which were announced without signed verification Form 34s.
Votes cast exceeded the number of registered voters, including Tiaty, Laisamis, Igembe Central, Buri, Chuka, IburiIgambaNgombe, Lari, Kapenguria, Saboti, Turbo, Marakwet West, Kajiado West, Bomet East, Mt Elgon, Langata and Aldai.
Results in Form 36 disclosed by the First Respondent were materially different from the results that were posted in the final tally of the presidential results published by the First Respondent. This included in Webuye East, Webuye West and Igembe Constituencies.
Registered voter numbers in polling stations were inflated in Form 34 contrary to what was contained in Form 36. These included Kaproi Nursery School, Metipso Primary School, Maina Primary School, asaibul Primary School, Sewerwa Nursery School, Liter Secondary School, Chesongoch Catholic Church, Mungiwa Primary School, Chawich Primary School and Lemeuywo Primary School. In most of those circumstances, more votes were cast than the total number of registered voters.
More than two Form 36 reflecting different returns. These included Kikuyu Constituency, Juja Constituency, Chuka Constituency, Thika Constituency.
Alterations in Form 36 without acknowledgment including Kiambaa and Limuru Constituencies.
More valid votes cast in some constituencies reflected in Forms 36 than in Form 34 including in Chesumei, Emngwen and Ainamoi.
Different entries in two Forms 36 submitted in respect of the same constituency for example in Mathira Constituency.
Published results materially different from the results reflected in the County tallying, for example in Nakuru, not to mention the material variation between the verbal declaration made by the various Commissioners of IEBC at the national tallying centre allegedly after verification of results and the fiinal figures which are set out by the IEBC including those of South Imenti, Igembe South, Lagdera, North Imenti, Central Imenti, Boment East and Sigor.
***
Highlights/Quotes from the affidavit
" I believe that First and Second Respondents in breach of the Constitution, failed to establish systems which are accurate, secure, verifiable, accountable and/or transparent and indeed declared results which in many instances had no relation to votes cast at the polling station, developed methods which were opaque and intended to manipulate the results in the course of which the Petitioners’ representatives were altogether excluded from the process."
" In the final tally, the total number of votes cast in the Presidential Elections differed materially from those declared by the First and Second Respondents for purposes of the Gubernatorial and Parliamentary elections which took place on the same date clearly attesting to my belief that massive electoral fraud and malpractice occurred or permitted to occur by the First and Second Respondents in contravention of the requirements of the Constitution and the legislative framework in place as regards the 4th March, 2013 presidential election."
Highlights/quotes from the petition/re electronic system:
"its failure and collapse, on a catastrophic scale on the polling day, so fundamentally changed the system of polling and the number of votes cast, owing to inordinate and inexplicable delays at the polling stations thereby reverting Kenya to the discredited manual system, with all the attendant risks and opportunities for abuse and manipulation which in fact took place; "
"Respondents in breach of the Constitution, failed to establish systems which are accurate, secure, verifiable, accountable and/or transparent and indeed declared results which in many instances had no relation to votes cast at the polling station, developed methods which were opaque and intended to manipulate the results in the course of which the Petitioners’ representatives were altogether excluded from the process."
"the numerous instances of huge discrepancies in the total numbers of votes declared by the First and Second Respondent in the presidential election held on 4th March, 2013 is inexplicable upon any reasonable hypothesis other than the existence of actual ballot stuffing, multiple voting or gerrymandering or inflating of the numbers of votes in the tallying"
"A curious and very concerning feature of the First Respondent's conduct was that it allowed Kencall to co-host both its server and that of the TNA, which of course may compromise the integrity of the electoral process but at very least gives the very real impression that the TNA has access to sort of information which is at the very least initially confidential to the First Respondent."

1.Bill Clinton and Hillary Clinton

Aliyekuwa Raisi wa Marekani Bill Clinton na Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje Bibi Hillary Clinton ndio Ndoa ambayo inashikilia namba moja kuwa Ndoa ambayo imewavutia watu wengi zaidi katika mwaka 2012 kwa mujibu wa mitandao mbali mbali.Ndoa hii ilifungwa mwaka  1975,Octoba 11.Kwa mara ya kwanza walikutana mwaka 1970.Pamoja na Ndoa hii kupita kwenye misuko suko mbali mbali lakini bado imeendelea kuwa Imara na Inaonekana kuwa ni ndoa yenye afya zaidi kuliko nyingine zaidi katika mwaka 2012.

2.Bill Gates and Melinda Gates 

Pamoja na Bill Gates kushikilia namba moja kwa utajiri lakini bado anaendelea kufanya vizuri kwenye ndoa yake yeye pamoja na mkewe Melinda.Ndoa ya Bill Gates na Melinda ndio inashikilia namba mbili kwa kupendwa na kuvutiwa zaidi na watu wengine duniani kulingana na mitandao mbali mbali kwa mwaka 2012.Ndoa hii ilifungwa mwaka 1994 January 1 kwenye visiwa vya Hawaii.BAdo ndoa hiii haijatetereka hata kidogo kwa muda mrefu wamekuwa wakifanya kazi pamoja ikiwa ni Pamoja na mfuko wao wa Misaada ulimwenguni kote wenye Jina la Bill and Melinda Gates Foundation.

3.Barack Obama and Michelle Obama

Raisi wa Marekani Barack Obama na Mkewe Michelle Obama ndio ndoa ambao inashikilia namba tatu ilionyesha kuwavutia watu zaidi katika mwaka 2012 kwa mujibu wa mitandao mbali mbali.Kwa mara ya kwanza wanandoa hawa walikutana mwaka 1989 lakini harusi Rasmi ilifungwa Octoba 3,1991.Huyu ndie Rais wa 44 wa Taifa lenye Nguvu zaidi na Ushawishi mkubwa zaidi Ulimwenguni kwa sasa.
Mwaka 2012 katika Uchaguzi wa Nchii Hiyo familia yake ndio inahesibika ilitoa mchango mkubwa kwenye ushindi wa kiti cha U-Raisi kwa mara nyingine baada kuonekana kwamba Baba wa Familia hiyo angelishindwa kwa mujibu wa kura za maoni na maneno ya mitandao mbali mbali.

4.Marissa Mayer na Zack Bogue.

Mwaka 2009 ndipo Marissa Mayer na Zack Bogue walipoamua kuoana na kuwa mke na mume.Ndoa hii ikiwa bado haina muda mrefu lakini imeingia kwenye rekodi katika mwaka 2012 kuonyesha ni moja ya ndoa ambazo zinawavutia watu wengi.Marrisa Mayer(Mwanamke) aliamua kuacha kazi kwenye Kampuni ya Google  kama msaidizi wa CEO na kuamua kujiunga na Kampuni Ya Yahoo na alifanikiwa kuwa CEO wa kampuni ambayo ilikuwa ikipoteza wateja kwa kasi na kupoteza umaarufu wake wa awali na kuifanya kupoteza mapato yake kwa kiasi kikubwa.Mdada huyo utajiri wake kwa mwaka unakadiriwa kufikia kiasi cha dola Milioni $ 300 kwa mwaka.
Pia ndoa hii inaingia kwenye Category ya  ndoa bora miuongoni mwa wanateknolojia(Information Technology Category) katika mwaka 2012.


5.Diane Sawyer and Mike Nichols

Mwaka 1998 ndipo watu hawa wawili walipoamua kufunga ndoa na kuishi pamoja kama mke na mume.Diane ni moja ya wanawake maarufu na watangazaji wa vipindi mbali mbali kwenye luninga kwa muda mrefu piaalifanikiwa kupata Tuzo kama Director Behind the Scene wa movie mbali mbali kwa kipindi cha nyuma.Ndoa hii inashika namba tano kuwa ni moja ya ndoa inayopendwa na kuvutia watu wengi zaidi kwa mwaka 2012 kupitia mitandao mbali mbali Ulimwenguni.Wote hawa wawili ni wafanyakazi wa vyombo vya habari kwa pamoja.
Hakuna mtu ambaye ameishi kwenye sayari hii katika siku zote za uhai wake bila kukosea kwenye jambo lolote.Mafanikio yote tunayoyaona leo yametokana na makosa mengi ambayo watu waliyafanya siku za nyuma.Yaani kwa maana nyingine hatuwezi kujua tumepatia juu ya jambo fulani bila kujua kutokupatia kuna sura gani.Ili shilingi ijulikane ni shilingi lazima iwe na pande mbili.Hakuna shilingi ambayo siku zote ina upande mmoja ndivyo pia maisha yalivyo.
Ukisoma Historia za watu mbali mbali maarufu na mashuhuri utakuja kukuta hapo mwanzo walikosea sana juu ya kile walichokuwa wanakifanya baada ya kugundua kwamba wamekosea ndipo hujaribu kufanya marekebisho kwanza kuleta muonekano bora juu ya jambo waliloliamini kuwa ni sahihi.


1.Makosa Uliyoyafanya Wewe Binafsi(You are Own Past Mistakes)

Kukosea ni sehemu ya maisha lakini sio maisha yote,Unapogundua umekosea unanyanyuka na kuendelea mbele.Makosa yako binafsi ni moja ya walimu wazuri waliokufandisha ndio maana leo upo hivyo ulivyo,Hauwezi kuishi zaidi ya makosa ambayo uliyoyaona kwako binafsi.
Kama uliwahi kufukuzwa kazi kwa sababu umekosea kufanya jambo fulani kwa uangalifu,Siku unapopata kazi mpya unajitahidi sana kile kilichokufukuzisha kazi  usikirudie tena.Iwapo Kuna wakati huwa tunatumiaga hela zote bila kujali siku unapopatwa na dharura inayohitaji fedha ya muhimu sana na wewe fedha zote ulitumia vibaya inakufundisha kwamba siku ukipata fedha nyingi lazima kuna kutunza kiasi fulani cha fedha hata iwapo dharura itatokea tena usiaibike.Usiogope kukosea maana makosa yako ya leo ndio yanakusaidia kutengeneza maisha yako ya kesho.
Iwapo tusingejua maisha ya dhambi yakoje  na matokeo yake hapa Ulimwenguni tusingejua hata Mungu anafwananaje kwenye maisha yetu ya kila siku.
Mwanzuoni mmoja aliibuka na kusema Kwamba kama Haukuwahi Kukosea juu jambo lolote basi tambua haukuwahi kujaribu kitu kipya kwenye maisha yako.



2.Makosa ya Watu Wengine(Others Mistakes).

Wahenga walisema ukiona mwenzio ananyolewa Nywele basi wewe wewe weka maji Kichwa.Unapofanikiwa kumuona Mtu anakata mti na panga butu alafu akashindwa kumaliza kazi kwa wakati basi wewe kesho ukitaka kukata mti utajifunza kulinoa panga hilo.Hakuna mtu ambaye ana uwezo wa kuishi na kufanya kila kitu na kujifunza kwa makosa ya kwake binafsi tunawahitaji wengine ili kuweza kujifunza.Makosa ya mtu mwingine leo ndio Mafanikio yako ya kesho.
Ukiona mtu amefilisika na matumizi mabaya yake ya fedha na kushindwa kuendesha miradi alioianzisha siku zote utatumia makosa ya mtu yale kama sehemu ya rejeo ili kutoweza kufanya makosa aliyoyafanya yakapelekea matokeo mabaya.Mara nyingi watu waliojifunza kusikiliza na kuangalia makosa ya wengine juu ya jambo fulani kwa umakini wamekuwa na mafanikio zaidi kwenye jambo husika kuliko hata yule ambaye mwenyewe ambaye amewahi kukosea.
Tunawahitaji wengine ili kuweza kuendelea mbele.



Mwisho wa Siku tunaendelea kusema Epuka kuishi kwenye makosa yaliyopita lakini yatumie makosa kama mwalimu wako,Yaliopita si ndwele lakini tugange yajayo.Usiogope kukosea jaribu kufanya vitu vipya kukosea ni sehemu ya maisha.Maisha ni safari ambayo haina mjuzi bali wote tuwanafunzi kwenye kila jambo.Ishi ndoto zako jaribu kutafuta fursa mpya za maisha na jaribu kuzitumia bila woga kwa sababu Makosa yako ya Jana ndio Mafanikio yako ya Kesho.
Mwaka 1996 Sheria ya Ndoa za Jinsia Moja ilisainiwa na  aliyekuwa Raisi wa 42 wa Marakeni Bill Clinton ijulikanayo Kama Defense of Marriage Act a.k.a DOMMA.

Siku chache zilizopita Raisi huyu amaiomba Mahakama Kuu nchini Marekani kuifuta Sheria Hii kwa sababu ya Mapungufu Mbali Mbali yaliopo kwenye hii Sheria.

Raisi huyu Ameendela kueleza kwamba kwenye Sheria ya Ndoa ijulikanayo kama DOMA (Defense of Marriage Act )kusema wazi kwamba ndoa ni Muunganiko kati ya Mwanamke na Mwanaume tu na sio zaidi ya Hapo.Lakini zaidi ya hapo Mahakama Kuu ya Marekani imesema itatoa maamuzi yalio rasmi kisheria mwezi Juni mwaka huu kuhusu ndoa za jinsia moja.

Majaji wataamua kama Defense of Marriage Act kama inashabiliana na kanuni za Taifa linaloheshimu uhuru ,usawa na haki kwa ujumla na ambazo hazipingani na Katiba Mama ya Nchi Ya Marekani.

Raisi huyo aliendelea kusema kwamba Wakati anapitisha Sheria hiyo Ulikuwa ni wakati tofauti na Sasa sababu hakuna hata jimbo moja lililokuwa linatambua ndoa za jinsia mmoja lakini majimbo mengine yilikuwa yinafikiria kufanya hivyo na wengi walikuwa wanataka mabadiliko ya haraka.Kwa Mfano Mpaka  kufikia sasa Majimbo zaidi ya Tisa ikiwemo Colombia District watu wenye mahusiano ya jinsia moja hawewezi kupatiwa huduma za kajamii kama ilivyo kwa watu wenye mahusiano ya jinsia tofauti…..USA Today ndio limeripoti .

Hii inaonyesha kwamba Viongozi wa Kisiasa wanapokuwa madarakani wanapenda kufanya maamuzi ambayo yatawapelekea wao kubaki kwenye madaraka au kulinda hadhi za vyama vyao vya kisiasa au kwa maslahi yao binafsi ama ya kundi fulani bila kuangalia athari zake za badae.