Wakati Nchi zetu za Ukanda wa Afrika Mashariki zikiwa na bado na maswali mengi juu ya viongozi wa Dini Wanawezaje kuwa Matajiri wa Kupindukia lakini Sivyo Ilivyo katika nchi za Afrika Magharibi haswaa nchini Nigeria.Siku Chache Zilizopita tumekuwa tukifwatilia mitandao mbali mbali ya chini Nigeria na tukakutana na hiki,Wachungaji wenye Asili Ya Nigeria na Wanaoishi Nigeria ambao ni matajiri zaidi kuliko wachungaji Wengine.

1.Bishop David Oyedepo

Huyu ndie mwanzilishi wa Kanisa na huduma ya  Living Faith World Outreach Ministry, a.k.a Winners Chapel Ulimwenguni mwote.Ndie Mchungaji na Askofu tajiri zaidi kuliko wote nchini Nigeria.Utajiri wake unakadiriwa kuwa kiasi cha Dola Milioni $ 150.Takwimu hizi zilikusanywa Mwaka 2011-2012.Huduma ya  Living Faith World Outreach Ministry, a.k.a Winners Chapel ilianzishwa mwaka 1981 pia ndio Kanisa kubwa zaidi kuwahi kutokea katika bara la Afrika.Kanisa lake linachukua zaidi ya Washirika 50,000 hawa wakiwa wamekaa kwenye viti bila bugudha yeyote.Mchungaji huyu anamiliki ndege 4 zake binafsi.Ni Mmiliki wa Chuo Kikuu kiitwacho Covenant University nchini Nigeria.Amefanikiwa kuwa na Kampuni Yake ya Uchapishaji Iitwayo Dominion Publishing House.Zaidi ya hapo anamiliki Shule yake Ya Sekondari Binafsi nchini humo ijulikanayo Kama Faith Academy.



2.Chris Oyakhilome

Huyu ndiye mwanzilishi wa Kanisa na Huduma ya Believers’ Loveworld Ministries, a.k.a Christ Embassy.Utajiri wake Unakadiriwa kufikia kati ya dola Milioni  $ 35 - $ 50 kwa mwaka 2011-2012.Kanisa la Believers’ Loveworld Ministries, a.k.a Christ Embassy lina Zaidi ya washirika 40,000 duniani kote na wengi wao wakiwa Viongozi wa Serikali na Wamiliki wa Makampuni Mbali mbali.Anamiliki Vitu mbali mbali ikiwepo Kituo cha Utangazaji cha Televisheni Chenye jina la LoveWorld TV Network. Pia amefikiria kuanza kuwekeza kwenye Hoteli na Nyumba za Upangaji sehemu Mbali mbali Ulimwenguni.


3.TB Joshua

Huyu ndio mwanzilishi wa Kanisa na Huduma ya Synagogue Church Of All Nations (SCOAN) nchini Nigeria.Utajiri wake unakadiriwa kufikia kiasi cha Dola Milioni $ 10 - $ 15 .Anamiliki Jengo la Kanisa lenye uwezo wa kuchukua Washirika 15000 wakiwa wamekaa bila Shika wa tatizo.Kanisa la Synagogue Church Of All Nations (SCOAN) lilianzishwa Mwaka 1987.Kwa sasa ana matawi katika nchi Mbali mbali nje na ndani ya Afrika.Miaka Minne aliyopita alitoa msaada wa Fedha Wenye thamani ya Dola Milioni $ 20 kwa kituo cha Matibabu cha Jeshi kilichokuwa kinaitwa Niger Delta Militants.Ni mmiliki wa Kituo Cha Utangazaji cha Televisheni chenye Jina La Emmanuel Tv.




4.Pastor Matthew Ashimolowo


Huyu ndiye mwanzilishi wa Huduma na Kanisa lijulikanalo kwa jina Kingsway International Christian Centre (KICC).Lenye Makazi yake nchini Uingereza.Utajiri wake Unakadiriwa kuwa Kiasi cha dola $6 – $10 .Mwaka 2009 Kanisa Kingsway International Christian Centre (KICC) lilitangazwa kwamba ndilo Kanisa Kubwa Zaidi la Kipentekoste nchini Uingereza.Pastor Matthew Ashimolowo ni mmiliki wa Baadhi ya Vituo vya Uandishi wa Vitabu  ambavyo Huandika Makala Mbali mbali za Vitabu pamoja na Utengenezaji wa Documentaries Mbali mbali.


5.Pastor Chris Okotie


Huyu ndiye Mwanzilishi wa Kanisa la Household of God Church nchini Nigeria.Utajiri wake unakadiriwa kufikia kiasi cha Dola Milioni $3  -$10.Miaka Michache iliyopita ni mmoja wa wachungaji waliojitokeza kugombea Uraisi wa Nchi ya Nigeria kwa vipindi vitatu tofauti na huku akiwa kiongozi wa Chama Chake Binafsi cha Siasa.Kiasi kikubwa cha Washirika wake ni Macelebrity wa Nigeria pamoja na watu wengine maarufu kwenye kila eneo.Pia kwenye Miaka ya 1980's ndie Mwanamuziki Mzuri wa Pop kwa kipindi hicho Nchini Nigeria.Anamiliki Vitu kadha wa Kadha ikiwemo magari yenye thamani kubwa zaidi Ulimwenguni kama Hummer na Porsche.