Tarehe 1/9/2013,Majira ya Alasiri kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza Patawaka Moto kwa Pambano kali la Ndondi(Ngumi) Zisizokuwa na Ubingwa Kati ya watangazaji wawili Maarufu wa Kituo cha Radio za Injili hapa Tanzania.Akiendelea kuongea na Waandishi Wahabari na Bloggers wa Kikristo Neema Gasper alieleza kwamba Kundi Moja Maarufu la Dancing la Kikristo litakuwepo kwenye Ukumbi Siku Hiyo na Pia Bila Kusahamu Wanamitindo wa Kikristo watashiriki Kuonyesha Mavazi Mbali Mbali ya Kikristo Katika Ukumbi wa Huo

Siku chache zimepita tangu Neema Gasper alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari pamoja na Blog za Kikristo juu ya ujio wake mpya wa Albamu yake itwaayo "SHUJAA" akiendelea kuongea na Waandishi Wahabari na Bloggers ameeleza kua mapato yatakayopatikana katika uzinduzi huo asilimia fulani ya mapato itapelekwa kusaidia wajane na yatima  waishio katika mazingira magumu.Albamu ya "SHUJAA" itakuwa na Nyimbo Takribani 8.

Neema Gasper Akiongea na Bloggers na Waandishi wa Habari wa Kikristo
Akiendelea Kuongea na Waandishi wa Habari na Bloggers aliendelea kufafanua kwamba Mbunge Machachari na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samuel Sitta ndiye atakayekuwa Mgeni Rasmi kwenye Uzinduzi huo

Mh Sumuel Sitta,Waziri wa Ushikiano wa Afrika Mashariki
Waimbaji wengine wa nyimbo za injili watakaomsindikiza Neema Gasper katika uzinduzi wa album yake ni pamoja na Rose Mhando,Bahati Bukuku,Madam Ruth, Martha Mwaipaja, Everine Msoma, Ambwene Mwasongwe, Maxmillian Machumu, Edson Mwasabwite Enock Jonas na wengine wengi.


Vingilio katika uzinduzi huo vimepangwa kuwa Viti maalum Tshs 10,000/=, Kawaida Wakubwa Tshs 5000/= na watoto sh Tshs 2000/= wageni 50 wa kwanza watajipatia mafuta na Losheni kutoka kwa Gress Product

Ticket zinapatikana  Praise Power Radio,Wapo Radio, na pia ticket pia zitapatikana mlangoni siku hiyo hiyo ya uzinduzi katika ukumbi wa Ubungo Plaza.

Dont Dare To Miss!!!!