Mtandao wa Amazon ni miongoni mwa mitandao michache Ulimwenguni inayofamika kwa kufanya mauzo ya vitu mbali mbali kupitia njia ya Mtandao.Mtandao huu unauza Muziki na vitu kadha wa kadha kupitia njia ya Online lakini siku ya Leo Tumeamua Kuangalia Muziki wa Injili na Wanamuziki wake wanaofanya vizuri kwenye Mauzo kwa Muda mrefu zaidi kulingana na Mtandao huo.


1.Mountain High... Valley Low

Mountain High... Valley Low ni Albamu ya Muziki wa Injili iliyoachiliwa mwaka 1999 na Mwanamuziki Maarufu wa Injili nchini Marekani Yolanda Adams chini ya Lebo yake ya Elektra Records.Albamu hii mpaka sasa imeshachukua  tuzo mbali mbali kama Grammy Award pia kwa Mujibu wa Mitandao mingine ya Mauzo kwa ujumla mpaka sasa Yolanda Adams na Albamu Hii ameshafanya mauzo ya Nakala milioni 2,374,000.Albamu hii ina nyimbo takribani 11 na zote zimefanywa kwenye Studio ya Elektra Records.Hii ndio Albamu inayoshikilia namba moja kulingana na mtandao wa Amazon.


2.Tri-City4.Com

Mwaka 2001 Kundi la TRI-CITY SINGERS lilifanikiwa kupewa tuzo ya Grammy baada ya albamu yao ya TRI-CITY4.COM kufanya vizuri mwaka 2000.Albamu hii iliachili rasmi mwaka 200,februari 29.Albamu hii ina nyimbo takribani 16 zilizotengenezwa chini ya Lebo ya EMI Gospel.Kundi hili lilianza kufanya vizuri baada ya mwanamuziki Donald Lawrence kushika hatamu baada ya Director aliyekuwepo kung’atuka kwenye nafasi aliyokuwa anaishikili.Hili ni Kundi la Nchini Marekani ambalo lilichukulia kama kwaya bora kuwahi kufanya mauzo zidi kwenye Mtandao wa Amazon.Hiii ni Albamu namba Mbili kwa Mauzo kulingana na Mtandao wa Amazon.


3.2nd Chance

Siku ya July 30,2002 ndipo Albamu ya Pili Ya Mwanamuziki Karen  Clack Sheard ndipo ilipoingia Sokoni rasmi ikiwa na Jina la 2nd Chance.Kabla ya Kuachilia Albamu hii Mwanamuziki Karen Clack Sheard alisumbuliwa na Tatizo la Mishipa ya Damu ya kwenye paji la Uso Kupasuka.Madaktari walisema Uwekano wa kupona Ugonjwa huo ni Asilimi 2% na asilimia iliyobaki ilikuwa ni Kifo tu haya yote yalitokea mwaka 2001.Baada ya Kuanza kuachia Mauzo ya Albamu hii mwaka 2003 kupitia wimbo wa The Heavens Are Telling ndipo alipoweza kuchaguliwa kuingia kweny Kinyang’anyiro cha Tuzo za Grammy nchini Marekani.Mpaka sasa Albamu hii yenye nyimbo 13,Inaendelea kushikilia nafasi ya tatu kwa  kufanya mauzo makubwa ambayo hayajawahi kufikiwa mpaka sasa kwenye mtandao wa  Amazon.


4.I Believe

Mwaka 1996 mwezi Machi tarehe 12 Mwanamuziki Marvin Sapp ndipo alipoingia rasmi kwenye game za Muziki wa Injili nchini Marekani.Mpaka Sasa Marvin Sapp ameshaachilia albamu 9 za Muziki wa Injili.Kwa Mujibu wa Mtandao wa Amazon Albamu ya I Believe iliyoachiliwa June 11, 2002 ndio inayoshikilia nafasi ya Nne kwenye Mtandao huo kwa Mauzo makubwa kuwahi kutokea.Albamu hii ina jumla ya nyimbo takribani 13.Albamu hii ilitolewa chini ya Lebo ya Verity nchini Marekani.Hii ndio albamu ambayo rekodi yake pia ya mauzo haijawahi kuvunjwa na Inaendeelea kushikilia namba nne kwenye mtandao wa Amazon.


5.Grace & Mercy

Mwaka 1967 Mwanamuziki Marvin Sapp ndipo alipozaliwa kwenye mji Grand Rapids, Michigan nchini Marekani.Baada ya Mwaka 1996 kuamua kuimba Kama mwimbaji Binafsi mwaka Desemba 16,1997 ndipo  alipoachilia albamu ya Grace & Mercy.Mwaka 1998 albamu hii ichaguliwa kuingia kwenye Kinyang’anyiro cha Tuzo za Grammy.Albamu hii ina takribani Nyimbo 10 pekee yake.Huu ndie mwanamuziki pekee aliyefanikiwa sasa kuingiza Albamu 2 kwenye Tano bora kwa Mauzo ya Muda mrefu na yanayoshikilia Rekodi ambayo mpaka sasa haijavunjwa wala kuondolewa katika nafasi ya nne na ya tano kulingana na mtando huo wa Amazon.