Maisha ya mwanadamu yamejengwa katinga msingi wa uwajibikaji wa mtu binafsi kwenye maswala mbali mbali ambayo tunakutana nayo kila siku kwenye maisha yetu.Bila uwajibikaji a kuchukua hatua kwenye kila jambo na kuwa watendaji kwenye kile tunachokiamini ni sawa na kupigia mbuzi gitaa ukitegemea acheze,Wahenga walisema Kuwa Ukitwanga PiliPili kwenye Kinu Mshahara wake ni Kukohoa,Kwa Maana nyingine kile anachopanda mtu ndicho anachovuna mtu.Ukipanda maisha ya kulaumu kwa makosa na changamoto mbali mbali kwenye maisha unayokutana nayo hakukufikishi kokote,mwisho wa siku utaishia kuvuna lawama na malalamiko.

Maisha yetu ya jamii na utendaji wetu wa kila siku tumeyajenga kwenye kulaumu chanzo cha tatizo zaidi badala ya kutumia muda mrefu kujadili sulihisho la tatizo.Utamaduni wa kulaumu kwenye maisha ya mtanzania ni kama uji na mgonjwa.Mara zote tunashindwa kuweza kutafuta suluhisho wa tatizo na changamoto tunazokumbana nazo.

Siku za Karibuni tumepatwa na Kifo Cha Mwanamuzi wa Bongo Fleva Anyejulikana kwa Jina la Albert Magwair.Baada ya Kifo chake kutokea Watu wametumia Muda Mrefu kukilaumu kwamba Kituo Fulani cha Radio ndio Kimesababisha Kifo chake,Baada ya Kusoma Report ya Madaktari ambayo imekuwa ikisambazwa kwenye mitandao Mbali Mbali Imekujulikana Kwamba Ndugu yetu alikufa kutokana na Uchovu na Matumivi ya Vilevi na Dawa Za Kulevya Baada ya Mwili wake kufanyiwa Uchunguzi(Habari Zisizo Rasmi).Nikajiuliza Je  Kituo hiki Ndio Kilimtuma atumie Vilevi na Madawa ya Kulevya.Je Kama Kituo Hiki kilimnyonya na Kusabishia Msongo Wa Mawazo Kwanini Yeye Binafsi asingetafuta njia Mbadala ya Kujinasua Kwenye Jambo hili la Kunyonywa?Kuna Mengi Sana.Lakini Baada ya tukio la Kifo kutokea Je hawa wengine waliobaki ambao wengine ni waathirika wa Matumizi ya Madawa ya Kulevya na Vilevi tunawasaidiaje?Malaumu hayasaidii.Tunapaswa kutafuta suluhisho la kudumu juu ya matatizo yetu Binafsi yanayotukabili badala ya Kutupia wengine lawama.

Mtu binafsi ndiye Suluhisho la Matatizo na Changamoto zake Binafsi,Hakuna mtu anayeweza kusimamia kukusaidia kuleta utatuzi wa changamoto zako binafsi.Unapolaumu wengine na wao wankulaumu pia kwa uzembe ulioufanya.

Wewe binafsi ndio unaweza kusimama na kuweza kutafuta suluhisho la kudumu kwenye kila kunachokukabili kwenye kila hali maishani mwako.Muda Mwingi wa lawama na malaumu hausaidii.Mara nyingi tumekutana na mfano wa Kesi za Mama wa Kambo na Watoto wa Kambo.Watoto hawa wa tumewajengea uwezo mkubwa wa kuwalaumu wamama ambao wanawalea na kuwafanya waonekane wabaya.Pamoja na Changamoto wanazokutana nazo tulipaswa kwajengea uwezo wa kupambana na changamoto wanazokutana nazo badala ya kuwajengea uwezo wa kulaumu.Kumbuka hata wakiwa watoto ipo siku Moja watakuwa watu wazima je hapo wataendelea kuwalaumu Mama zao wa Kambo .hapana.Hapa ndipo watapaswa kujisimamia wenyewe kwa majukumu yao ya kimaisha.Suluhisho la Mtu na Changamoto ni Mtu Mwenyewe na Sio Lawama.

Shangazi yangu siku Moja alinieleza kwamba mara nyingi watu ambao wengi ni wepesi wa kulaumu basi hata utendaji wao na maisha yao ni ya kubahatisha.Ni Rahisi kuilaumu Serikali Yetu haitupi fursa za maendeleo lakini cha kushangaza kuna watu wanaendelea je hawa wanaendeleaje?Je wao wana Mabawa au Wao ni Super Human?

Maisha ya Maendeleo ya Jamii Ni Watu wenyewe,Serikali yoyote duniani unayoiona ni Taswira ya Wananchi wake.Kuishutumu Serikali Kwenye Miasha yetu mabovu ya kila siku ni Kama kujaribu Kupigana na Kivuli Chako Mwenyewe.Unapoona Ubabaishaji kwenye Serikali,Tafuta Muda uangalie utendaji wa maisha ya Wananchi wake wa kila siku,ndipo utagundua serikali na wananchi wake hawatofautiani kwenye maswala mbali mbali.Kumbuka Serikali ni Watu na Iliwekwa na Watu.Kuendelea kulaumu hakusaidi.Dawa ni Kutafuta Suluhisho kile kinachotukabili kwenye maisha yetu ya kila Siku.Tutumie Muda mwingi kufikria kitu gani tunapaswa kuwa nacho maishani mwetu badala ya kulaumu kusiko na sababu za msingi.Sisi  tuwajibike kwanza ndipo tutafute mengine.

Wakati unatumia muda mwingi kulaumu kwenye tatizo ulilo nalo Wengine wanatumia fursa za lawama zako kuendelea.

Wakati wewe unaona lawama ndio suluhisho la maisha yako ndipo wenye akili wanapokaa chini na kusaidia kutafuta sulusho ya lawama zako na mwisho wa siku suluhisho la mtu mwingine kwako huwa la Muda tu sababu hajui ni haswa unahitaji maishani mwako,Suluhisho la kudumu lipo Ndani yako,Na watu wanapoendelea kutafuta suluhisho zaidi juu ya tatizo lako kwenye maisha yako ya lawama siku zote utaendelea kuwa mtumwa kwao,maana utatumia nguvu nyingi na gharama kubwa kuweza kupata suluhisho la Muda la mtu mwingine kwenye maisha yako.Kuchukua kutumia suluhisho la Mtu Mwingine kwenye maisha yako ni kama kujaribu Kuiba Kivuli cha Jirani yako Kisha Ukitegemea kifwanane na wewe na kikutoshe.

Mwisho wa Siku wakati Lawama zako zinaendelea kwa watu wengine Maisha Bado yanaendelea kila siku na Watu wanafanikiwa kwenye ndoto zao kwa Kukufanya mtumwa wa kutumumikia ndoto zao.Kufa kwa Imamu Sio Mwisho wa Ibada,Maisha yanaendelea na kazi zinaedelea na Ujenzi wa Fikra Huru na za Haki Unaendelea.Unapoendelea kulaumu hata siku zako za kuishi zinakuwa chache maana utayatumikia matatizo badala ya kutumikia Kufurahia maisha ambayo wewe binafsi ndio jibu la Maisha yako.
Nikiwa nimeamka Siku ya Tarehe 1/1/1994,Mama aliniambia Hata sisi tuliwahi kuwa kama wewe ulivyo.Wakati maneno hayo yanasemwa sikuelewa yana maana gani,Maana sikuwahi kufafanuliwa ila niliona siku zikienda na zikisogea mbele,Mara nikajikuta namaliza Level Moja Ya Elimu huku nikienda Nyingine na Mara Elimu Ya Juu.Naam Muda unaenda na Muda haurudi.Kufanya malengo yoyote bila kuwa na mipaka ya muda bado hauwezi kufikia lengo.Hakuna Lengo Lisilokwenda na Muda.

Jamii yetu ya Kitanzania imelelewa kuishi kwamba kesho ipo tu,Lakini cha kushangaza hatufikirii kama hiyo kesho sio yetu maana hakuna kilicho na uhakika wa kuiona Kesho hiyo.

Baada ya Kusoma Kidogo..Zamani tukiwa tunakuwa Shule za Msingi Tulikuwa tunafundishwa kumeza Nyakati Mbali Mbali za Sentensi kwa Kingereza Yaani Tenses,Kwa Mara ya Kwanza Nilisikia Kitu Kinaitwa Future Tense Mwaka 1996,Niliimeza Baada Ya Miaka Michache Kupita Kuna Siku Nikajiuliza Ivi Kuna Future Tense au ni Future Time na Hiyo Future Time or Future Tense Zinatoka wapi....Ingawa sikuwa na Uelewa Mpana,Baada ya kufwatilia nilikuja kupata Ufumbuzi kwamba Hakuna Future Tme wala Future Tense...Wewe Binafsi Ndio Future Tense na Future Tense....Fikiria kama wewe ukiwa Haupo Je kuna kuwa na future Tense au Future Time??

Dunia ya Kwanza yaani Naamanisha Nchi zilizoendelea Muda kwao ni Muhimu wanafanya Kila liwezekanalo kuweza kuokoa Muda ili kuweza kufikia malengo wanayojiwekea,Kuanzia kwenye usafiri na Utendaji wao wa shughuli za kila siku.Kuna wakati unajiuliza Kama unakaa kwenye Foleni ya Gari Masaa Matatu na Unapokwenda Ukitumia Mguu hayazidi hata Masaa Mawili kwanini usichague kutembea???Kizazi chetu kina Excuse nyingi....Utasikia Jua kali,Je wazazi wetu hawakuliona Jua?Au Sisi Ndio Ngozi Zetu zina ukakasi kuliko wao?Swali la kujiuliza??Maisha yetu hapa duniani yamefungwa kwenye Muda,yaani Unapochezea Muda ndio Unachezea maisha yako Pia.


Unapochezea Muda Unachezea Maisha yako pia,Ni ngumu kumshauri mtu aliyezoea kuishi kwenye maisha yasiyozingatia Muda,Ukimwambia Utasikia "No Hurry In Africa".Mtu huyu akikwama juu ya jambo fulani ukimwambia jambo hili ulipaswa ufanye miaka mitano iliyopita ananza kutoa macho,Sasa unabaki unajiuliza huyu vipi,Tangu tunakuwa kuna watu hawaendi mbele wala hawarudi Nyuma yaani wapo wapo,Ukimwambia na Ukimshauri Utasikia Sisi Tumeliona Jua Kabla yako.Kumbuka Kila unachofanya Hapa duniani kina mwisho wake kama kilikuwa kina mwanzo basi mwisho Upo.

Unapochezea Muda Pia na Hata Resources nazo Zinapotea.Fikiria Mfano wewe ndio Mchezaji Mpira,Mwili wako ndio Resources moja wapo ya kutumia ili kukuwezesha kufikia malengo fulani kwenye maisha yako.Kumbuka kadri unavyokuwa mtu mzima Resources hiyo inazeeka na mwishowe kuchakaa na kutokuweza kutumika tena na kama itatumika sio katika kiwango husika kwenye maisha yako.Fikiria wewe ni mwimbaji Sauti yako ndio resources yako ,Je unafikiri Unavyoweza kuimba leo na Ndani ya Miaka 30 ijayo utaweza kuimba hivyo hivyooo???Anayekupotezea Muda,Anakipotezea Malengo.

Mwisho wa Siku Nashaangaa yaani mtu kazunguka huko katafuta cha kufanya kakosa anakuja kwako anakuambia twende mahali fulani,Ukifika Kule mahali utasikia twende mahali kwingine,Mwisho siku unamaliza siku nzima umechoka una umetumia muda wako kuzurura barabarani bila kufanya kitu cha maana unapoona kuna vitu vunaweza poteza muda wako kataa kuvilea,Badilisha mfumo wa maisha.Kumbuka hakuna wakati ujao,Wakati Ujao ni sasa na Wakati Ujao ni Wewe.Usifikirie ya Kesho wakati ya Leo Haujayamaliza.

Maisha Yetu Yamefungwa katika Muda,Baada ya Muda fulani unapaswa uwe umefanya jambo fulani,Ndio maana kwa sisi mabachela mtu akifika hadi Miaka 40 hajaoa watu wanajiuliza kwanini hajaoa,Tatizo sio Kuoa tatizo ni muda wa kuoa.Zingatia Muda wako kwenye Kila jambo Maana Muda ni Wewe na Wewe ni Muda.

...Punch Of The Week..............Anayepoteza Muda,Anapoteza Malengo

Mara nyingine katika Punch Of The Week Tunaendelea kuangalia Mada Mtambuko na Zinazotuzunguka kwenye maisha yetu ya Kila Siku....Naam...Leo Tunaangalia Mada inayosema Watu Hawasemi Lakini Wanaambiana.

Mara Nyingi kwenye maisha yetu ya kila siku tumeona watu wanakuwa wanatunyamazia kwa nama moja au nyingine kuhusu swala/jambo fulani linalokuhusu wewe binafsi ili hali wewe ukifikiri wako kimiya,ukweli ni kwamba watu hawasemi tu lakini wanaambiana kuhusu wewe na kila jambo unalolifanya kwenye maisha yako ya kila siku.Mara nyingi kuna mambo mengi yanaweza kuwa yanajadiliwa kuhusu wewe lakini hauwezi jua maana hakuna anayekumbia.Tambua kila unachofanya kwenye maisha yako ya kila siku watu wanaambiana hata kama kiwe kizuri au kibaya unachofanya,kiwe cha kupendeza au cha kuchukiza lakini wataambiana tu.

Mara chache sana watu wanakaa kuzungumza habari za mafanikio ya mtu namna mtu anavyopiga hatua kwenye maisha yake kwenye nyanja mbali mbali na kuweza kufanikiwa kuanzia kwenye Imani,Kiuchumi,Kisiasa na hata kijamii pia.Watu wengi wanapokaa pamoja mara nyingi huongea mambo ambayo sa nyingine yanaweza yasikufurahishe ukiyasikia lakini ndivyo watu walivyo.Ni ngumu kuyasikia maana hawakwambia.Tambua kila jambo unalolifanya kwenye maisha yako ya kila siku unaweza ona watu wamekufungia mdomo na kama hawako na wewe lakini jua ni moto wa kuotea mbali.Hakikisha kila hatua na jambo unalolifanya hakikisha unalifanya kwa usahihi na umakini mkubwa hata iwapo watu hawakuoni.Wanaweza kujifanya hawakoni lakini kiukweli wanakutazama tu wanagojea wakutane na watu wengine ambao wako kama wao na waanze kuzungumza bila ya wewe kujua.

Mara nyingi Habari Mbaya za Mtu husambaa mapema zaidi kuliko nzuri.Mwana saikolojia mmoja alisema Binadamu kwa Asili ni Wachoyo na Walafi yaani hawapendi kuona mwingine anafanikiwa kwenye jambo fulani kwenye maisha yake.Yuko tayari kuharibu kwa kusema mabaya yako hata kama hayana ukweli ili mradi akuharibie maisha yako.Ki-Ukweli wewe unawez ukawa unatembea njia na kuona hamna shida na unacheka na wengine lakini Watu hawasemi Tu ila wanazungumza kwa muda wao wanaoujua zaidi.Je umeshawahi kujiuliza,je kama ungepewa nafasi ya kusikiza maongeze ya watu kwenye simu pale TCRA ya 
kil siku unahisi ukijisikiaje??Watu hawasemi Lakini Wanaambiana.Makosa ya mtu huonekana zaidi kuliko uzuri wa mtu,Waswahili wanasema Baya moja Hufuta Wema 1000 ulioutenda.Ni rahisi kusemwa ubaya wako kuliko uzuri wako Maana kwa asili binadamu ni Wabaya kama Alivyosema mwanasaikolojia.

Mwisho Napenda Kusema imekupasa kuwa makini namna unavyojiwakilisha mbele ya watu,awe mtu wako wakaribu unayemwamini au usiyemwamini ni muhimu kuchukua tahadhari mapema.Fanya maswala yako kwa uminifu ili hali kama ungetamani wengine wakufanyie hata iwapo watu hawakuoni.Make Sure haufanyi vitu kwa ujinga,fanya kwa umakini huenda wanajifanya hawakuoni lakini wanakuona.Fanya kwa kiwango cha Juu lakini pale ambapo unaona umefika mwisho acha,Jitahidi kuweka juhudi kwenye kila jambo unalolifanya na kwa umakini mkubwa sana.Watu hawasemi lakini Wanaambiaana...


..................Watu Hawasemi Lakini Wanaambiana.............................
Miaka michache iliyopita nilikutana na msemo huu( "If you want to hide something from a Black Man Put it in a Book"). ambao ulinitia hasira kidogo na kunifanya nijiulize mara mbili mbili kwanini.Msemo huu miaka ya nyuma ulitumika nchi Marekani ambao ulikuwa una lengo la kuwabagua watu weusi kupata haki ya msingi ya kujifunza maana walikatazwa kusoma na kujifunza vitu kadha wa kadha.Lakini Baadaye baada ya kufwatilia kidogo nilikuja kugundua tatizo lilikuwa halipo kwa waliotunga aina hii ya taratibu bali lilikuwa kwa waliowekewa utaratibu huu.Watu weusi walikuwa ni watu wasiopenda kujifunza na kusoma baada yake waliamua kutumia muda mwingi kufanya vitu visivyo na tija kwa muda mrefu ambavyo vilitumia nguvu zaidi kuliko akili zaidi.

Mfano Michezo kama Basket na Rugby na michezo kadha wa kadha.Waafrika hawa walibuni michezo mingi kadha wakadha ili kujiletea burudani na maisha yao kuendelea lakini walishindwa kushika nyazifa muhimu na kupata maendeleo yaliyobora.Watu weusi wachache waliopata kupenda kusoma walipewa nafasi kubwa na hata uwezo wao wa kusoma na kuendesha vitu ulikuwa tofauti na wengine.

Tukirejea hapa Afrika kwetu na Haswa Nchi yetu ya Tanzania kwa miaka mingi Kutafuta maarifa na elimu ambayo yatakufanya uendelea kudumu zaidi kwenye changamoto za maisha imekuwa ngumu.Tumekuwa tukilalamika kuhusu swala la maendeleo lakini Upande wa pili je tuna uwezo wa ziada ambao unaweza kutufanya tuendelee kwa haraka.Baada ya kufwatilia kwa kiasi kikubwa nimekuja kugundua wasomaji wa vitu ni wachache na wafwatiliaji wa vitu niwachache.Ukitaka kujua uwezo wa mtu na anavyojua vitu angalia hata namna ambavyoa anaendesha maisha yake na anavyofikiria na kuchambua vitu.Katika pita pita zangu za kusoma vitu nilikuna na huu msemo usemaao.."
“Insanity is doing the same thing, over and over again, but expecting different results" by Albert Einstein.


1.Maarifa ni jambo linalodumu ndani ya Mtu Binafsi.

Unapoweza kujiongezea maarifa kwa kusoma na kujiendeleza katika aina tofauti tofauti ya ujuzi kichwani mwako wewe ndio utafaidika kwa sehemu kubwa kwa maisha yako daima.Mtu anaweza akakupokonya cheti au kikapotea lakini Maarifa ya mtu hayawezi kupokonywa wala kupotea maana ni jambo lililoko ndani ya mtu daima na swala ambalo linadumu mpaka siku za mwisho za uhai wake hapa ulimwenguni.Ubongo wa Binadamu ni mithili ya Viungo vingine tu vya mwili kadri vinavylozidi kutumimiwa ndivyo vinavyozidi kudumu daima na kuwa imara.Ubongo ni mfano wa Mguu wa Mcheza Mpira,Maana Mcheza Mpira asipofanya mazoezi kwa muda mrefu au kucheza uwanjani kipaji huanza kupotea taratibu na mwishowe hufa kadhalika ubongo wa mwanadamu ndivyo ulivyo unavyotumika zaidi ndivyo unavyofanya kazi katika hali ya ubora na utadumu kwa muda mrefu zaidi.

2.Kila maarifa yaliyopo kichwani yanathamani yake.

Kila siku tumekuwa tukienda kuomba kazi na kufanya usahili kwenye maofisi ya watu mbali mbali ili mradi tupate ajira.Unapokweenda kwenye usahili mara nyingi hauingi na hata karatasi lengo kubwa linakuwa ni kujua una uwezo na una maarifa kiasi gani kuhusu ulichokisoma na unaweza kuleta tija kwenye kampuni husika?Baada ya kufanya usahili wanaweza kukuajiri na kukupangia kiasi fulani cha malipo ambacho ndicho kinakuwa sawasawa na thamani ya Maarifa yako.Ndio maana kuna viwango vya Mishahara kazini.Ofisi Nyingi mtu anapoenda kusoma akirudi Mshahara huongezeka,Ni kwa sababu ameongez kiwango cha maarifa kichwani mwake.Unapongeza Maarifa mbali mbali kichwani mwako ne ya maisha ya kawaida ya watu wengine ndivyo Thamani yako Hupanda kwa maana nyingine...Mshahara unaolipwa na Maarifa yako vinatosha na vinaenda Kabisa.


3.Maarifa ni Jambo linalorithishwa kutoka kizazi hadi Kizazi kama ulivyo Ujinga.

Familia nyingi zilizo bora kwenye maisha yetu ya kila siku ni familia ambazo ziliwekeza kwenye maarifa siku za nyuma kwenye maisha yao ya kila siku.Mara nyingi tumepika kelele kuhusu swala ma maendeleo na vitu mbali mbali lakini tunashindwa kujiuliza je watu walitumia muda gani kuwekeza katika maarifa.Kun msemo wa wahenga wansema alivyo Baba na Mama ndivyo Watoto walivyo.Tumendelea kupiga kelele kwamba Tanzania kuna anguko la Elimu(Maarifa) maana yake tumejua kuna athari zake katika vizazi vijavyo.Unapokuwa na maarifa zaidi ni rahisi kuwasaidia hata watoto wako kwenye njia iliyobora.Usiwalaumu watoto wa kizazi hiki Bila kujua uwezo wa wazazi wao katika kuwekeza katika swala zima la maarifa.Je wanatumia muda gani na wanawekeza kiasi gani.Na rudi pale pale .Maarifa ni jambo la Urithi kwa Watoto kama ulivyo Ujinga.Kama hautaki watoto wako wawe wajinga siku zote wekeza kwenye maarifa nao watafaidi katika maisha yao yajayo hata usipokuwepo.



.....Maarifa Huuwisha Nafsi Daima Bali Ujinga Hushakaza Mwili......Unapokuwa na maarifa zaidi ndivyo unavyostawi zaidi kuanzia kwenye nafsi na daima lakini Unapokosa maarifa unakuwa Mtumwa wa wengine ambao wanakuwa na maarifa ziadi yako.
Maisha yetu ya kila siku ni mithili ya mapambano kuelekea jambo fulani kwenye kufikia hatma za maisha yetu.Kila siku tunafanya vitu mbali mbali kuweza kufikia hatma iliyo bora ya maisha yetu.Hakuna mtu anayependa kuwa na hatma mbaya kwenye maisha.Iwapo utafanikiwa hata kukaa na mlevi wa matapu tapu karibu akiwa amelewa chakari ukimuuuliza unataka kwenda jehanamu atakwambia hapana nataka kwenda mbinguni pamoja na ulevi alio nao.Wazuoni wachache siku za nyuma walisema Maisha ni Mapambano,Sehemu yeyote inayokuwa na mapambano maana yake ni vita baani ya pande mbili zinazotofautiana kimaslahi.Mmoja anaona anaonewa na mwingine anaona yuko sawa.

Ni hatari kuingia kwenye mapambano fulani bila kujua adui yako yukoje kwenye uwanja wa vita na pia ni hatari kutokulijua eneo la kupigani vita lakini pia silaha za kupigania vita na jeshi la aina gani linaweza kupigana vita.Unapokosa kujua vyote hivi ni rahisi kupoteza aina yeyote ya vita kwenye maisha yako.


Mara nyingi tumeingia kwenye mapambano bila kujua adui tunayepambana nao kwa wakati huo kwenye maisha yetu na kutupelekea sisi wenyewe kupapasa pasa kwenye kila jambo ambalo tunalifanya.Ni rahisi kwa mlokole kukemea pepo la umaskini na kuendelea kuomba bila kuchukua hatua fulani kwenye maisha.

Umaskini hautoki kwa maombi bali kwa kufanya kazi kwa bidii na bila kukataa tamaa na kufwata kanuni halali za kiutendaji.Ujinga ni tatizo kubwa kwenye jamii yetu juu ya adui ambaye tunafikiri tunapambana naye.Ni rahisi kupambana na CCM tukiwaona kama ni shida kumbe tatizo sio wao ni msingi mibovu ilojengwa tangu mwanzo wa uongozi na fikra zao.


Tunaweza kujua adui ambaye tunapambana naye kwenye maisha yetu ya kila siku ili kuweza kufikia hatma bora ya maisha ya kila siku lakini tatizo linakuja namna ya kujua eneo la mapambano,je ni jangwani au msituni au kwenye maji..??je kama ni jangwani je ramani ya jangwa hilo ikoje na kama ni msitu je msitu huo ukoje??

Ni muhimu kujua eneo ambalo utalitumia kama eneo la mapambano  ya vita vyako vya kila siku.Ni rahisi kwa mwanafunzi mpya wa chuo kujua course anayoifikiria kuisoma chuo lakini kipi ni chuo bora na chenye walimu bora juu ya course anayotaka kusoma.Unapokosa kujua battle ground yako ni bora usianzishe vita maana kuna uwezekano wa adui yako kukushinda maana eneo na uwanja wa vita ana ufahamu wa kutosha.


Silaha za kupia vita vyovyote inategemea na adui unayepigana naye na eneo ambalo mnalotumia kupigana vita.Ni ngumu kurusha makombora ya masafaa marefu zaidi ya kilomita 1500 kwa saa na huku ukiwa unapigana vita na Kisiwa cha Mafia.

Adui yako ndio anayekupa lead ya kwamba ni aina gani ya silaha utumie kupigana naye.Miaka ya mwanzo mwa 1990 tuliambiwa mtu akienda chuoni anapewa pesa lakini kutokana na wrong info basi tulijua mtu anapofika chuoni ni maisha ya burudani na raha lakini kumbe ni kinyume chale unapaswa kuweka jitihada zaidi.Kama ulikuwa ukikesha kusoma mara mbili kwa mwaka ulipokuwa Sekondari unapofika chuo kulala usiku wa manane ni jambo la kawaida tu lisilo na mjadala.Mara ya kwanza watu wengi hupata shida sababu hawakuelewa adai aliyeko mbele yao.


Kuna aina tofauti tofauti za department za jeshi linapofika swala la mapambano kwenye vita haiwezekani vita ikawa inapiganwa kwenye Eneo la Bahari wewe ukapeleka jeshi za miguu au vita ikapigana kwenye msitu wewe ukapelekea jeshi la maji.Kila sehemu inachagua aina gani ya jeshi unaloweza kulitumia kwenye mapambano ya vita vyako as long as umeshajua adui,eneo,silaha na pia unaweza kujua aina ya jeshi unaloweza kutumia kwenye uwanja wa mapambano.

Kwenye Jeshi kuna aina mbali mbali za wataalamu ni lazima ujue kama unaweza kutumia expert wachache tu na ukamaliza vita kwa upesi au unaweza ukatumia aina gani ya wataalamu kufikia hatma yako kwenye maisha.Maisha ni mapambano hakuna anayefikiri kushindwa lakini tangu mwanzo wa vita yeyote ni rahisi kujua yupi ni mshindi na yupi ni mshindwa.


.....Kupigana Vita usiyoijua nia Kucheza Kamali Karibu na Kituo cha Polisi.......
Hakuna kitu kilicho kirahisi kwenye maisha ya mwanadamu,Vyote vinahitaji nguvu ya ziada kuweza kufika malengo na kilele cha mafanikio binafsi.Unaweza kuona kitu kwa mtu kinaenda tu kwa njia nyepesi lakini hauwezi jua ameanzi wapi.Ukionacho leo ni Rahisi Kuna siku Kilishawahi kuwa Kigumu.

Kufikia malengo ya kimafanikio kwenye maisha kunahitaji nguvu,uwezo kujitoa na hata kuachana na vitu vingine ili kuweza kufikia maisha ya kimafanikio.
Wakati tunaanza darasa la Kwanza miaka ya nyuma tuliingia tukiwa hatujui kusoma wala kuandika kabisa lakini baada ya kujitoa na kufanya kwa bidii leo hii ukishika kitabu tuu unajua namna ya kusoma na kuandika.


1.Ni Rahisi Kuona Mafanikio Ya Mwingine na Ukayafurahia.

Hakuna jambo lilorahisi kufurahi kama kufurahia mafanikio ya mwingine bila kuja wapi alianzia na maamuzi gani alioyachukua.Sisi tunapoona matokeo ni rahisi kufurahia matokeo bila kutaka kujua mwanzo wa jambo ulikuwaje.
Miaka Michache iliyopita watu tulikuwa hatujui Precision Air lakini wanaojua historia ya Mzee Michael Shirima(Mwenyekiti wa Precision Air) wanaweza kuelewa nini Maana ya Kufilisika na Kurudi Kijijini na Kulima Kahawa na Ndipo Mtu anapata mwanga mpya wa kuanza kujaribu tena kuanza na wazo la kuwa mmiliki wa Kampuni ya Precision Air.
Leo hii sisi tunafurahia matokeo yake kwa kupanda ndege lakini kumbe kuna mtu alifilisika na akarudi kijijini na kuanza tena.Kufikia mafanikio inabidi uyashinde mazoea binafsi maishani mwako

2.Ni Rahisi Kukosoa Mafikio ya Mtu kuliko Kuanza ya Kwako.

Moja ya kipaji ambacho tunacho watu tulio wengi ni cha Kukosoa,Mtu anapoona mwenzake anapiga hatua baada ya kumsaidia kuboresha hatua zake kuweza kufikia mafanikio yake tunaanza kukisoa angefanya hiki au kile alafu unakaa pembeni ukisubiri aanguke uanze kusema nilitabiri mithili ya Nabii fulani.

Hakuna kitu kiachoaanza kikiwa chepesi.Kila ukionacho leo ni Rahisi  Kuna Siku Kilishawahi Kuwa Kigumu .
Hakuna urahisi kwenye jambo lolote wahenga walisema Siku zote Mwanzo ni Mgumu na Njia iendayo uzimani ni Nyembamba na Imesonga.
Ni rahisi sana kuanza kusema vibaya mafanikio ya mwingine kuliko kuweza kuanza ya kwako na ikafikia kipindi ukajivunia.
Mtu shujaa na mwenye mafanikio ya kweli ni yule anayechukua changamoto anazokutana nazo na kuweza kuzitumia kujijenga na kusonga mbele.Kama haukuwahi kukosea juu jambo lolote base tambua haukuwahi kujaribu kufanya kitu siku zote maishani mwako.

 Hakuna Mwanzo ulikokuwa rahisi kwenye kila jambo unapotaka kulianzisha ndio maana ukitaka kufikia mafaniko yako binafsi haupaswi kuishi na makosa ya jana leo na haupaswi kuishi na matarajio ya kesho leo bali unapaswa kuitumia vizuri kila dakika na sekunde unayoweza kuipata leo.
Kumbuka jana ni historia lakini Kesho ni Muujiza.Fanya jambo ambalo litakuwezasha kufikia malengo fulani ukitegemea urahisi wa jambo tambua upotevu uko karibu kuliko unavyodhani.
Laini Laini Maana yake si rahisi.Mwanzo ni Mgumu.Mwanzo wa Neno ni Mgumu kuliko Mwisho wake.

"Kila ukionacho leo ni Rahisi  Kuna Siku Kilishawahi Kuwa Kigumu"
Jengo la Ghorofa 15 katikati ya jiji la Dar es Salaam mtaa wa Indra Gadhi limeanguka leo asubuhi  pamoja na Watu wapatao 60 ndani yake mkiwemo watoto wa Madrassa katika jengo hilo. 
Mpaka sasa maiti zilizoopolewa ni 14 na majeruhi zaidi ya 30 wamekimbizwa hospitali.

Pata Habari kwa Picha

Wakati Jengo linaanguka

Muonekano wake Baada ya Jengo Kuanguka

Hili Ndilo Eneo la Tukio

Kazi Uokozi Ikieendelea kwenye Eneo la Tukio
Siku ya Tarehe 23/2/2013 kwenye Ukumbi wa Kanisa la Victory Christian Center Tabernacle (VCCT) kulikuwa na sherehe ya Huduma ya Soul Breakfast Kutimiza Miaka Miwili Tangu ilipoanzishwa Machi,2011.
Huduma Hii ni Maalumu kwa Wanafunzi wa Viwango tofauti tofauti vya Elimu Kuanzia Sekondari Mpaka Elimu za juu hapa nchini Kwetu Tanzania.
Huduma Hii ilianza na wanafunzi wachache sanaa mwaka 2011 lakini mpaka sasa kuna takribani wanafunzi 200 ambao wana hudhuria kwenye huduma hii.Lengo La Huduma Hii ni Kuwawezesha Wanafunzi kupata ujuzi wa kawaida wa maisha ya mtaani baada ya kutoka shule lakini pia na namna ya kutumia fursa zote zinazopatikana wakati wakiwa kwenye maeneo yao ya Elimu wanaposomea.


Ibada ya Sherehe ikianza

Inter -  Collage  Praise and Worship Team ikiwa Jukwaani

Soul Breakfast Team Maurice Okao(Mwenyekiti wa Soul Breakfast) na Director wa Campus Ministry  Samuel Sasali

Praise and Worship Team ikienda Sawa

Pastor Dr Huruma Nkone alikuwepo siku hiyo

Write The Word Coconut kwa Kutumia Mwili Wako

Director wa Campus Ministry Samuel Sasali Akielezea Maana ya Soul Breakfast  

Rivers of Joy International(Junior) Wakienda Sawa

Praise and Worship Imenoga

Cheza muziki wa Yesu

Twende Sawa

Wadau wakienda Sawa na Muziki wa Yesu
Prezzor Chavala akifanya Vitu vyake kwenye Jukwaa

Pastor Dr Huruma Nkone akinena na Watu waliofika Siku Hiyo

Paul Clement kutoka Glorious Team akifanya vitu vyake kwenye Jukwaa

Hawa ndio Presenters na Watu walifanya kazi na Soul Breakfast mwaka 2012-2013 wakiwa wameshika Vyeti Vyao baada ya Kutunukiwa kwa Utayari wao 
Soul BreakFast Committee  wakiwa na Presenter na Wadau Wengine wakipata pich a ya Pamoja na Pastor Dr Huruma Nkone

Maurice Okao Mwenyekiti wa Soul Breakfast Committee akieleza jambo

Mc wa Soul Breakfast Siku hiyo akienda Sawa

Wadau wakisikiliza jambo kwa Umakini Mkubwa Sana

Mwendo wa Celebration tu hapa

MC akienda Sawa

Vuvuzela Zilikuwa Sehemu ya Sherehe ya Soul Breakfast



Huyu ndie Mc Pilipili Mtoto wa Mama Roda

Kikazi Zaidi Mc Pilipili ya Shughuli


Mwendo wa Kazi tu Hapa

Enzi za Primary hizo 

Paul Clement pamoja na Team yake Wakimaliza Shughuli