CITY CENTRE CHURCH T.A.G (UPANGA)
7:00 A.m. / 10:00Am.
Andrew Palau will Preach at both Sunday Service
7 August ,2012
PRESS CONFERENCE
10:00a.m.
Location TBD. All Media Houses will be invited.
Bishops, Local Artists, Andrew Palau and BMX team will address the media.
6 - 10 August ,2012
READING EYE GLASS CLINICS
10:00a.m-4:00p.m.
St. Nicholas’ Anglican Church (Ilala)
Tanzania Assemblies of God (TAG) (Mbagala)
The Lutheran Church (Vingunguti)
Baptist Mission Church (Magomeni)
*10,000 Pairs of Reading Glasses will be available at these 4 locations for free. US and Tanzanian Eye Doctors are partnering together under Love Tanzania to bring a tremendous gift in these 4 communities. Come Early to see the Doctor and receive a free pair of reading glasses
6 - 10 August ,2012
SOCCER + BASKETBALL CLINICS
9:00-11:30a.m / 1:30-4:30p.m.
Play for Hope
15 Professional Soccer / Basketball coaches from Rwanda will host clinics for thousands of kids in Ilala, Temeke and Kinondoni.
SCHOOL PRESENTATIONS
Duggie Dug Dug and a team of Volunteers will do presentations in 8 primary Schools.
Vic Murphy, John Andrus (BMX ACTION SPORTS Team) will do Demos in 5 Primary Schools and then will team up with the Play for Hope Afternoon Main site. The Action Sports team will be joined by international evangelist Mike Parker and a team of volunteers.
WOMEN’S DINNER
5:00 p.m. Karimjee Hall
Matron of Honor, Evelyne Warioba, and the LTF Women’s Committee are inviting 600 Women to an elegant dinner to hear Wendy and Andrew Palau share their story.
8 August ,2012
BUSINESS AND CIVIC LEADERS DINNER
6:00 p.m. Karimjee Hall
600 Government, Corporate CEOs, Dar es Salaam leaders will be invited to another special Dinner moment with Andrew Palau.
*NOTE: Events at Karimjee are not open to public to attend. These two dinners are invitation only events. If you as Media desire to attend to cover the story please contact Lillian to indicate an interest to attend.
10 August ,2012
FMX (MOTOR CROSS) PRACTICE
2:00-3:00 p.m. Jangwani Ground
JUNGLE RUSH FMX from Joberg will be onsite getting ready for Love Tanzania Festival. Cameras are encouraged and live shots are available for Evening News Stories.
DEDICATION PROGRAM
3:00-6:00 p.m. Jangwani Grounds
All Volunteer Workers will be asked to attend this dedication time. Potentially 2,000-3,000 workers will attend.
Saturday – Sunday 11-12 August
LOVE TANZANIA FESTIVAL WITH ANDREW PALAU
1:00 – 3:00p.m
CHILDRENS PROGRAM
Games, Jumper Castles, Soccer Clinics and DUGGIE DUG DUG
3:00-4:00p.m.
ACTION SPORTS DEMOS
FMX/ BMX presentation
4:00-8:00p.m.
MAIN STAGE
THE VOICE
CHRISTINA SHUSHO
JOHN LISU/ SAFARI PAUL
National Worship Leaders
MASANJA – Faith Story
International GOSPEL MUSIC artists
DON MOEN
NICOLE C. MULLEN
DAVE LUBBEN
![]() |
Muimbaji mashuhuri Nicole C Mullen atahudumu |
![]() |
Donnie Moen kuhudumu |
Thanks to Hossana Inc and Christian Bloggers in Tanzania
KITABU kinachozungumzia kashfa ya kihistoria ya ununuzi wa rada, uliowahusisha aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Andrew Chenge na aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT) Dk. Idriss Rashidi, tayari kimeingia nchini.
Ndani ya kitabu hicho, kilichokuwa kikusubiriwa na wengi kiingie nchini, kinachoitwa The Shadow World Inside The Global Armrs Trade, Mtunzi Andrew Feinstein ameeleza kwa kina mchakato ulivyoendeshwa, ukiwahusisha watu wa madaraka na kada mbalimbali ambao ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair.
Andrew Feinstein
Tony Blair anatajwa katika kitabu hicho kuwa ndiye aliyemshawishi aliyekuwa Rais wa Tanzania wakati huo, Benjamin Mkapa, kununua rada hiyo kutoka kampuni ya kutengeneza silaha ya Uingereza BAE-Systems.
Sailesh (Shailesh) Vithlani
Pamoja na hao, wanatajwa wafanyabiashara wenye asili ya India, lakini ambao wanaishi/walipata kuishi Tanzania, Tanil Somaiya ambaye alikuwa akimiliki kampuni ya uwakala wa simu ya Shivacom na Sailesh (Shailesh) Vithlani, kuwa watu wa kati wa biashara hiyo.Kuibuka kwa kitabu hicho kunaongezea tu katika taarifa za awali zilizopata kuchapishwa na kutangazwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini kuhusu ununuzi wa rada hiyo ambao ulipingwa sana si tu ndani ya Tanzania, bali hata Benki ya Dunia na Uingereza kwenyewe.
Wakati huo aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa, Clare Short, alikataa katakata Tanzania, moja kati ya nchi masikini kabisa duniani, kutumia mabilioni ya fedha kununua rada katikati ya umasikini unaonuka.
Anasema mwandishi wa kitabu hicho katika sehemu moja ya maandishi yake: “Wakati akipigia chapuo, Tume yake ya Afrika (Commission for Africa) juu malengo ya kuwa na utawala bora katika Afrika, Tony Blair alimshawishi Rais wa Tanzania, moja ya nchi masikini kabisa duniani kununua rada ya kijeshi kwa bei ya zaidi ya dola za Marekani milioni 40.
Wakati huo Tanzania ilikuwa na ndege nane tu za kivita, nyingi zikiwa katika hali mbovu kiasi cha kuzifanya zisitengenezeke. Rushwa ya karibu dola za Marekani milioni 10 inadaiwa ililipwa kwenye mpango huo.”
Kwa mujibu Andrew Feinstein, akiba ya dhahabu iliyohifadhiwa katika BoT ambayo, hata hivyo, thamani yake halisi haijafahamika, ndiyo iliyotumika kufadhili upatikanaji wa mabilioni ya fedha kwa njia ya mkopo kutoka Benki ya Barclays, ili kufanikisha ununuzi wenye utata wa rada ya kijeshi.
Katika taratibu za benki kuu mbalimbali duniani, dhahabu imekuwa ikihifadhiwa kama moja ya njia za nchi husika kujimudu dhidi ya mitikisiko ya kiuchumi. Tanzania ni kati ya nchi inayotumia mfumo huo wa kuhifadhi dhahabu.
Mwandishi huyo anasema katika kitabu hicho kwamba Dk. Idriss ndiye aliyekuwa kiungo muhimu katika kufanikisha mkopo kutoka Benki ya Barclays kwa masharti kuwa dhamana iwe akiba ya dhahabu iliyoko katika Benki Kuu ya Tanzania.
Bila kutaja thamani halisi ya akiba hiyo lakini akitaja kiwango cha mkopo husika, Andrew Feinstein anasema: “Katika mchakato huo, Dk. Idriss ndiye aliyekuwa na jukumu la kuidhinisha malipo hayo ya ununuzi wa rada (akiwa Gavana wa Benki Kuu), kwa masharti kwamba Benki ya Tanzania iweke dhamana akiba yake ya dhahabu ili mkopo (wa ununuzi rada) upatikane.
Feinstein anaeleza pia kwamba bosi huyo wa BoT ndiye aliyehakikisha michakato yote ya kifedha (malipo) inafanyika kwa mujibu wa sheria za Uingereza (zenye kinga katika michezo ya utoaji ‘chochote’ katika masuala ya ununuzi) na si sheria za Tanzania.
Mwandishi anasema Chenge, ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Fedha na Uchumi, anatajwa kuhusika kutoa ushauri wa kisheria (kwa wakati huo akiwa Mwanasheria Mkuu), ushauri ambao unatajwa kuzingatiwa katika hatua nyingine za uamuzi, ukiwamo uamuzi wa Benki ya Barclays kutoa mkopo wa ununuzi wa rada.
Inadaiwa kuwa ili kuhakikisha mkopo kwa ajili ya ununuzi wa rada unapatikana kutoka Benki ya Barclays, wakala wa ununuzi huo Sailesh Vithlani, aliwasilisha nakala ya maoni ya Mwanasheria Mkuu wa Tanzania (Chenge) katika Benki hiyo.
Andrew Chenge
“Malipo yaliyofanywa kwenye akaunti ya Chenge yanalingana kikamilifu na uwasilishaji wa maoni yake (ya kisheria) kwa ajili ya kufanikisha upatikanaji wa mkopo na ununuzi wa rada.”
Kwa mujibu wa kitabu hicho, mazingira hayo ya ushiriki wa Chenge kwa njia ya kutoa ushauri wa kisheria yanathibitishwa na mawakili wake wa kimataifa, walioko Marekani pamoja na Uingereza ambao baada ya kuhojiwa walikiri ushiriki huo wa Chenge.
Namna walivyochota mamilioni
Inaelezwa kuwa kwa mujibu wa rasimu ya ripoti ya SFO (Taasisi ya Uchunguzi Makosa ya Jinai ya Uingereza), Chenge alipokea malipo ya jumla ya dola za Marekani milioni 1.5 (zaidi ya bilioni 1.5) kati ya Juni 1997 na Aprili 1998 kutoka Benki ya Barclays, tawi la Frankfurt.
Fedha hizo zililipwa katika benki ya Barclays huko Jersey - Uingereza, katika akaunti inayomilikiwa na kampuni iliyotajwa kwa jina la Franton Investment Limited. Kampuni hiyo imetajwa kumilikiwa na Chenge, ikiwa ni maalumu kwa ajili ya uhamishaji fedha kiasi cha dola za Marekani 600,000 (zaidi ya Sh milioni 600).
Maelezo zaidi katika kitabu hicho yanabainisha kuwa, dola hizo 600,000 za Marekani zilihamishwa kutoka kwenye akaunti ya kampuni ya Chenge kwenda kwenye akaunti nyingine, inayomilikiwa na Kampuni ya Langley Investments Ltd, iliyokuwa ikiendeshwa na Dk. Idrissa Rashidi (aliyewahi pia kuwa Mkurugenzi wa TANESCO).
Katika kitabu hicho, Feinstein ambaye aliwahoji washiriki mbalimbali wa sakata hilo, wakiwamo baadhi ya maofisa wa upelelezi nchini anasema: “Septemba 20, mwaka 1999, Chenge binafsi aliidhinisha uhamishaji wa dola za Marekani milioni 1.2 (zaidi ya Sh bilioni 1.2) kutoka akaunti ya kampuni (yake) ya Franton kwenda Royal Bank of Scotland International, huko Jersey.
Namna BAE ilivyojipenyeza
Mwaka 1997, kampuni ya BAE ilinunua kampuni iliyojulikana kama Siemens Plessey Systems (SPS) ambayo ilikuwa katika mchakato wa mapatano ya kibiashara na Serikali ya Tanzania tangu mwaka 1992 kwa ajili ya mauzo ya rada.
Kama sehemu ya makubaliano katika kuinunua kampuni ya Siemens Plessey Systems (SPS), BAE ilikubali kuendelea kumtumia wakala wa SPS, Sailesh (au Shailesh) Vithlani. Katika mazingira hayo, Sailesh aliomba kufanyike marekebisho kuhusu ahadi zake kwa maofisa wa Serikali ya Tanzania.
Hali hiyo inatokana na ukweli kwamba, ‘dili’ la mwanzo ambalo lingefanikisha biashara ya pauni za Uingereza milioni 110 lilizuiwa na Benki ya Dunia pamoja na Chombo mahsusi cha Uingereza cha kusimamia masuala ya maendeleo (Uk’s overseas Development Administration).
Uingiliaji wa Waziri Clare Short
Mwaka 2000, dili ikaibuka upya na safari hii kampuni ya BAE ikiligawa mradi (dili) huo katika awamu mbili ili kuunfanya uonekane ni mradi nafuu, lakini Clare Short, aliyepata kuwa Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa alipinga mpango huo.
Upinzani huo ulihusisha hoja mbalimbali ambazo ni pamoja na mchakato mzima wa ununuzi umegubikwa na utata na kubwa zaidi, teknolojia ya rada hiyo imekwishapitwa na wakati. Hoja nyingine ni kwamba, Tanzania haina na shida na rada hiyo na badala yake, kilichokuwa kikihitajika ni rada ya ‘kiraia’ kwa ajili ya kuboresha huduma za anga na hasa kwa kuitazama sekta ya utalii.
Hata hivyo, licha ya upinzani wote huo kutoka kwa Waziri Clare Short na Waziri mwenzake wa Mambo ya Nje wa Uingereza kwa wakati huo, Robin Cook, mpango wa ununuzi wa rada uliendelea mwaka 2001 kwa BAE System kuiuzia Tanzania rada kwa thamani ya pauni za Uingereza milioni 28.
Katika hali ya kupinga mchakato wa ununuzi wa rada hiyo, Oktoba, mwaka 2001 ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya Usalama wa Anga (ICAO), ilieleza kasoro katika ununuzi wa rada hiyo ya kijeshi.
Ripoti hiyo inanukuliwa ikisema; “Rada inayonunuliwa ni kwa ajili ya shughuli za kijeshi na kwa hiyo, haitakuwa na msaada mkubwa kwa shughuli za anga kwa ajili ya ndege za kiraia. Mpango wa ununuzi wa rada hiyo si sahihi na ni wa gharama mno.”
Kutokana na ripoti hiyo, Kampuni ya BAE iliishushia lawama ICAO kwamba imetoa taarifa za uongo na hasa kwa upande wa gharama za uuzaji.
Lakini wakati BAE na ICAO wakiingia katika malumbano, Msemaji wa Benki ya Dunia alitoa tamko akisema; “Matumizi hayo ya fedha (ununuzi) hayako wazi, yana utata mkubwa.”
Tafsiri iliyotolewa ni kwamba, bajeti ya dola za Marekani milioni 40 kwa ajili ya ununuzi wa rada hiyo ni sawa na theluthi moja ya bajeti ya elimu nchini Tanzania na kwa hiyo, ni kiwango kikubwa cha fedha ambacho kinakinzana na vipaumbele vya kibajeti vya Tanzania, kama elimu na afya.
Wengi walipata kuzungumzia sakata hilo la ununuzi wa rada wa karibuni kabisa akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambaye alisema katika mkutano na waandishi wa habari kwamba angezungmzia suala hilo kwa kutaja wahusika wakati wa kuwasilisha bajeti ya wizara yake akijibu hoja za wabunge waliokuwa wanataka wahusika watajwe hadharani na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
Huko nyuma Chenge mwenyewe alipata kuzungumzia suala hilo, na hasa, kumiliki kwake kwa akaunti za fedha nyingi nje ya nchi yeye akiwa kama mtumishi wa umma.
Akiwajibu waandishi wa habari wakati wa safari yake moja ya kurejea nchini, Chenge alisema fedha hizo zilikuwa ni vijisenti tu, kauli ambayo iliwatibua wengi wa Watanzania ambao shilingi kwao ilikuwa imeota matairi.
Na katika hatua nyingine wakati huo, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Edward Hosea alipata, mara mbili, kunukuliwa akisema Chenge hakuwa na kesi ya kujibu katika kashfa hiyo ya rada.
Kitabu hiki kimetua nchini katikati ya taarifa za ufisadi mwingine uliofanywa na Watanzania, wakiwamo wastaafu wa vyeo vya juu wanaotajwa kuwa wamefutika fedha zinazokadiriwa kuwa mabilioni ya shilingi katika akaunti za nchini Uswisi zinazotokana na migao ya rushwa.
Thanks to Gazeti la Raia Mwema na Uchambuzi makini
Pori la Akiba la hifadhi ya Taifa lililogeuzwa msitu mateso, mauaji Joseph Zablon
WENGI wamezoea kuuita Msitu wa Pande, lakini eneo hilo ni Pori la Akiba, lililopo kilometa 25 kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam katika Barabara Kuu kuelekea mji wa Bagamoyo.
Pori hilo la Akiba linamilikiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, lilitangazwa kuwa la akiba mwaka 1952.
Ili kufika Msitu wa Pande kutokea katikati ya mji, utalazimika kuteremkia kituo cha daladala cha Bunju ‘B’.
Kutoka hapo kuna daladala zisizo rasmi na pikipiki (bodaboda), ambazo zinasafirisha abiria kwa kutumia barabara inayoanzia eneo hilo kupitia katikati ya msitu huo hadi eneo la Mbezi, Barabara Kuu ya Morogoro.
Pori hilo lina ukubwa wa ekari 1,226 na kilometa za mraba 15.
Lilipewa hadhi ya kuwa Pori la Akiba baada ya kuzingatia vigezo mbalimbali na tafiti tofauti kubaini kuwepo kwa viumbe hai na aina za mimea adimu, zisizopatikana maeneo mengine.
Msitu wa Pande unazungukwa na vitongoji vya Mpiji Magohe, Kibesa, Msakuzi na Mbopo.
Hata hivyo, katika miaka ya karibuni pori hilo limejipatia sifa mbaya ya kutumika kama kichaka cha kutesea watu, mauaji na vituko mbalimbali.
Sifa hiyo mbaya ya pori hilo ilianza kuvuma mwaka 2006 baada ya wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge, mkoani Morogoro kuuawa na polisi katika eneo hilo kwa kilichoelezwa kuwa walidhaniwa kuwa ni majambazi.
Baada ya hapo Tume iliundwa kuchunguza tukio hilo, ikabainika kuwa waliouawa hawakuwa majambazi.
Askari waliohusika na maujai hayo walifunguliwa kesi, ambayo ilivuta hisia za wengi kutokana na unyeti wake na mazingira ya tukio lenyewe.
Mbali ya vituko vya hapa na pale vinavyoshuhudiwa na kusimuliwa na majirani wa msitu huo, mwaka huu ikiwa miaka sita tangu kuuawa wafanyabiashara wa Mahenge, pori hilo limezizima tena, baada ya kiongozi wa madaktari, Dk Steven Ulimboka kutekwa, kuteswa na kisha kutelekezwa katika msitu huo.
Jeshi la Polisi liliibuka kupitia Kamanda Kova kwa mara nyingine kuhusu swala hili likikemea kuhusu malumbano mbali mbali juu ya mjadala huu kati ya Taasisi za Dini za Kikristo na Jeshi la Polisi baada ya swala hili Kufikishwa katika Mahakama …Na haya ndio maswali ambayo tumekuwa tukijiuliza …

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu Dar es Salaam,Suleiman Kova
- Je Katiba Katiba inasemaje Juu ya Kujadili swala ambalo limefikishwa mahakamani ,Je linaruhusu upande mmoja kutoa taarifa na kuuzuia mwingine kujibu ?
- Je katiba inasemaje kuhusu mtu unaporipoti kituo cha Polisi juu ya mtu ambaye analeta fujo kwenye eneo lako?Je anapokamatwa wewe uliyepeleka taarifa unakuwa mtuhumiwa au mshutumiwa bila kuulizwa au kupewa taarifa?
- Je kama kuna uthibitisho juu ya kile kinachodaiwa kuhusu mtuhumiwa(Kanisa la Ufufuo na Uzima) kwanini hakisemwi mpaka mtuhumiwa anapolalamika ndipo wewe ujibu tena kupitia vyombo vya habari ?
- Je ni upi uwezo wa intelijesia yetu juu ya mambo kama haya …..haswa hizi issue za kupika?...Wako wapi waliorudisha fedha za EPA?Au ndio funika kombe mwanaharamu apite?Hapa ndipo unapokuja usemi kwanini walioko jela wengi ni maskini?
….Kumbuka kuwa hata mara zote mtu mkimiya anaponyamaza sio kuwa hana cha kusema bali hutumia busara na uvumilivu…Muda unapofika uvumilivu ukafikamwisho ndio haya sasa tunayoyaona….