Baada ya wiki Moja iliyopita kwenye Miji ya Dodoma Na Mbeya kutikiswa na tukio la Campus Night,Jana usiku(23/11/2012) ilikuwa ni zamu ya mji wa Singida kutikiswa na tukio hili Adhimu nchini Tanzania,Rise and Shine ndio ilikuwa theme mjini Singida,Baada ya blog hii kupata habari kutoka kwenye chombo cha kuaminika kwamba zaidi ya watu 700 waliamua kumpa Yesu maisha yao huku takribani watu yapata zaidi ya 5000 wakihudhuria kwenye tukio hili ambalo linatokea mara moja tu kwa mwaka

Pata Matukio katika Picha 



Hapa tupo Katika ya Safari kuelekea  Singida 
Victor & Chavala

Ndani Ya Singida

Costa Mbili Watu Full...

Watu Wakifanya Furaha za Shangwe kwa Bwana


Samuel Yonah... the best guitarist, composer, arranger of all times


Watu pipoz...


The audience Praising and dancing


Prosper ,Steve Wambura,and Chavala


Mungu wa Mapendo...


Students Joint Mass Choir


Papaa Ze Blogger(T-shirt Nyeupe) Mc wa Shughuli akienda sawa


Pastor Dr Huruma Nkone na Daniel a.k.a Kenge wakimsifu Mungu


The Mass Choir perfoming


Hata Baada ya Kumaliza Honey Moon siku chache zilizopita lakini  Steve Wambura hakuacha kumsifu Bwan


The Empire wakifanya Vitu vyao


700 peoples received Jesus


Steven Wambura a.k.a Le grand Mopao akiendesha jahazi
Kama kawa Swahiba Mc Pilipili Hakubaki Nyuma..Pasua Mbavu Singida


Rivers of Joy International wakienda Sawa kwenye Praise and Worship


Katika Yote Ujumbe Mkuu ulikuwa Hauwezi songa Mbele Bila Yesu...Yesu Ni Jibu La Mambo yote
Mara zote tumekuwa tukifanya vitu tukijua kwamba tupo sahahi lakini mara nyingi tumekuwa hatupo sahaihi kutokana na upeo wetu mdogo wa kufikiri vitu kwenye nyanja mbalimbali na athari mbali mbali zokanazo na vitu mbali mbali.Unapofanya kitu kwa fikra halisi na utimilifu wa mambo ndipo unaweza kugundua kwamba uko sahihi hapana mara nyingi matokeo mazuri ya kile ulichofanya ndio hutupa jibu kwamba input ambayo umeiweka/umeitumia ilikuwa sahihi au hapana.Maamuzi yetu  huadhiriwa na vitu mbali mbali na hutufanya tuwe sahihi au hapana kutokana na vitu hivyo.Kwenda Kanisani Hakukufanyi kuwa Mkristo na Wala Kusimama Karibu na Karakana ya Magari hakukufanyi kuwa Gari.

1.Mazingira

Mazingira tuliyokulia yanamchango mkubwa sana kwenye maisha yetu na huwa na athari kubwa juu ya vile vitu ambavyo tunaishi na na namna tunavyofanya maamuzi yetu.Mfano Siku Moja tulipokuwa Kanisa fulani...Mzungu alisimama akitoa ushuhuda kwamba Yaani Maisha Mabaya sana kwake na Amechoka Kula Kuku kila siku,Wakati aliposimama Mama mmoja akaeeleza namna ambavyo hawana chakula kabisa.Ukifwatilia kinachowatofautisha hawa watu ni mazingira waliyo kulia.Lakini pamoja na yote Mazingira yanaweza kukufanya uwe sahihi au hapana kutokana pia na mtazamo wako binafsi.....Kwenda Kanisani hakukufanyi kuwa Mkristo wala Kusimama karibu na Karakana ya Magari hakukufanyi kuwa Gari

2.Information 

Habari za kila siku ambazo tunazipata zinaathiri sana maisha yetu tunatoishi kila siku na katika nyanja tofauti tofauti embu fikiria kama tungekekuwa toka tumezaliwa kwenda shule isingekuwa ni lazima/kungekuwa na mfumo mwingine wa kusoma,Habari hizo ndizo zingekuwa chanzo cha namna tunavyofanya vitu vyetu na namna tunavyoralate na wengine na namna tunavyofanya maamuzi ya maisha yeyote kwenye maisha yetu.Fikiri kama tungeambiwa kula makande ni sumu toka tunazaliwa mpaka tulipo maamuzi yetu yangejengeka kwa namna hiyo bila kuzingatia maswala Mengine.Hembu fikiria kwamba tungekuwa tunambiwa Ukimwi hausababishi kifo na hauna madhara kwenye maisha yetu ya kila siku je ingekuwaje?

3.Watu

Marafiki,Ndugu na jamaa wanamchango mkubwa na maisha yetu katika kila tunachokifanya,Ndio maana wahenga walisema ukitembea na mwizi na wewe utakuwa mwizi basi si kama mwizi kwa asilimia zote bali lazima hata uamulie kuwa kibaka,Chuma hunoa chuma siku zote.Marafiki wanaokuzunguka wanamchango mkubwa sana kwenye maisha yako,Wataalamu wanasema ukitaka kujua pato la la mwezi kwene ajira yakeChukua marafiki wake watano wanaomzunguka kwa ukaribu sana,Tafuta wastani wao unaweza kujua pato lake la mwezi.Lakin pamoja na hayo yote ni vizuri kuaangalia marafiki ,ndugu na jamaa wanaotuzungumza wanamchango gani kwenye fikra zet na namna tunavyoishi kila siku.Haiwezekani ukatembea na Chizi wewe ukaonekana mwenye akili.

Pamoja na mambo yote unaweza ukawa umeathiriwa kwa namna mbaya kutokana na sababu hizo tatu za ambazo ndizo zimekuwa sehemu kubwa ya maisha yetu lakini kumbuka bado unaweza kufanya vizuri zaidi
Hata kama umefanya vibaya sana bado unaweza ukabadilika na kufanya vizuri zaidi...Kumbuka ...Kwenda Kanisani Hakukufanyi kuwa Mkristo wala Kusimama Karakana ya Magari Hakukufanyi Kuwa Gari..

...Kwenda Kanisani Hakukufanyi kuwa Mkristo wala Kusimama Karakana ya Magari Hakukufanyi Kuwa Gari..
Rising The Standard ndio ilikuwa kauli mbiu katika Campus Night iliyofanyika katika Mji wa Mbeya siku ya Ijumaa ya tarehe 16/11/2012 bila kusahau mji wa Dodoma nao uliendelea kutikiswa na Event hii ya Campus  Night yenye kauli mbiu My Life,My Love , My All.Naam matukio haya pacha yaliwakutanisha wanafunzi wa elimu ya vyuo mbalimbali katika maeneo husika

Kama ilivyo ada Mc maarufu wa Mji Papaa Sebene ndio alikuwa mshereheshaji wa Event iliyofanyika Mbeya naam...


Katika Segment ya Comedy Mc Pilipili alitikisa mji wa Mbeya,Kama ilivyo ada ya King Chavalla hakukosekana akiwaacha wanafunzi hoi kwa comedy

Wasemaji wa Siku hiyo katika Mji wa Mbeya walikuwa ni Pastor Dr Huruma Nkone,Rose Mushi,Dr Kimambo,Mr Msigwa na Dr Maboko,Wote hawa walizungumzia namna ya ku-rise Spiritual Standard pia na maisha ya kawaida tu ya mwamini katika eneo la uanafunzi



Pastor Dr Huruma Nkone alisema ushalobaro wala utoz toz na u-sista du haumsaidia mtu kuwa na clear future only Jesus can Transform your life na ata-rise standard zako..Kwa mara nyingine tulishudia Radical Gospel ya Dr Huruma Nkone isiyokuwa na kificho.

Nabii Mke a.k.a Rose Mushi alishusha sindano za kurise starndard zako kwenye swala la mahusiano.Alisisitiza kuwa bila Yesu mahusiano yako ni bureee...Alikazia akasema ni Bora uachuke kwa kumtii Mungu kuliko kuumtii mwanadamu.Kama ilivyo ada akiwa hana mic unaweza kumwangalia na kumfikiria unavyopenda..Kosa linafanyika tu pale akiwa na Mic....Ukumbi mzima ulikuwa moved na Nguvu ya Mungu through Rose Mushi.

Dr Kimambo aliongelea swala la Academic and Execellence pindi uwapo shule pia..Akatoa kanuni na mfumo wa namnq ya kurise standard zako na namna ya ku-execel academically..It was more than Powerfully...Kama ulimisi hii na wewe ni mwanafunzi wa mji wa Mbeya pole.Katika yote aliyoongea alisema huwezi fanya chochote bila Yesu.

Dr Maboko aliendelea kuongelea swala Ujasiriamali kwa wanafunzi,alijaribu kushare expirience yake katika swala zima la ujasiriamali bila kusitasita alieleza namna ya kurise standard zako katika swala zima la fedha huku ukiwa bado ni mwanafunzi.Lakini mwisho wa Yote alisema ukitaka kurise standard zako ,Yesu ni jibu la lako.

Mr Msigwa .a.k.a Branch Manager wa CRDB Mbozi mjini,aliendele kusema zaidi kuhusu Mahusiano na Changamoto ambazo kama vijana tunazipitia alieeza namna bora ya kupata mke au mume ambaye anaweza akakufaa na ukaendela kuonekana kuwa bado wewe ni bora na unafanya vizuri kati maswala mengine ya maisha pia
Rose Mushi a.k.a Nabii Mke akiendelea kufwatilia nini kinachoendelea kwenye Campus Night

Pastor Dr Huruma Nkone akeendela kukata Gospel ya ulweli

Music Director Pastor Mathew Sasali pamoja na Mama Pastor Rebecca Sasali wakiongoza jukwaa la Praise and Worship 

Sauti ya Dubu ukipenda Mr Dr Nyanda akiwa kazini kama Mc wa siku hiyo

Praise and Worship chini ya Mama Pastor ikifanya kaziii.....

Watu Pipoz

Sebene ya Yesu ikiwafanya watu wadance

Twende Sawa

Watu Pipoz

Moja ya Matunda ya Campus Night zilizopita akitoa ushuhuda

Mc Shupavu a.k.a Papaa Ze Blogger akiendelea na Kaziii

Twende Sawaaa

Makofi kwa ajili ya Yesuu!!!

Twende Sawa

Pastor  Dr Huruma Nkone akiendelea kukata Gospel kama Katapila

Wanafunzi wakimpa Yesu Maisha yao

Wanafunzi wakimpa Yesu Maisha yao

Dr Kimambo akikata shule 

Watu Pipoz

Nabii Mkee akitabiria Watu

Haikuwa Ya kitoto hata Vice President wa Mzumbe Campus ya Mbeya alikuwepo(Mwenye Top ya Kijani)

Mc Pilipili akiwa Kazini

Dr Maboko akiendelea kuongelea Ujasiriamali

Mr Msigwa akiendela kukata shule ya Mahusiano

King Chavalla akipasu mbavu za watu
Hembu angalia huu umati hapa karibia na Saa kumi na moja asubuhi..lakini watu wapo tuu

Hitimisho katika Jumbe zote zilizoongelewa katika Campus Night hizi ni kwanmba Yesu ndio jibu la kila kitu kwenye kila idara ya maisha na kila kona .Yeye ndio mwanzo tena ni mwisho wa kila jambo.
Leo katika segment ya Punch of The Week tunaendelea kujadili mambo mbali mbali ambayo yanaweza kutusaidia kubadilisha mfumo wetu wa kufikiri na namna ambavyo tunaweza kuangalia vitu kwa namna ya pekee.

Tanzania ni moja ya nchi ambayo imebahatika kuwa na rasilimali nyingi sana za aina tofauti tofauti katika kila nyanja lakini sisi watanzania tumekuwa tukiendelea kubaki katika hali ya kutojitambua na kuendelea kulaumu mifumo mbali mbali katika uendeshaji wa vitu.Lakini cha Kushangaza Pindi wageni wanapokuja ndani ya nchi wanatumia rasilimali tulizo nazo na wanapata upenyo wa kufanikiwa huku tukiendela kuwaona kama wachawi.Kumbuka unapokiona wewe kitu hakifai na kukidharau au kutokuwa na mtazamo sahihi ndipo inakuwa nafuu kwa mchukuzi.Kuvuja kwa pakacha ya nafuu ya mchukuzi.

Katika eneo hili tumejaribu kuangalia mambo machache amabayo yanaweza kukusaidia kuweza kujitambua kuweza kusonga mbele katika maisha yao bila woga na kujidharau huku ukijua faida yake katika siku zijazo.Ukiwa kama ndugu,jamaa,rafiki,unaweza ukaamua kufanya mabadiliko yako mwenyewe bila kushurutishwa wala kulazimishwa na mtu.

1.Social Yardstick(VIpimo vya Kijamii)
Muda mwingine kwenye maisha yetu tumeshindwa kuzitumia fursa ambazo tunazo sababu tumetumia jamii kama sehemu ya kipimo chetu cha kuendesha mambo na vitu vyetu.Mfano Utasikia "Yaani mtoto wa fulani hakufanikiwa na alikuwa na akili sana wewe ndio utafanikiwa?.Unaposikia ivyo mara njingi watoto wetu wamedumaa na hata akili zetu zimeduma tumeshindwa kujua watu wengine ni wengine na sisi ni sisi.Jaribu wewe mwenye usitumie mtu mwingine kama kipimo chako cha maendeleo."CHEZA MUZIKI KUTOKANA NA MDUNDO UNAOUSIKIA KICHWANI MWAKO NA SIO HUO UNAOUSIKIA KWA JIRANI YAKO"
Kuitumia jamii kama kipimo chako cha kuendesha vitu ni makosa jaribu kutumia uwezo wako na nguvu zako ili kuweza kupiga hatua kwenye nyanja nyingi za maisha yako binafsi hata ya familia yako.”Mfano…”Mara nyingi familia nyingi zimetumia watoto wengine kama kipimo cha malezi kwa watoto wa familia zao na sio wao kama wao wanaweza kulea na kuwakuza watoto wao,uzuri au ubaya wa mototo hautokani kuwa mototo wa jirani yako ni mzuri au mbaya.

 2.Comparison(Kujilinganisha)
Hili limekuwa miongoni mwa matatizo makubwa kwa tumetumia watu wengine kama sehemu ya kipimo cha mafanikio Fulani ingawa si vibaya kujua mwingine anafanya nini.Unapotumia muda mwingi kujilinganisha na mwingine unapoteza uwezo wako halisi wa kufanya vitu katika uwanda mpana wa maisha yako.Kumbuka kila mtu ana maono na ndoto zake kwenye maisha yake unapojaribu kuwa kama yeye unaishi maisha yake wakati wewe sio yeye.Jifunze kuishi maisha bila kujilinganisha linganisha na wengine maisha ni kujaribu kutumia fursa zilizopo.Kumbuka unaweza ukafanya ziaidi kuliko mtu unayejilinganisha naye kwa kufanya ziaidi vizuri sana.
Unaweza ukajikuta unafanya vitu chini ya kiwango kumbe uwezo wako unaweza ukawa ni mukubwa zaidi ya hapo.
“Fikiria Steve Paul Jobs au Bill Gates wangejilinganisha bila kila mmoja wao kuaamua kuishi kama yeye leo kuna baadhi ya vitu ambavyo tungekuwa tunakosa kwenye Ulimwengu huu.

 "CHEZA MUZIKI KUTOKANA NA MDUNDO UNAOUSIKIA KICHWANI MWAKO NA SIO HUO UNAOUSIKIA KWA JIRANI YAKO"
Mara nyingi tumekuwa na hulka ya kurahisisha vitu kuliko ulivyo uhalisia wa vitu kwenye shughuli zetu za kila siku.Mara nyingi tumedharua vitu sababu hatujui gharama ya vitu hivyo kwenye maisha ya watu wengine na uhalisi wa shughuli hizo wanazozifanya.Sisi tunakuja kuona matokeo ya mchakato mkubwa sana ambao wamekuwa nao kwenye maisha yao na kazi zao za kila siku.Mfano "Ni Rahisi kumuona Konda anakusanya nauli kwenye Daladala ukamjibu/kumwangalia kwa kumdharau lakini hujui mpaka ameumua kufikia hapo amepitia nini pia hatujui gharama halisi ya kufanya kazi hiyo sisi tunaona matokeo tu ya kukusanya fedha muda huo,Kama ni rahisi basi jaribu kuifanya wewe utaelewa...."Laini Laini Maana yake Sio Rahisi"

Kondakta wa Mwenge Posta Via Shekilango Road
Ni rahisi kumuona mwingine amekosea kulio wewe kujiona umekosea.Watanzania tulio wengi tuna kipaji cha kukosoa kuliko kurekebisha kwenye kile mtu anachokosea.Mara nyingi huwa tunaona matokeo tu ya kile mtu anachokianya ndio maana tunapenda kukosoa Mfano"Ni Rahisi kumkosoa mchezaji wa mpira kuwa amekosea angepiga vile angefunga"Lakini tunasahau Gharama ya mazoezi anayoyafanya kufikia pale ni kubwa kama ingekuwa ni rahisi ungeamua kuwa mchezaji then tuone kama utakosoa au hapana.Kokosea sio tatizo lakini punishment tunayotoa haiendani na kosa lenyewe.Laini Laini Maana yake Sio Rahisi
Christiano Ronaldo
Sisi ni wavivu wa kufikiria mara nyingi,Hatupendi kufwatilia vitu ndio maana tunakuwa wepesi wa kuchukukia vitu vyote kuwa ni rahisi sana kumbe sivyo vilivyo kwenye uhalisia."Mfano...Makampuni ya simu yanapotoa matangazo yao wanakwambia hudumu fulani ni Bure,Je kweli ni Bure ?Je kwanini Baada ya kumaliza kutangaza utasikia "VIGEZO NA MASHARTI VITAZINGATIWA"Je hivi vigezo na masharti kuzingatiwa ni vipi?Basi kwa maana nyingine kuna gharama ya kulipa inaweza isiwe pesa lakini inaweza kuwa gharama ya kufwata vigezo na masharti inaweza kuwa kubwa zaidi.

Soma Chini kwenye picha kwenye Maandishi yamezungushiwa na alama Nyeusi

Wakati Steve Jobs anaanza kumpuni yake ya kwanza Apple akiwa Garage kwao na Mzee Paul Jobs ilikuwa ni rahisi sana kuwadharau kwa sababu huakuweza kufikiria mafanikio ambayo leo wangekuwa nayo.Watu wengi leo tunapenda kufurahia mafanikio ya wengine kitu ambacho si kibaya lakini hapo hapo tunayakosoa kwa kusema ningekuwa mimi ningefanya hivi na vile.ni bora ukae kimiya sababu hakuna mtu anayependa kukosea kwenye maisha kila mtu anapenda kufunya vizuri katika kila kona ya maisha pia kumbuka picha ya ndoto ya mtu anayo mtu mwenyewe na sio mwingine.Gharama ya mtu alolipa mtu mpaka tunafika kuona mafanikio sio ndogo.Leo tunatouch to Ipad na tunafurahia Simu za Iphones lakini haukumbuki kuna mtu alilipa gharama.Laini Laini ya kubofya Ipad na Simu za Iphones haimaanishi ni Rahisi.
Steve Jobs 
Ni vizuri kuwa na mtazamo halisi na gharama halisi na kile unachotaka kukifanya lakini pia ni muhimu kujua vya wengine na gharama za vile vitu wanavyofanya kuliko kukurupuka na kuanza kufikiria katika namna tofauti na jinsi uhalisia wa vitu ulivyo.Penda kufwatilia vitu vizuri kwanza ndipo ufikie kufikia kuhitimisha huku ukiwa na uhakika wa kile unachotaka kukifanya

...........................................Laini Laini maana yake sio Rahisi......................................
Watanzania na jamii yetu kwa ujumla tumejengwa na kukuzwa zaidi katika hali ya kupenda kufikiria kushindwa kuliko kushinda katika maisha yetu na kila siku kutokana  na malezi na namna mfumo wa vitu vingi wa maisha unavyoendeshwa.Mfumo wa maisha yetu tangu tunaanza tungu nyumabani tukiwa wadogo na hata tunapoanza shule mazingira yetu hayaamini katika kushinda kuliko kushindwa.Kujiamini katika kila tunachofanya ni kama umekuwa mzimu ulio hai unaosumbua maisha yetu tangu tungali wadogo mpaka watu wazima.Muda mwingine tumejitungua misemo ambayo ukifwatila haina mashiko zaidi ya kutaka kutuondoa uoga tu na sio zaidi...."Tukiwezeshwa Tunaweza".Swali la msingi je hao waliweza waliwezeshwa na na nani na wana vichwa vingapi na wamewezaje kufika hapo.
Tukiendelea kwa namna hii safari ya ukombozi katika nyanja mbali mbali yaani Kifikra,Kiuchumi,Kijamii,Kisiasa na hata kidini itakuwa ni kama kumtafuta kuku anayenyoshesha tukitaka atupatie maziwa....


 Mambo machache ambayo yanaweza kutufanya tupende kufikiria  katika kushindwa zaidi kuliko katika kushinda................


1.System(Mfumo)
Mfumo wetu wa malezi kuanzia watoto na hata mfumo wa uongozi katika nchi yetu katika nyanja mbali mbali hauutupi mwanya wa kuweza kufikiria na kuamini katika kushinda katika kila tunalolifanya zaidi ya kufikiria na kupenda kushindwa zaidi bila ya sisi wenyewe kujua nini tatizo limeanzia wapi.
             
Pamoja na mfumo mbovu katika kila nyanja ya maisha yetu ambao tumekutana nao sio kigezo cha kutufanya iwe kisingizio kwamba tusiamini katika kushinda zaidi ya kufikiria katika kushinda.."System haipo kwa ajili ya walio nje ya system bali system ipo kuwapa favour  wale waliopo kwenye system tu"Ni jukumu lako kuamua kubadilisha mfumo wako mwenyewe kwenye fikra zaidi kuiko kuendelea mfumo sababu utaishia kulaumu tu na hautafika kokote.

2.Historical  Background(Maisha yetu na Historia za Nyuma)

Familia zetu nyingi za kiafrika haziamini katika kushinda zaidi kuliko kushindwa.Ni familia bora na chache sana ambazo zinaweza kuamini katika kushinda kuliko kushindwa tangu tukiwa wadogo..Familia nyingi zimekuwa na mtazamo hafifu tangu watoto wanapoanza shule kuanzia maneno wanayotakiwa mpaka matendo wanayofanyi katika nyanja mbali mbali hii haikupi njanya ya kufikiria na uwanda mpana wa kuamini ushindi unawezeka..utasikia wanasema ..."Yaani Baba yako aliishia hapo ,Babu hapo hapo,Mimi mwenyewe mama yako pamoja na wote sisi kuwa na akili kwenye ukoo wetu bado nimeishi hapo ...je wewe utaweza au ndio unajifanya una akili sana?"Wanashindwa kujua wao ni wao na sisi ni sisi kwani kuna vitu vingi vimebadilika sana.
          
Ndio utasikia hata mtu akishindwa kwenye jambo dogo tu...Yaani sisi sijui tunamikosi gani....Yaani hii ni tatizo kubwa katika jamii...wewe ndio mkosi wa kwanza wa kushindwa kufanya maamuzi sahihi.


3.Relationship Break ups.

Katika kizazi chetu kutokana na sarakasi nyingi za kimahusiano ambazo tumekuwa zikitupata kwa kuvunjika na kushindwa kuwa na mahusiano bora ya kimapenzi imetupelekea kushindwa na kujiamini katika kila tunachokifanya.Huu msuko suko wa kupiga vibuti na kupigwa vibuti(Kuacha na Kuachwa) limekuwa ni tatizo kubwa la kufanya watu wengi kutosonga mbele na kupiga hatua mpya katika maisha yetu ya kila siku.
                         
Mara tu anapoonza kugika hatua mpya ndani yake bado anasutwa unasikia maneno haya "lakini wewe umeachwa na sijui kama utapendwa tena".Matokeo yanayopelekea watu kujitungia maneno ya ambayo hayana hata mashiko na uelewa timamu.Utasikia watu wanasema."Wanaume wote si sawa..yaani wote baba na mama mmoja au Wanawake wote si wale wale".Ukisikia mtu anasema hivyo fwatilia yaani kuna sehemu katendwa.

4.Past Failures.

Baada ya watu kuweza kushindwa katika maisha yetu katika kipindi fulani cha nyuma imepelekea mioyo yetu kushindwa kujiamini katika kila hatua mpya ambayo tunataka kuichukua ili kuweza kuendelea mbele.Kushindwa katika jambo fulani katika kipindi cha nyuma haina maana ya kwamba hauwezi kushinda katika jambo lingene katika maisha....Mfano "Watoto wengi wakifeli Kidato cha Nne huamini kuwa maisha yameishia hapo kumbe maisha bado yanaendelea ."
                     
Kumbe ni wakati wakujaribu fursa mpya za kimaisha na mambo Mengine.Imekupasa kujaribu tena katika kila unachokifanya hata kama ulishindwa nyuma hiko sio kigezo kwamba utashindwa tena na wala sio sababu ya msingi ambayo unaweza ukaeleza watu.Fanya tena na tena...

"Mbunge wangu wa Ubungo Mh.John Mnyika alipojaribu mwaka 2005 kugombania Ubunge kwenye jimbo la Ubungo alishindwa lakini hiyo haikuwa tiketi ya kukata tamaa matokeo yake mwaka 2010 alijaribu tena..ndipo ushindi ulipopatikana..Leo hii tunachekelea na kufurahia kumbe ni hatua ya mtu aliyoamua kuchukua maamuzi mwenyewe.

........Jenga tabia ya  kufikiria kushinda zaidi kuliko kushindwa zaidi...
Wanafunzi wengi wa Jamii ya Kitanzania tumejengewa mfumo ambao haupendi/hatupendi kujifunza na kutafuta mafundisho nje ya masomo yetu haswaa kipindi tukiwa kwenye vyuo na shule lakini sisi wenyewe tumeshindwa kutafuta upenyo wa kujifunza nje ya maisha ya shule kwa sababu moja au nyingine.....Lakini safari hii Kanisa la Victoria Christian Center Tabernacle a.k.a VCCT limeamua kukuletea Seminar yenye Jina SHAPING YOUR DESTINY chini ya Kitengo cha kanisa hilo kinachoitwa CAMPUS MINISTRY.
Usafiri utatolewa Bure kutoka kwenye vyuo vyote hapa Dar es Salaam mpaka eneo la Tukio katika Hema la Kisasa la Kanisa hilo Mbezi Beach.......
Topic zitakazokuwa presented.......!!!

1.How to Live a Balanced 
2.Discovering Talents and Opportunities while in a College
3.Maintaining and Building Meaningful Relationship
4.How to Excel In and Out Of The Class 

Presenter are :-


Pastor Dr Huruma Nkone
Chris Mauki
Samuel Sasali a.k.a Papaa Ze Blogger
John Lisu





















                                       




DONT DARE TO MISS !!!!!!!!!
| |
| |